Saturday, May 16, 2026

KAMATI YA URATIBU YA MRADI WA SOFF YAKUTANA JIJINI DODOMA








Dodoma, 14 Mei 2026

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), kwa kushirikiana na Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), walifanya kikao kazi cha tano cha Kamati ya Uratibu  wa Mradi wa SOFF (Systematic Observations Financing Facilit)  katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.

Kikao hicho kiliwakutanisha wataalamu muhimu ili kupitia maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa SOFF na kujadili vipaumbele vya kimkakati kwa mwaka 2026, vinavyolenga kuhakikisha ufanisi katika utekelezaji wa shughuli za mradi.


Majadiliano yalijikita katika utekelezaji wa Mpango Kazi wa Mwaka 2026,  ufuatiliaji na tathmini ya mradi, pamoja na shughuli za mawasiliano na uhamasishaji zilizopangwa kwa mwaka 2026. Kamati pia ilipitia maamuzi na maelekezo kutoka kikao cha Tatu cha Kamati Tendaji ya Mradi wa SOFF kilihofanyika Aprili 2026.


Wakizungumza katika ufunguzi, Wenyeviti wenza wa kamati hiyo, Dkt. Paschal Waniha kutoka TMA na Dkt.Abbas Kitogo kutoka UNDP, walisisitiza umuhimu wa kuendelea kushirikiana kikamilifu ili kuhakikisha utekelezaji unafanyika kwa wakati katika shughuli zote zilizopangwa za mradi wa SOFF Tanzania.Aidha,

kikao kilihitimishwa kwa wajumbe kutoa dhamira ya pamoja ya kuimarisha uratibu, kuharakisha utekelezaji wa shughuli zilizopangwa, na kuongeza ufanisi wa jumla wa mradi wa SOFF nchini Tanzania.

THE FIFTH SOFF PROJECT TECHNICAL COORDINATION COMMITTEE IN TANZANIA CONVENES IN DODOMA

Dodoma, 14th May 2026;

The Tanzania Meteorological Authority in collaboration with the United Nations Development Programme (UNDP)  convened for the Fifth Meeting of the Systematic Observations Financing Facility (SOFF) Project Technical Coordination Committee (PTCC-5) at Morena Hotel in Dodoma.

The meetin








g brought together Members of the PTCC and key experts to deliberate on the implementation progress of the SOFF project and to discuss strategic priorities for implementation of the project in 2026 aimed at ensuring efficiency in the implementation of project activities.


The agenda of the meeting focused more on the implementation of the approved 2026 SOFF Project Annual Workplan, project monitoring report, as well as planned monitoring, communication and outreach activities for 2026. The committee also strategized on the implementation of decisions and directives by the SOFF Project Steering Committee (PSC), which were given by the PSC at the 3rd meeting held on 9th April 2026.


Speaking during the opening session, the PTCC Co-Chairs, Dr. Paschal Waniha and Dr. Abbas Kitogo from TMA and UNDP respectively, emphasized the importance of continued effective collaboration to ensure timely implementation of all planned SOFF project activities. 


Also the PTCC-5 meeting concluded with a shared commitment among PTCC members to strengthen coordination, accelerate the implementation of planned activities, and enhance the overall effectiveness of the SOFF project in Tanzania

Wednesday, April 15, 2026

TMA ENHANCES REGIONAL COOPERATION AND CAPACITY BUILDING IN METEOROLOGICAL SERVICES THROUGH WMO CAPACITY-BUILDING PROGRAMME

 TMA ENHANCES REGIONAL COOPERATION AND CAPACITY BUILDING IN METEOROLOGICAL SERVICES THROUGH WMO CAPACITY-BUILDING PROGRAMME 










Dodoma, 13 April 2026


The Tanzania Meteorological Authority (TMA) through the World Meteorological Organization (WMO) capacity building programne, hosted a regional delegation from the Institut Géographique du Burundi (IGEBU) and the South Sudan Meteorological Services (SSMS) for Practical training and capacity building on Numerical Weather Prediction (NWP), Severe Weather Forecasting, and Quality Management Systems (QMS) held from 12th to 17th April 2026 in Tanzania.


Organised through WMO Climate Risk and Early Warning Systems  (CREWS) Project,  the visit aimed at strengthening technical capacity of  IGEBU and SSMS Experts  in meteorological service delivery, particularly in the areas of NWP, QMS and Severe Weather Forecasting.


Opening the programme, TMA Director General and Vice-Chair of the Intergovernmental Panel on Climate change (IPCC) Dr. Ladislaus Chang’a, underscored Tanzania’s commitment in strengthening  regional cooperation and in providing training and technical support to  other NMHS including through various WMO programme.


“This practical visit demonstrates our strong commitment to advancing meteorological services not only in Tanzania, but across Africa, including through sharing our experience, knowledge and technical capacity in various aspects of meteorological services. Through South-South Collaboration and Cross-Learning, we can accelerate the enhancement of our service delivery in the continent and build resilience against weather and climate challenges. We are honored to host you here at TMA, both in Dodoma and Dar es Salaam.” Said Dr Chang'a


 Zablon Shilenje a representative  from WMO regional office for Africa(RA I) on behalf of Director of WMO Africa, Dr. Agnes Kijazi expressed the appreciation for Tanzania leadership and commitment to regional collaboration. 

“We are grateful to Tanzania for its leadership and for sharing its expertise, as well as for its continued support to South Sudan and Burundi. It is important that we move forward together and ensure that no one is left behind. Capacity building plays a critical role in strengthening meteorological services".Saidi Mr. Zablon


Permanent representative of Burundi with WMO, Mr Deogratias Babonwanayo commended the initiative and thanked TMA for providing technical support to Burundi “We are grateful for the opportunity to come to TMA and learn from their experience in implementing Quality Management Systems. This visit and the knowledge tha we get,  will greatly support the enhancement of our services in Burundi.”


Mr Mojwok Ogawi Modo who is the Permanent representative for South Sudan with WMO  also highlighted the importance of the Visit. 

“This visit will provide valuable practical insights and strengthen our capacity in QMS, NWP and in Severe Weather Forecasting. We are confident that the lessons learned here will contribute to improving meteorological services in South Sudan.”


This practical visit reflects Tanzania’s ongoing leadership in fostering regional integration and cooperation in meteorological services reinforcing efforts and commitment to strengthening climate services for sustainable development.

TMA YAENDELEA KUWAJENGEA UWEZO TAASISI ZA HALI YA HEWA BARANI AFRIKA KUPITIA PROGRAMU ZA WMO

 TMA YAENDELEA KUWAJENGEA UWEZO TAASISI ZA HALI YA HEWA BARANI AFRIKA KUPITIA PROGRAMU ZA WMO









Dodoma, 13 Aprili 2026


Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imewapokea na Viongozi na Wataalamu wa hali ya hewa kutoka Taasisi ya Hali ya Hewa ya Burundi (IGEBU) na Taasisi ya Hali ya Hewa ya Sudan Kusini (SSMS) kwa ajili ya mafunzo ya vitendo  kuhusu Utabiri wa Hali ya Hewa kwa Njia za Mahesabu (NWP), utabiri wa hali mbaya ya hewa, na mifumo ya usimamizi wa ubora (QMS). Mafunzo hayo yanafanyika kuanzia tarehe 13 hadi 17 Aprili 2026 Tanzania.


Mafunzo haya yameandaliwa kwa ushirikiano na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) kupitia Mradi wa Kuboresha Mfumo wa Utoaji wa Tahadhari za Hali Mbaya ya Hewa (CREWS). Mafunzo  yanalenga kuwajengea uwezo wa utaalamu na mbinu bora katika utoaji wa huduma za hali ya hewa katika ukanda wa Afrika Mashariki.


Akifungua programu ya mafunzo hayo kwa vitendo, Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi, Dkt. Ladislaus Chang’a, alisisitiza dhamira ya Tanzania kupitia TMA katika kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika masuala ya huduma za hali ya hewa.


“Mafunzo haya yanaonesha dhamira yetu thabiti ya kuboresha huduma za hali ya hewa si tu nchini Tanzania bali katika ukanda mzima wa Afrika. Kupitia ushirikiano na mafunzo haya, tunaweza kuboresha utoaji wa huduma na kujenga uimara na ustaimilivu dhidi ya changamoto za mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi. Tunafuraha kubwa kuwakaribisha hapa TMA katika Ofisi zetu za Dodoma na Dar es Salaam.”Alizungumza Dkt. Chang'a.


Akizungumza kwa niaba ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani, Bw. Zablon Shilenje alitoa shukrani kwaniaba ya Mkurugenzia wa WMO Afrika, Dkt.Agnes Kijazi kwa uongozi wa Tanzania na dhamira yake katika kutoa ushirikiano wa kikanda.


“Tunashukuru Tanzania kwa kuendeleza ushirikiano hususani katika eneo la kuwajengea uwezo wataalamu wa hali ya hewa kutoka Afrika ikiwemo Sudan Kusini na Burundi. Ni muhimu tusonge mbele pamoja na kuhakikisha hakuna anayebaki nyuma katika uboreshaji huduma za hali ya hewa".Alisema Bw. Zablon


Naye, Mkurugenzi Mkuu wa IGEBU, Bw. Deogratias Babonwanayo, alipongeza mpango huo:“Tunashukuru kwa fursa ya kushirikiana na TMA na kujifunza kutokana na uzoefu wao katika utekelezaji wa mifumo ya usimamizi wa ubora. Mafunzo haya yatachangia kwa kiasi kikubwa kuboresha huduma zetu nchini Burundi.”


Kwa upande wake, Bw. Mojwok Ogawi Modo, Mkurugenzi Mkuu SSMS, alieleza umuhimu wa ziara hiyo:“Ziara hii itatoa nyenzo muhimu kwa vitendo na kuendelea kuimarisha ushirikiano wetu na washirika wa kikanda hususani Tanzania. Tunaamini kwamba mafunzo tunayoyapata hapa yatachangia kuboresha huduma za hali ya hewa nchini Sudan Kusini".


Ziara hii ya vitendo inaakisi uwekezaji endelevu wa Tanzania katika kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika sekta ya hali ya hewa, na kuboresha miundombinu ya utoaji huduma za hali ya hewa kwa maendeleo endelevu.

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...