Monday, December 30, 2019

MENEJIMENT YA TMA YAJIPANGA UTEKELEZAJI WA SHERIA YA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA

Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), Dkt. Agnes Kijazi katika picha ya pamoja na washiriki wa kikao kazi cha kujenga uelewa na mkakati wa utelezaji wa sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa kilichofanyika Kibaha, Tarehe 27-28 Desemba 2019.
Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), Dkt. Agnes Kijazi akizungumza na washiriki wa kikao kazi cha kujenga uelewa na mkakati wa utelezaji wa sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa kilichofanyika Kibaha, Tarehe 27-28 Desemba 2019.
 Mwanasheria wa TMA Ndugu, Emmanuel Ntenga akifafanua baadhi ya vifungu vya sheria kwa washiriki wa kikao kazi cha kujenga uelewa na mkakati wa utelezaji wa sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa kilichofanyika Kibaha, Tarehe 27-28 Desemba 2019.
 Mkurugenzi wa Ofisi ya Zanzibar-TMA, Ndugu, Mohamed Ngwali akizungumza katika kikao kazi cha kujenga uelewa na mkakati wa utelezaji wa sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa kilichofanyika Kibaha, Tarehe 27-28 Desemba 2019.
Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri-TMA, Dkt. Hamza Kabelwa akizungumza katika kikao kazi cha kujenga uelewa na mkakati wa utelezaji wa sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa kilichofanyika Kibaha, Tarehe 27-28 Desemba 2019.
Mkurugenzi wa Utafiti na Matumizi-TMA, Dkt. Ladislaus Chang'a akizungumza katika kikao kazi cha kujenga uelewa na mkakati wa utelezaji wa sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa kilichofanyika Kibaha, Tarehe 27-28 Desemba 2019.
Mkurugenzi wa TEHAMA na Huduma za Ufundi-TMA, Dkt. Pascal Waniha akizungumza katika kikao kazi cha kujenga uelewa na mkakati wa utelezaji wa sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa kilichofanyika Kibaha, Tarehe 27-28 Desemba 2019.
Meneja Rasilimali Watu Bi. Mariam Is-Haaq akizungumza katika kikao kazi cha kujenga uelewa na mkakati wa utelezaji wa sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa kilichofanyika Kibaha, Tarehe 27-28 Desemba 2019.
Washiriki wakizungumza katika kikao kazi cha kujenga uelewa na mkakati wa utelezaji wa sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa kilichofanyika Kibaha, Tarehe 27-28 Desemba 2019.

Kibaha, 28 Desemba 2019;

Menejimenti ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imefanya kikao kazi kwa siku mbili ili kupitia kwa pamoja na kupata uelewa wa namna bora ya utekelezaji wa sheria Na. 2 ya mwaka 2019 ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.

Akizungumza wakati wa kufunga kikao kazi hicho, Mkurugenzi Mkuu wa TMA na mwenyekiti wa kikao aliwataka wakurugenzi na mameneja kujenga utamaduni wa utendaji kazi wenye lengo la uboreshaji huduma ilikufikia malengo ya Mamlaka katika utekelezaji wa sheria iliyopo. Aidha, aliwapongeza na kuwashukuru washiriki wa kikao kazi hicho kwa jinsi walivyojitoa kuifanya kazi hiyo kwa umakini mkubwa kwa zaidi ya saa kumi na mbili za kazi kila siku pasipo mtu yoyote kuondoka.

‘Nataka baada ya kikao hiki viongozi wote muwe mstari wa mbele katika kuhakikisha watumishi mnaowasimamia wana fahamu sheria, taratibu na kanuni kwenye utekelezaji wa majukumu yao kwa maslahi ya Mamlaka na Taifa kwa ujumla’. Alizungumza Dkt. Kijazi.

Awali, akifungua kikao kazi hicho Dkt. Kijazi aliwapongeza wafanyakazi wote wa TMA kwa utendaji mzuri wa kazi uliopelekea kufanikiwa kukishikilia cheti cha ubora cha ISO 9001:2015 baada ya ukaguzi uliofanyika kati ya tarehe 16 na 20 Disemba, 2019 ambapo TMA ilikaguliwa na Mkaguzi wanje kutoka Canada.

Kikao kazi hicho kiliwakutanisha Mkurugenzi Mkuu, wakurugenzi, Mkurugenzi Ofisi ya Zanzibar, Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Hali ya Hewa- Kigoma, mameneja kutoka makao makuu, mameneja wa Kanda na wanasheria wa TMA.

Awali, wajumbe walipitia vifungu vyote vya sheria na kujadili kwa kina ili kuhakikisha viongozi wote wa Mamlaka wanakuwa na uelewa wa pamoja wa sheria hiyo ili kurahisisha utekelezaji wake katika maeneo yao ya kazi na hivyo kuchangia katika ustawi wa maendeleo ya nchi kupitia sayansi ya hali ya hewa.

Aidha, wajumbe hao waliainisha maeneo ya uboreshaji katika kanuni hususan kwenye udhibiti wa huduma za hali ya hewa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ukusanyaji mapato, utoaji huduma za hali ya hewa kwa usahihi na kwa wakati pamoja na kutoa elimu kwa umma na wadau kuhusu sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania. 

‘Tunapaswa kutoa elimu kwa umma hasa wale wadau ambao wanamiliki vituo vya hali ya hewa watambue kwamba ni kosa kisheria kuwa na vituo ambavyo havijasajiliwa na pia kutumia vifaa ambavyo havijahakikiwa (calibration) na TMA’ . Alisema Dkt. Kijazi.

Naye Mkurugenzi wa Ofisi ya Zanzibar-TMA, Ndugu. Mohamed Ngwali akitoa salamu za shukrani kwa niaba ya washiriki wote, alimshukuru Mkurugenzi Mkuu wa TMA kwa kufanikisha kikao kazi ambacho kimeongeza uelewa mpana wa matumizi ya sheria mpya ya TMA na kuahidi kudumisha umoja katika utendaji kazi kwa watumishi wote.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...