Thursday, July 25, 2024

TMA CHACHU KATIKA KUSAIDIA KUPUNGUZA ATHARI ZA KUZAMA MAJI NCHINI.



 





DAR ES SALAAM, 24 JULAI 2024.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetajwa kuwa chachu ya kupunguza athari za kuzama maji nchini kwenye mkutano na waandishi wa habari uliyoandaliwa na Shirika la Usimamizi wa Mazingira na Maendeleo (EMEDO) katika ukumbi wa hoteli ya Mbezi Garden, tarehe 24 Julai 2024. Mkutano huo ni moja ya maandalizi ya kuadhimisha Siku ya Kuzama Maji Duniani (World Drowning Day) ambayo huadhimishwa kila mwaka tarehe 25 Julai.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi Mtendaji wa EMEDO Bi. Editrudith Lukanga amezipongeza taasis za Serikali kwa kushirikiana na EMEDO, huku akiitaja TMA kama Taasisi ambayo imekuwa chachu katika kusaidia kupunguza athari zitokanazo na hali mbaya ya hewa na hivyo kuepusha jamii kuzama maji.

"Kupitia ushirikiano kati yetu na taasis mbalimbali za serikali, TMA imekuwa chachu katika kusaidia kupunguza athari zitokanazo na hali mbaya ya hewa na kuepusha jamii kuzama maji". Alisema Bi. Editrudith Lukanga.

Kwa upande mwingine Afisa Mkaguzi wa Vyombo Majini (TASAC), Ndg. George Mnali ameelezea utaratibu wao katika kukabiliana na hali mbaya ya hewa mara baada ya kupata taarifa za TMA, kazi yao ni kuzichakata kulingana na matumizi yao katika kuhakikisha wanapunguza athari zinazoweza kujitokeza Baharini au Ziwani.

Aidha, Mtaalam wa hali ya hewa mwandamizi kutoka TMA, Ndg. Aloyce Swenya, alielezea huduma mbalimbali zinazotolewa na Mamlaka na kuishukuru taasis ya EMEDO kwa kuendeleza ushirikiano huku akiwasisitiza wadau wengine kuhamasika katika utumiaji wa taarifa za hali ya hewa ikiwemo huduma mahususi zinazotolewa na TMA ili kuleta maendeleo endelevu hapa nchini.

Monday, July 22, 2024

TMA AND UNDP CONDUCTS A JOINT MEETING TO DISCUS DOCUMENTS FOR SYSTEMATIC OBSERVATION FINANCING FACILITY (SOFF) PROJECT IMPLEMENTATION IN TANZANIA


Group photo of participants of the joint meeting between TMA and UNDP, which was held on 19th July, 2024 at Morena Hotel, in Dodoma City.




Co-Chair of the meeting from TMA, Acting Director General of TMA, Permanent Representative of Tanzania with WMO and Vice Chair of IPCC, delivering remarks during the joint meeting between TMA and UNDP held on 19th July, 2024 at Morena Hotel, in Dodoma City. On his right hand side is the Co-Chair from UNDP Mr, Godfrey Mulisa, Senior Governance Adviser at UNDP

Co-Chair of the meeting from UNDP Mr, Godfrey Mulisa Senior Governance Adviser at UNDP (on the right hand side) delivering remarks during the joint meeting between TMA and UNDP held on 19th July, 2024 at Morena Hotel, in Dodoma City.

Co- Chair of the meeting between TMA and UNDP (Dr. Ladislaus Chang’a on the left handside and  Mr. Godfrey Mulisa on the right hand side)  seated facing the participants of the meeting when they co-chaired the meeting on 19th July, 2024.



Dodoma, Tanzania; 19th July, 2024.

 

Tanzania Meteorological Authority and UNDP conducted a joint meeting whose objective was to initiate the preparatory phase of the implementation of the Systematic Observation Facility Fund (SOFF) project in Tanzania. The meeting was held on 19th July, 2024 in Dodoma.

 

The meeting was Co-Chaired by the Acting Director General of TMA, Permanent Representative of Tanzania with the World Meteorological Organization (WMO) who is also the Vice Chair of The Inter-Governmental Panel on Climate Change (IPCC), Dr. Ladislaus Chang'a and Mr Godfrey Mulisa, Senior Governance Adviser at UNDP who represented the Resident Representative of UNDP in Tanzania.

 

The objective of the meeting was to deliberate on the preparation  of  draft working tools prepared by the Project Technical Coordination Committee (PTCC). The documents which were presented for review and guidance by the Co-Chairs include the Work Plan for the SOFF Project implementation in Tanzania during July – December, 2024; Terms of Reference of the Project Technical Coordination Committee (PTCC); and Terms of Reference of the Project Steering Committee (PSC) at National level. The meeting also deliberated on the high level launching event of SOFF project which is scheduled to take place by September, 2024.

 

In their opening remarks, both Co-Chairs from TMA and UNDP appreciated the great work done and commitment shown by the PTCC in preparing the documents. The Permanent Representative of Tanzania with WMO also emphasized on the Tanzania commitment to the implementation of SOFF and insisted the PTCC to continue with the commitment to ensure successful implementation of SOFF project in Tanzania and that it leaves a legacy in the whole value chain of provision of weather and climate services in Tanzania and becomes a roll model to others. "We are committed in ensuring that the implementation of SOFF project in Tanzania will leave a long-lasting legacy not only in Africa but to all developing countries across the world. That's why we are putting all the necessary efforts and have assembled a very strong competent team in all the required areas of implementation process so as to ensure everything proceeds as planned" said Dr Chang'a. Dr Chang'a also thanked the UNDP for their continued support in this process. Mr. Godfrey Mulisa, Senior Governance Adviser at UNDP who represented the UNDP Resident Representative,  Mr. Shigeki Komatsubara also thanked TMA for the commitment shown in  continuing  with the good existing partnership between TMA with UNDP. 

 

"I would like to thank TMA for the very good leadership and commitment, you have really demonstrated that you really qualified to be part of this programme, and the reason we are here in the investment phase of the project." Said Mr Mulisa. PTCC is a technical body that has been formulated at National level of SOFF project governance in Tanzania to report to the PSC. The meeting was considered as a pre-meeting of the SOFF Project Steering Committee, which is planned to take place before the official launching of the project. SOFF is a United Nations Multi-Partner Trust Fund (UN MPTF) co-established by WMO, UNDP and the UNEP at COP26. It is a specialized UN climate fund to support countries in closing the Global Basic Observing Network (GBON) weather and climate data gaps, especially in Least Developed Countries (LDCs) and Small Island Developing States (SIDS).

 

Wednesday, May 22, 2024

MWISHO WA KIMBUNGA “IALY”


Dar es Salaam, 22 Mei 2024 Saa 4 Usiku:

Taarifa hii inahitimisha mfululizo wa taarifa za kilichokuwa Kimbunga “IALY” zilizokuwa zikitolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) tangu tarehe 17 Mei 2024. Mwenendo wa mifumo ya hali ya hewa unaonesha kuwa katika kipindi cha saa 6 zilizopita, Kimbunga “IALY” kimepoteza kabisa nguvu yake, kikiwa kaskazini mashariki mwa pwani ya Kenya.

Hivyo, kwa sasa hakuna tena tishio la kimbunga “IALY” katika nchi yetu. Aidha, wakati kikipita karibu na pwani na nchi yetu kati ya jana tarehe 21 na leo tarehe 22 Mei 2024 kimeweza kusababisha vipindi vya mvua, upepo mkali na mawimbi makubwa katika maeneo ya pwani ya nchi yetu kama ilivyotabiriwa awali.

Hata hivyo ikumbukwe kuwa, japo tunaelekea mwishoni mwa msimu wa Masika, 2024, tunakaribia kuanza kwa msimu wa Kipupwe, na kwasababu hiyo, vipindi vya upepo wa Kusi baharini vinaweza kuanza kujitokeza na kuambatana na mawimbi makubwa kwa baadhi ya nyakati.

USHAURI: Wananchi na watumiaji wa bahari wanashauriwa kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania pamoja na maelekezo na miongozo inayotolewa na mamlaka husika.

Friday, May 17, 2024

WAZIRI WA UCHUKUZI ASHIRIKI MKUTANO WA SITA WA MAWAZIRI WENYE DHAMANA YA MASUALA YA HALI YA HEWA BARANI AFRIKA (AMCOMET-6)

Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mnyaa Mbarawa (MB) ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza la Mawaziri wa Africa wenye Dhamana ya Hali ya Hewa (African Ministerial Conference on Meteorology – AMCOMET)- akishiriki katika Mkutano wa Sita wa Baraza la AMCOMET (AMCOMET-6).

 
Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mnyaa Mbarawa (Mb) ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza la Mawaziri wa Africa wenye Dhamana ya Hali ya Hewa (African Ministerial Conference on Meteorology – AMCOMET)- akifuatilia majadiliano  katika Mkutano wa Sita wa Baraza la AMCOMET (AMCOMET-6) uliofanyika kwa njia ya mtandao, tarehe 16 Mei 2024. Wanaofuatilia Mkutano huo pamoja na Mhe. Waziri ni Dkt. Geofrid Chikojo (Kulia)- Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) na Bw. Wilbert Muruke (Kushoto)-Meneja wa Uhusiano wa Hali ya Hewa Kikanda na Kimataifa.

Dodoma, Tarehe 16 Mei 2024.

 

Tanzania kupitia Wizara ya Uchukuzi ikiongozwa na Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mnyaa Mbarawa (Mb) na Wataalamu kutoka Wizara ya Uchukuzi na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) walishiriki katika Mkutano wa Sita wa Baraza la Mawaziri wenye Dhamana ya Hali ya Hewa Barani Afrika (Sixth African Ministerial Conference on Meteorology – AMCOMET-6) uliofanyika tarehe 16 Mei 2024 kwa njia ya mtandao.

 

Mkutano huo wa AMCOMET ulipokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa shughuli za AMCOMET kutoka kwa Sekretarieti hiyo na kuridhia Mpango Mkakati wa utekelezaji wa masuala ya hali ya hewa Barani Afrika uliohuishwa pamoja na kuidhinisha Mpango wa Utafutaji Rasilimali kwa ajili ya utekelezaji wa Mkakati wa kuimarisha huduma za hali ya hewa Barani Afrika. Masuala mengine yaliyojitokeza tangu Mkutano wa Tano wa AMCOMET ulioofanyika Machi 2021, yalijadiliwa na kutolewa maazimio. Aidha, AMCOMET-6 imejadili maendeleo ya Sekta ya Hali ya Hewa na umuhimu wake kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi barani Afrika.

 

Vilevile wajumbe walijadili na kukubaliana umuhimu wa kuendelea kuzijengea uwezo wa kisera na kitaalamu Taasisi za Hali ya Hewa ili kuendelea kuimarisha ubora na ufanisi katika utoaji wa huduma hususan taarifa za utabiri na tahadhari za matukio ya hali mbaya ya hewa yanayochagizwa na mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi. Madhara yatokanayo na matukio ya hali mbaya ya hewa yameendelea kujitokeza kwa sura tofauti ikiwa ni pamoja na matukio ya mafuriko na ukame yanayoshuhudiwa Barani Afrika na kwa hivi karibuni katika eneo la Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania. Huduma zinazotolewa na Taasisi za Hali ya Hewa ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango wa Umoja wa Mataifa wa kuhakikisha kuwa, kila nchi inakuwa na mfumo mzuri wa utoaji wa tahadhari kwa watu wote ifikapo mwaka 2027 (UN Early Warning for All-AW4ALL initiative).

 

Akichangia katika mada ya Mkutano inayohusiana na maandalizi ya Mpango wa Utekelezaji, Ufuatiliaji na Tathmini na Mpango wa Kukusanya Rasilimali, Mhe. Prof. Mbarawa alimpongeza Mwenyekiti wa AMCOMET aliyemaliza muda wake (Cameroon) pamoja na Sekretarieti kwa kufanikisha maandalizi ya mipango hiyo, ambayo ni utekelezaji wa Mkakati Jumuishi wa Masuala ya Hali ya Hewa wa Afrika uliohuishwa (African Integrated Strategy on Meteorology) ambao Baraza la Mawaziri wa Umoja wa Afrika (AU) na Mkutano Mkuu wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa AU waliupitisha mwaka 2022. “Haya ni mafanikio makubwa ya kisera ambayo sote tunapaswa kuhusika katika utekelezaji wake, hivyo tunapongeza sana kazi kubwa iliyofanywa hadi sasa. Hata hivyo ni vyema kuhakikisha kuwa mipango hii inaendana vyema na mipango mingine ya kikanda na kitaifa ili kuhakikisha kwamba hakuna anayeachwa nyuma katika utekelezaji wake” Alisema Prof. Mbarawa.

 

Baraza la Mawaziri wenye dhamana ya masuala ya hali ya hewa katika Bara la Afrika (AMCOMET) hukutana kila baada ya miaka miwili. Wajumbe wa mkutano wa AMCOMET ni Waheshimiwa Mawaziri wenye dhamana ya masuala ya hali ya hewa Barani Afrika na Mwenyekiti aliyepokea kijiti cha kuongoza AMCOMET kwa kipindi cha miaka miwili ijayo kuanzia 2024 hadi 2026 ni nchi ya Uganda.


UWEPO WA KIMBUNGA “IALY” KATIKA BAHARI YA HINDI KASKAZINI MWA MADAGASCAR


Dar es Salaam, 17 Mei 2024:

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inatoa taarifa ya uwepo wa kimbunga “IALY” katika Bahari ya Hindi kaskazini mwa kisiwa cha Madagascar.

Mifumo ya hali ya hewa inaonesha kuwa kimbunga hicho kitaendelea kusalia katika Bahari ya Hindi katika eneo kati ya Madagascar na visiwa vya Shelisheli kwa siku nne zijazo kabla ya kuanza kupungua nguvu.

Aidha, kutokana na umbali kutoka nchini, kimbunga hicho hakitarajiwi kuwa na athari za moja kwa moja katika kusababisha ongezeko la mvua nchini. Hata hivyo vipindi vya upepo mkali na mawimbi makubwa vinaweza kujitokeza katika Bahari ya Hindi.

USHAURI: Watumiaji wa bahari na wananchi kwa ujumla wanashauriwa kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania pamoja na kupata ushauri na miongozo ya wataalam wa kisekta.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kufuatilia mwenendo wa kimbunga hicho na athari zake kwa mifumo ya hali ya hewa hapa nchini na itaendelea kutoa taarifa kila inapobidi.

Imetolewa na:
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.

Tuesday, May 14, 2024

SEVERE WEATHER FORECASTING PROGRAMME TO OPEN UP NEW COLLABORATION IN AFRICA.

 


















Dar es Salaam, Tanzania, 14 May 2024.

Chairperson of Tanzania Meteorological Authority (TMA) Board, Hon. Judge Mshibe Ali Bakari urged for more collaboration among National Meteorological and Hydrological Services (NMHSs) of Eastern Africa countries to promote innovation and collaboration in addressing challenges facing effectiveness in early warning services specifically forecasting of severe weather events. “I really encourage NMHSs to consider collaborating among yourselves to harness available capacities in our respective countries in ensuring that we achieve the goal of attaining effective early warning services in line with the ‘United Nations Early Warning for All initiative”. Said Hon. Mshibe during the opening ceremony of the Meeting of the Regional Sub-programme Management Team (RSMT) of Severe Weather Forecasting Programme for Eastern Africa (SWFP-EA), on 14 -17 May 2024, Four Points, Dar es Salaam.

He also commented on the role of local capacities and collaboration as the key to complement the global guidance products in enhancing the capacity of Regional Specialized Meteorological Centres and National Meteorological Hydrological Services in provision of improved products and quality services.   

The Acting Director of TMA -Zanzibar Office , Mr. Masoud Faki who represented the Acting Director General of TMA  said, among the benefits that TMA acquired through the implementation of Severe Weather Forecasting Programme are Weather Forecast Guidance products from the Contributing Global and Regional Meteorological Centers which have demonstrated to be highly useful in preparation of National level weather forecasts through the cascading approach involving downscaling to the national domain.

“TMA has been given the role by WMO to oversee activities of the “Regional Specialized Meteorological Centre – Dar es Salaam (RSMC-Dar es Salaam)” with the responsibilities of preparing and issuing severe weather forecast guidance products for the Lake Victoria basin for use by the National Meteorological and Hydrological Services (NMHSs) of Eastern African countries around Lake Victoria basin”, Explained Mr. Masoud.

On the other hand, Representatives of WMO Secretariat Dr. Ata Hussain expressed his sincere appreciation to the United Republic of Tanzania for hosting important gathering which seeks to improve early warning services, specifically forecasting of severe weather events in Eastern African countries with the aim of reducing fatalities associated with weather hazards. This meeting is therefore of vital importance to the work of National Meteorological and Hydrological Services (NHMSs) in enhancing Early Warning Services delivery, particularly Severe Weather Forecasting to support Disaster Risk Reduction in the Eastern Africa Sub-region in line with the “United Nations’ Early Warning for All” initiative.

Participants were from Tanzania, Burundi, Djibouti, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Somalia, Sudan, Uganda, Djibouti, Somalia, South Sudan and other experts from Contributing World Meteorological Centres -WMCs and Regional Specialized Meteorological Centres -RSMCs.


Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...