Tuesday, December 17, 2019

KATIBU MKUU MWALUKO ATAKA MIPANGO KABLA YA MAAFA NA SIO WAKATI WA MAAFA

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko akisisitiza jambo wakati wa kikao cha Jukwaa la Taifa la Usimamizi wa Maafa nchini, jijini Dodoma. Tarehe 16 Desemba, 2019.


Mkurugenzi Idara ya Uratibu wa Maafa , Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Jimmy Matamwe,akieleza umuhimu wa Jukwaa la Taifa la Usimamizi wa Maafa nchini wakati wa kikao cha Jukwaa hilo, jijini Dodoma, Tarehe 16 Desemba, 2019.kulia kwake ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji) Dorothy Mwaluko na Mkurugenzi wa Kituo cha Taifa cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura, Ofisi ya Waziri Mkuu, Meja, Selestine Masalamando.

Baadhi ya wajumbe wa Jukwaa la Taifa la Usimamizi wa Maafa nchini wakifuatilia kikao cha Jukwaa hilo, jijini Dodoma, tarehe 16 Desemba, 2019. Jukwaa hilo hutathmini na kutoa ushauri wa kitaalamu kwa serikali kuhusu majanga ya aina zote.

Baadhi ya wajumbe wa Jukwaa la Taifa la Usimamizi wa Maafa nchini wakifuatilia kikao cha Jukwaa hilo, jijini Dodoma, tarehe 16 Desemba, 2019., Jukwaa hilo ni muhimu kwa ajili ya ushauri wa maeneo ya kipaumbele katika usimamaizi wa maafa.

Baadhi ya wajumbe wa Jukwaa la Taifa la Usimamizi wa Maafa nchini wakifuatilia kikao cha Jukwaa hilo, jijini Dodoma, tarehe 16 Desemba, 2019,  Jukwaa hilo linajumiisha wataalamu kutoka katika sekta za umma, binafsi, asasi za kiraia na kimataifa.

Mratibu wa masuala ya Maafa Ofisi  ya Waziri Mkuu, Charles Msangi akifafanua umuhimu wa ushirikishwaji wa wadau katika usimamizi wa maafa wakati wa  kikao cha Jukwaa la Taifa la Usimamizi wa Maafa nchini, jijini Dodoma, tarehe 16 Desemba, 2019

Baadhi ya wajumbe wa Jukwaa la Taifa la Usimamizi wa Maafa nchini wakifuatilia kikao cha Jukwaa hilo, jijini Dodoma, tarehe 16 Desemba, 2019, Jukwaa hilo linajumiisha wataalamu kutoka katika sekta za umma, binafsi, asasi za kiraia na kimataifa

Baadhi ya wajumbe wa Jukwaa la Taifa la Usimamizi wa Maafa nchini wakifuatilia kikao cha Jukwaa hilo, jijini Dodoma, tarehe 16 Desemba, 2019, Jukwaa hilo linalojukumu la kufuatilia utekelezaji wa Mkakati wa Kupunguza Madhara ya maafa wa Sendai, 2015-2030.

Baadhi ya wajumbe wa Jukwaa la Taifa la Usimamizi wa Maafa nchini wakifuatilia kikao cha Jukwaa hilo, jijini Dodoma, tarehe 16 Desemba, 2019, Jukwaa hilo limekutana kwa mara ya kwanza tangu Sheria ya maafa Na. 7  ya mwaka 2015 ianze kutumika

Wajumbe wa Jukwaa la Taifa la Usimamizi wa Maafa nchini wakiwa katika kikao cha Jukwaa hilo, jijini Dodoma, tarehe 16 Desemba, 2019, Jukwaa hilo linaundwa kwa kuzingatia kifungu cha 40 cha sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 7 ya mwaka 2015.

Wajumbe wa Jukwaa la Taifa la Usimamizi wa Maafa nchini wakiwa katika picha ya pamoja na  Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji) Bi. Dorothy Mwaluko, jijini Dodoma, tarehe 16 Desemba, 2019, Jukwaa hilo linaundwa kwa kuzingatia kifungu cha 40 cha sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 7 ya mwaka 2015.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji) Dorothy Mwaluko amelielekeza Jukwaa la Taifa la Usimamizi wa Maafa nchini kutoa ushauri wa kitaalamu unaojikita katika hatua ya kabla ya maafa kutokea na sio kujikita wakati wa maafa yanapotokea kama ilivyozoeleka, kwa kuwa ushauri wa namna ya kuzuia na kujiandaa na maafa kabla ya maafa kutokea huweza  kupunguza madhara ya maafa na rasilimali zinazohitajika katika upunguzaji wa madhara hayo.

Ameyasema hayo leo Jijini Dodoma tarehe 16 Desemba, 2019, wakati akifungua kikao cha Jukwaa hilo ambapo amebainisha kuwa wakati wa kukabili majanga na maafa kunakuwepo na mipango mingi ambayo hutekelezwa na wadau wa Usimamizi wa maafa na kwa uchache wakati wa urejeshaji hali wa maafa,  lakini mipango ya kujiandaa na  kuzuia maafa ambayo hufanyika kabla ya maafa kutokea  kwa ajili ya kuzuia au kupunguza madhara ya  maafa yatakapotokea huwa haitekelezwi.

“Tumekuwa na maafa hapa nchini ambayo yameleta madhara nchini,  itakumbukwa ajali ya moto mjini Morogoro hivi karibuni, tujiulize kuna mipango inayoendelea katika kuzuia majanga hayo, yapo maafa ya mvua yanaendelea kutokea,  lakini je ipo mipango ya kabla ya maafa kutokea, lakini pindi maafa yakitokea wadau wa usimamizi wa  maafa hujitokeza na kuanza kukabili maafa, sasa nataka nguvu nyingi ielekezeni kwenye mipango ya kabla ya maafa kutokea na hata ikibidi ainisheni majanga yanayoweza kutokea kwenye maeneo husika ili jamii iweze kujiandaa na kuyazuia maafa husika kabla yakutokea“ Amesisitiza Mwaluko.

Aidha, amelielekeza Jukwaa hilo kuupitia Mkakati wa Taifa wa Kupunguza athari za maafa na kuhakikisha kuwa unaendana na uhalisia wa hali ya majanga yanayotokea katika jamii ili uweze kutekelezeka kwa kuweka malengo yenye uhalisia, huku akisisitiza kuwa ni vyema mkakati huo ukatafsiriwa kwa Kiswahili ili uweze kutumiwa vyema na walengwa kuanzia ngazi ya msingi ya maafa ambayo ni kamati za vijiji.

Katika hatua nyingine  Katibu Mkuu, Mwaluko  amelielekeza Jukwaa hilo kuwa na ushirikiano miongoni mwa wadau wa jukwaa hilo kwa kila mdau kuainisha majukumu yake na namna anavyoyatekeleza majukumu yake, ili kuweza kujua jukumu la kila mdau na anafanya nini  na kwa wakati gani na hatimaye mipango ya kuimarisha Usimamizi wa maafa iwe inayotekelezeka.

“Kupunguza madhara ya maafa ni suala mtambuka lenye mchango mkubwa katika shughuli za maendeleo.Wakati mwingine wananchi wamekuwa wakipata madhara kwa kukosa uelewa hivyo ni vyema kila mdau kuwajibika katika majukumu yake kwa kutoa fursa ya uratibu wa usimamizi wa maafa kwa ushirikiano  wa wataalamu wa  fani mbalimbali” Amesema,  Mwaluko

Awali akiongea katika kikao hicho, Mkurugenzi Idara ya Uratibu wa Maafa , Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Jimmy Matamwe, ameeleza kuwa Jukwaa hilo ni chombo cha kisheria ambacho kipo kwa ajili ya kutathmini na kutoa ushauri wa kitaalam kwa serikali kuhusu majanga ya aina zote, ambapo Jukwa hilo  linaundwa kwa kuzingatia Kifungu cha 40 cha Sheria ya Usimamizi wa Maafa Na.7 ya mwaka 2015.

Kikao hicho kimeratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana  na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania kupitia ufadhili wa Awamu ya Pili ya Programu ya Kidunia ya Utoaji wa Huduma za Hali ya Hewa ya GFCS (Global Framework for Climate Services Adaptation Programme in Africa (APA) II). 

Jukwaa hilo ambalo linajumuisha wataalamu wa fani mbali mbalimbali  kwa kujumuisha sekta ya umma na sekta binafsi, mashirika ya kimataifa na umoja wa mataifa na asasi za kiraia jukumu lake la  msingi ni kutoa ushauri maeneo ya kipaumbele katika usimamizi wa maafa kwa uratibu na ushirikishawaji wa wadau ili kufanikisha kujumuisha upunguzaji wa madhara ya maafa katika mipango na sera za maendeleo ya taifa na katika misaada ya kibinadamu.  

CHANZO: OFISI YA WAZIRI MKUU

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...