Sunday, September 1, 2019

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) wakati akifungua kikao kazi kilichowakutanisha wanasayansi wa hali ya hewa (meteorologists) ili kujadili rasimu ya utabiri/mwelekeo wa msimu wa mvua za vuli Oktoba hadi Desemba 2019 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza, Dar es Salaam, Tanzania.





Matukio mbalimbali katika picha wakati kikao kazi kilichowakutanisha wanasayansi wa hali ya hewa (meteorologists) ili kujadili rasimu ya utabiri/mwelekeo wa msimu wa mvua za vuli Oktoba hadi Desemba 2019 kikiendelea. Kikao kazi kilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza, Dar es Salaam, Tanzania.


Tarehe 29/08/2019: ‘Kupitia kikao hiki natarajia kiwango cha usahihi wa utabiri wa msimu huu wa VULI kitakuwa juu zaidi ya misimu yote’, alisema Dkt. Kijazi, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Makamu wa tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) .

Alisema hayo wakati wa kikao kazi kilichowakutanisha wanasayansi wa hali ya hewa (meteorologists) ili kujadili rasimu ya utabiri/mwelekeo wa msimu wa mvua za vuli Oktoba hadi Desemba 2019 .

Aidha, Dkt. Agnes Kijazi alisisitiza kwa kuwajulisha washiriki hao kuwa TMA inategemea kuzinduliwa rasmi kutoka ‘Agency’ kwenda ‘Authority’ tarehe 05 Septemba mwaka huu, hivyo ni vyema wakatambua kwamba wanapaswa kufanyakazi kwa bidii ili kukidhi mategemeo ya wadau. Alisema, kazi kubwa waliyonayo kwasasa ni kuhakikisha mwelekeo wa msimu wa mvua za vuli 2019 unakuwa wenye manufaa na tija kwa watumiaji kwa kwa na usahihi na usambazaji wa viwango vya juu zaidi. 

TMA imewakutanisha wanasayansi kutoka vituo vyake mbalimbali nchini ikiwa ni mwendelezo wa utamaduni wake wa utendaji kazi wa pamoja. Mwelekeo wa msimu wa mvua za vuli 2019 utatolewa rasmi  tarehe 03 Septemba 2019.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...