Tanzania Meteorological Authority
Friday, March 20, 2026
Tuesday, March 17, 2026
MHE. KAKOSO ATOA WITO KWA WATANZANIA KUFUATILIA NA KUZINGATIA TAARIFA ZA HALI YA HEWA.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Mhe. Selemani Kakoso (MB) ametoa wito kwa watanzania kufuatilia na kuzingatia taarifa za hali ya hewa kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), kwa kuwa ni muhimu katika kupanga na kutekeleza mipango na shughuli katika sekta zote za kiuchumi na kijamii hapa nchini, aliyasema hayo wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu katika ofisi ya TMA, Dar es Salaam.
“Natoa wito kwa Watanzania kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri zinazotolewa na TMA kabla ya kuanza kutekeleza majukumu yenu katika sekta zenu ikiwemo kilimo, maji au kibiashara kwa kuwa TMA imekuwa ikitoa taarifa za uhakika kila siku kupitia vyombo mbalimbali vya habari. Kutokana na ubora na ufanisi wa huduma zao, na weledi na umahiri wa wataalamu wake, TMA wameaminiwa kutoa misaada ya kitaalamu kwa baadhi ya Taasisi za hali ya hewa katika nchi mbalimbali barani Afrika.” Alisisitiza Mhe. Kakoso
Kupitia ziara hiyo yenye lengo la kukagua miradi inayotekelezwa na TMA, kamati ilipata fursa ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Ofisi ya TMA Kanda ya Mashariki na Kituo cha Tahadhari ya Matukio ya Tsunami pamoja na Kituo cha Taifa cha Uhakiki wa vifaa vya hali ya hewa na baadaye Mamlaka ilielekezwa kuongeza jitihada za usimamizi katika kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa kwa kuzingatia matakwa ya mkataba.
Naye Waziri wa Uchukuzi mwenye dhamana ya kusimamia sekta ya hali ya hewa Prof. Makame Mbarawa (MB) alisema Serikali ya awamu ya sita itaendelea kuwekeza kwenye sekta ya hali ya hewa na kuisimamia kwa karibu. Mh. Mbarawa aliahidi kufuatiilia kwa karibu kuhakikisha kuwa fedha zinazohitajika kwa ajili yya ukamilishaji wa miradi hiyo muhimu ya ujenzi wa miundombinu ya huduma za hali ya hewa zinapatikana kwa wakati.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu, TMA na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi, Dkt. Ladislaus Chang’a aliishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kwa kuwa sababu mafanikio ya TMA yamechagizwa pia na mchango mkubwa wa kamati kutaka kuona changamoto za TMA zinatatuliwa, kupitia maelekezo mbalimbali waliyokuwa wanatoa kwa nyakati tofauti.
“Kupitia ziara ya mwaka 2022 Mwanza, kamati hii iliiongezea nguvu TMA katika kuhakikisha tunaimarisha miundombinu ya hali ya hewa ikiwemo ukamilishaji wa rada 5 za hali ya hewa, mitambo mbalimbali ya kiutendaji, ongezeko la rasilimali watu pamoja na kujengewa uwezo wa kiutendaji wataalam wa hali ya hewa” Alisema Dkt. Chang’a
Dkt. Chang’a aliishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuiwezesha Mamlaka katika utekelezaji wa miradi miwili ya ujenzi wa jengo la Ofisi ya TMA Kanda ya Mashariki na Kituo cha Tahadhari ya Matukio ya Tsunami, ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 65 pamoja na ujenzi wa Kituo cha Taifa cha Uhakiki wa vifaa vya hali ya hewa ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 40. Kukamilika kwa miradi hii miwili kutaifanya TMA kuwa katika nafasi nzuri ya kuwa kitovu cha kuhakiki vifaa vya hali ya hewa hadi Ukanda wa Afrika.
Sunday, March 8, 2026
WANAWAKE WA TMA WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI 2026, KWA KUFANYA SHUGHULI ZA KIJAMII.
WANAWAKE WA TMA WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI 2026, KWA KUFANYA SHUGHULI ZA KIJAMII.
Wanawake wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) wameadhimisha Siku ya Wanawake Duniani katika mikoa mbalimbali nchini Tanzania kwa kufanya shughuli tofauti za kijamii zinazolenga kuimarisha mshikamano na kusaidia jamii.
Maadhimisho hayo yalifanyika kwa kuzingatia kaulimbiu ya mwaka huu isemayo: “Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana; Msingi Jumuishi kufikia Dira ya Maendeleo 2050.”
Katika Mkoa wa Dodoma, watumishi wanawake wa TMA walipata fursa ya kutembelea Kituo cha Watoto Yatima cha Safina kilichopo Ntyuka, ambapo walikutana na watoto wanaolelewa katika kituo hicho na kuwapa faraja pamoja na kuwasaidia kwa mahitaji mbalimbali.
Ziara hiyo ililenga kuonesha upendo, mshikamano na kuwapa matumaini watoto wasiokuwa na wazazi au wale wanaoishi katika mazingira magumu.
Sunday, March 1, 2026
DKT CHANG’A AFANYA MAZUNGUMZO NA KATIBU MKUU WA SHIRIKA LA HALI YA HEWA DUNIANI (WMO)
Tuesday, February 24, 2026
TMA, UDSM ZAIMARISHA MAHUSIANO YA KITAALAM NA KITAALUMA
TMA, UDSM ZAIMARISHA MAHUSIANO YA KITAALAM NA KITAALUMA
Dodoma, Februari 18, 2025.
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wamejadiliana namna ya kuimarisha ushirikiano wa kitaalam na kitaaluma kwa lengo la kuimarisha taaluma na sayansi ya hali ya hewa ili kuchangia katika kuboresha huduma za hali ya hewa nchini.
Majadiliano hayo yamefanyika katika kikao maalum kilicholenga kuangalia maeneo ya ushirikiano uliopo na namna ya kuuboresha, hususan katika matumizi ya tafiti zinazofanywa na UDSM kuhusiana na masuala ya hali ya hewa na mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi.
Akifungua kikao hicho, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC), Dkt. Ladislaus Chang’a, alieleza kuwa ushirikiano kati ya taasisi hizo umedumu kwa muda mrefu na kikao hicho kimeweka mkazo katika kuimarisha maeneo mahsusi ya ushirikiano huo, ikiwemo kuimarisha uelewa na matumizi ya akili mnemba (AI) katika utafiti na huduma za hali ya hewa.
Akiongea wakati wa uwasilishaji wake Dkt. Paul T. S. Limbu Mhadhiri Mwandamizi wa Meteorolojia na Sayansi ya Hali ya hewa katika Idara ya Fizikia, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) amesema kwa zaidi ya miaka 13 ya kufundisha masomo ya hali ya hewa, bado kuna haja ya kuendelea kuimarisha zaidi ushirikiano kati ya UDSM na TMA.
Tunawashukuru sana TMA kwa kushiriki na kutusaidia katika mchakato wa kuboresha mitaala, ufundishaji na usimamizi wa tafiti.
Pia ameeleza umuhimu wa wanafunzi kupata elimu kwa vitendo kupitia ziara za kitaaluma katika miundombinu ya TMA, fursa za kujitolea baada ya kuhitimu, pamoja na ushiriki wa TMA katika uandaaji wa vitabu vya kufundishia .
Aidha, pande hizo zimejadili ushiriki wa UDSM katika warsha, semina na maadhimisho ya siku muhimu kama Siku ya Hali ya Hewa Duniani ili kuwajengea wanafunzi uzoefu wa moja kwa moja katika mazingira halisi ya kazi.
Kwa ujumla, kikao hicho kimeweka msingi wa kuendeleza mazungumzo ya kitaalam yatakayosaidia kuunganisha tafiti, elimu na utekelezaji katika kuboresha huduma za hali ya hewa nchini.
Thursday, February 12, 2026
SERIKALI YATENGA BILIONI 13 KUWEZESHA UJENZI WA OFISI ZA TMA.
SERIKALI YATENGA BILIONI 13 KUWEZESHA UJENZI WA OFISI ZA TMA.
Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Mhe. David Kihenzile, ametembelea ujenzi wa ofisi za Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) zilizopo Sinza Simu 2000, jijini Dar es Salaam. Ujenzi huu, unaofadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, unalenga kuongeza ufanisi wa utoaji wa taarifa sahihi za hali ya hewa.
Akizungumza katika ziara hiyo,Naibu Waziri wa Uchukuzi,Mhe.David Kihenzile amesema Serikali ya Awamu ya Sita imetenga takribani shilingi bilioni 13 kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za TMA. Miradi hiyo inahusisha ujenzi wa jengo la kisasa la Kanda ya Mashariki na Utoaji Tahadhari za Hali ya Hewa pamoja na kituo cha tahadhari za Tsunami nchini,pamoja na Kituo cha Taifa cha Uhakiki wa Vifaa vya Hali ya Hewa (National Meteorological Calibration Centre) kitakachosaidia kukagua na kuboresha vifaa vya hali ya hewa.
Mhe. Kihenzile amesema majengo yote mawili, yaliyoanza kujengwa mwaka 2023 na 2025, yanatarajiwa kukamilika kabla ya mwisho wa mwaka huu. Ameeleza kuwa miradi hiyo itaongeza ufanisi katika utoaji wa taarifa za hali ya hewa na kuwawezesha wataalamu kufanya kazi katika mazingira bora na ya kisasa.
Kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi,Mhe.David Kihenzile (MB), ametoa rai kwa Bodi na Menejimenti ya TMA kusimamia miradi hiyo kwa weledi, uzalendo na kuhakikisha inakamilika kwa wakati na kwa ubora uliokusudiwa.Aidha aliipongeza TMA kwa kumchagua mkandarasi wa ndani, Chuo cha DIT (Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam), kutekeleza miradi hiyo akieleza kuwa hatua hiyo inachochea maendeleo ya wataalamu na taasisi za ndani.
Pia,Naibu Waziri amewahimiza TMA kutoa taarifa kwa wakati ili kuwasaidia wananchi katika shughuli za kila siku zikiwemo usafiri, kilimo na matumizi ya bahari na amewahimiza wananchi kuendelea kuamini na kutumia taarifa rasmi za hali ya hewa kutoka TMA.
Featured Post
DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.
Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...
-
DODOMA; Tarehe 19 Agosti, 2024; Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imekutana na wadau kutoka sekta mbalimbali nchini ili kujipanga na...
-
Dar es Salaam, 22 /0 8 /202 4 ; Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa utabiri wa msimu wa mvua za VULI 202 4 kwa maeneo yanayopat...
-
Dar es Salaam, Tarehe 05/02/2026; Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa rasmi utabiri wa msimu wa mvua za Masika 202 6 kwa maeneo...















