Tuesday, December 24, 2019

TMA YASISITIZA WADAU KUCHOCHEA MATUMIZI SAHIHI YA TAARIFA ZA HALI YA HEWA KATIKA SEKTA ZAO.

Wadau wakiwa kwenye picha ya pamoja na mgeni rasmi, Dkt. Hamza Kabelwa (katikati mwenye miwani) katika warsha ya wadau kutoka sekta mbalimbali inayohusu matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa baina ya muandaaji na mtumiaji, iliyofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Pwani kuanzia Tarehe 22-24 Disemba, 2019.
Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania(TMA), Dkt. Hamza Kabelwa (Kushoto) akizungumza wakati akifungua warsha ya wadau kutoka sekta mbalimbali inayohusu matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa baina ya muandaaji na mtumiaji, iliyofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Pwani kuanzia Tarehe 22-24 Disemba, 2019.
Wataalam wa hali ya hewa kutoka TMA wakiwasilisha mada katika warsha ya wadau inayohusu matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa baina ya muandaaji na mtumiaji, iliyofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Pwani kuanzia Tarehe 22-24 Disemba, 2019.
Wadau mbalimbali wakichangia mada katika warsha ya wadau kutoka sekta mbalimbali inayohusu matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa baina ya muandaaji na mtumiaji, iliyofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Pwani kuanzia Tarehe 22-24 Disemba, 2019.



MKURANGA, PWANI  22/12/2019;
Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dkt. Hamza Kabelwa kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi alifungua warsha ya wadau kutoka sekta mbalimbali iliyohusu matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa baina ya muandaaji na mtumiaji wa taarifa za hali ya hewa, iliyofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Pwani kuanzia Tarehe 22-24 Disemba, 2019.

Katika hotuba  yake Dkt. Kabelwa  alisisitiza wadau mara watakapomaliza warsha hiyo kuchochea matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa katika sekta zao ili kupunguza au kuepusha athari zinazoweza kusababishwa na hali mbaya ya hewa.

“Mkiwa kama kiunganishi kati ya  TMA na wananchi tunawaomba ninyi washiriki kuchochea matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa katika sekta zenu”, alisisitiza Dkt. Kabelwa.

Aidha, washiriki walikumbushwa kutambua kuwa majanga ya asili hayawezi kuepukika, lakini taarifa zikiwafikia walengwa kabla ya janga husika kutokea basi zitasaidia kujipanga ili kukabiliana na madhara yanayoweza kujitokeza, hivyo Dkt. Kabelwa aliwataka washiriki kushirikiana na TMA kuhakikisha taarifa za hali ya hewa zinawafikia walengwa kwa wakati na kueleweka.

Warsha hiyo iliandaliwa na TMA na kufadhiliwa na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (World Meteorological Organization – WMO), chini ya mwamvuli wa Programu ya kidunia ya kuwaongezea ujuzi waandaaji na watumiaji wa taarifa za hali ya hewa barani Afrika (Weather and Climate Information Services for Africa - WISER).

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...