Monday, December 27, 2021

KIKAO CHA MWAKA 2021, TUGHE - TMA


 





Matukio mbalimbali katika picha wakati kikao cha TUGHE - TMA, mwaka 2021 kikiendelea katika ukumbi wa mikutano TCAA, Dar es Salaam. Tarehe 24/12/2021.






Thursday, December 23, 2021

HERI YA KRISMAS NA MWAKA MPYA 2022


 

WATAALAMU WATAKIWA KUFANYA TAFITI ZENYE TIJA.

Mgeni Rasmi, Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhe. Mwita Waitara (MB) akizungumza kabla ya kukizindua rasmi kitabu cha Klimatolojia na Athari zitokanazo na Matukio ya Hali Mbaya ya Hewa Tanzania, Katika Ukumbi wa Mikutano ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Ubungo Plaza, Tarehe 23/12/2021.  

Mgeni Rasmi, Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhe. Mwita Waitara (MB) akizindua rasmi kitabu cha Klimatolojia na Athari zitokanazo na Matukio ya Hali Mbaya ya Hewa Tanzania, Katika Ukumbi wa Mikutano ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Ubungo Plaza, Tarehe 23/12/2021. 

Mwenyekiti wa Bodi ya TMA, Dkt. Buruhani Nyenzi akitoa neno la ukaribisho kwa mgeni rasmi kabla ya uzinduzi wa kitabu cha Klimatolojia na Athari zitokanazo na Matukio ya Hali Mbaya ya Hewa Tanzania, Katika Ukumbi wa Mikutano ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Ubungo Plaza, Tarehe 23/12/2021. 


Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agnes Kijazi ambaye pia ni Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), akifafanua jambo kabla ya uzinduzi rasmi wa kitabu cha Klimatolojia na Athari zitokanazo na Matukio ya Hali Mbaya ya Hewa Tanzania, Katika Ukumbi wa Mikutano ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Ubungo Plaza, Tarehe 23/12/2021. 


Mwandishi wa kitabu hicho, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Utafiti na Matumizi ya Huduma za Hali ya Hewa, Dkt. Ladislaus Chang'a akielezea chimbuko la kuhamasika kuandika kitabu hicho cha Klimatolojia na Athari zitokanazo na Matukio ya Hali Mbaya ya Hewa Tanzania, Katika Ukumbi wa Mikutano ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Ubungo Plaza, Tarehe 23/12/2021.  

Mgeni Rasmi akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania baada ya kuzinduliwa rasmi kitabu cha Klimatolojia na Athari zitokanazo na Matukio ya Hali Mbaya ya Hewa Tanzania, Katika Ukumbi wa Mikutano ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Ubungo Plaza, Tarehe 23/12/2021.


Mgeni Rasmi akiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania(TMA) baada  ya kuzinduliwa rasmi kitabu cha Klimatolojia na Athari zitokanazo na Matukio ya Hali Mbaya ya Hewa Tanzania, Katika Ukumbi wa Mikutano ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Ubungo Plaza, Tarehe 23/12/2021. 


 Dar es Salaam; Tarehe 23 Disemba, 2021;
Wataalamu nchini wametakiwa kufanya tafiti zenye tija na kuelimisha jamii kupitia njia mbalimbali ikiwemo kuandika vitabu. Hayo yalizungumzwa na Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhe. Mwita Waitara (MB) wakati akizindua rasmi kitabu cha Klimatolojia na Athari zitokanazo na Matukio ya Hali Mbaya ya Hewa Tanzania, katika Ukumbi wa Mikutano ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Ubungo Plaza,Tarehe 23/12/2021. 

Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kuelimisha jamii na kuwaandaa na kuwataka wataalamu kutoa mchango chanya wa kusaidia kukabiliana na changamoto hizo, ikiwemo kufanya tafiti na kuelimisha jamii”. Alizungumza Mhe. Waitara.

Aidha, Mhe. Naibu Waziri alitoa wito kwa umma kukitumia vizuri kitabu hicho ili kujipatia elimu na uelewa zaidi kuhusiana na changamoto za hali ya hewa hapa Tanzania katika kupanga na kutekeleza mipango ya kijamii na kiuchumi kwa tija na ufanisi zaidi.
Katika hatua nyingine, Mhe. Waitara aliipongeza Bodi na Menejimenti ya TMA kwa usimamizi na kazi kubwa ya kuendelea kuboresha huduma za hali ya hewa ikiwemo utabiri mzuri uliotolewa wa kuhusiana na upungufu wa mvua katika maeneo mengi ya nchi kwa msimu huu wa mvua.

“Maeneo mengi yamekuwa na upungufu mkubwa wa mvua kama ambavyo mlisema katika taarifa yenu ya mwezi Septemba,2021. Utabiri na tahadhari mnazozitoa zinamchango mkubwa katika kuongeza ufanisi na tija katika shughuli zote za kiuchumi na kijamii na pia katika utekelezaji wa Miradi ya Kimkakati kama ya SGR na Ujenzi wa Bwawa la Nyerere”. Alifafanua Mhe. Waitara.

Awali wakati akimkaribisha Mgeni Rasmi, Mwenyekiti wa Bodi ya TMA, Dkt. Buruhani Nyenzi alisema Kitabu hicho ni cha sayansi ya hali ya hewa kinachoweza kutumika kwa ajili ya kuendeleza tafiti za hali ya hewa hasa kwa Tanzania na suala la kujivunia ni kuwa kitabu hicho kimeandikwa na mmoja wa wataalamu kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania ambaye ni Dkt. Ladislaus Chang’a.

 Akizungumzia mafanikio ya kitabu hicho, Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agnes Kijazi ambaye pia ni Makamu wa tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), alifafanua kuwa kitabu hiki kinatoa mchango mkubwa katika kuongeza uelewa wa changamoto za hali ya hewa kwa watu wote hususan wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu pamoja na Chuo cha Taifa cha Hali ya Hewa kilichopo Kigoma, watafiti, makandarasi na watunga sera. 

“Baadhi ya maudhui ambayo yamewekwa katika kitabu hiki ni pamoja na tathmini ya hali ya klimatolojia na mwelekeo wa joto, mvua, unyenyevu na upepo, ambapo uelewa wake ni wa muhimu sana kwasasa na hata kwa wakati ujao ili kupanga na kutekeleza shughuli zote za kiuchumi na kijamii, ikiwemo kilimo, Nishati, Afya, Maji na Usafiri”. Alifafanua Dkt. Kijazi.

Naye, mwandishi wa kitabu hicho ambaye pia ni Mkurugenzi wa Utafiti na Matumizi ya Huduma za Hali ya Hewa, Dkt. Ladislaus Chang’a alieleza chimbuko la kuhamasika kuandika kitabu hicho ni kutokuwepo kwa kitabu cha namna hiyo katika kufundisha kozi za klimatolojia na mabadiliko ya hali ya hewa UDSM na SUA, ushiriki mdogo wa wanasayansi wa Afrika katika masuala ya sayansi ya mabadiliko ya hali ya hewa katika Jopo la Kiserikali la Mabadiliko ya Hali ya Hewa Duniani – IPCChamasa na msukumo mdogo katika masuala ya sayansi na utafiti miongoni mwa vijana na changamoto ya mabadiliko ya hali ya hewa Tanzania na Duniani.

Friday, December 17, 2021

DR. KIJAZI ARGUED SCIENTIST TO KEEP PACE WITH RAPID CHANGE OF TECHNOLOGY ON DEMAND OF QUALITY WEATHER FORECAST.


Kibaha, Pwani;14th December 2021.

“Keeping pace with rapid change of technology in data processing and meet an increasing demand and needs of quality and user -friendly information is among the challenges that need to be addressed by National Meteorological Services including Tanzania Meteorological Authority (TMA), particularly when considering increasing climate variability and changes in the climate system”. Urged Dr. Agnes Kijazi, TMA Director General and Third Vice President of Word Meteorological Organization (WMO) during the official opening of training workshop on the latest long rabge forecasting Tools held at Kibaha, Pwani from 13th – 16th December 2021.

On additional to that, Dr. Kijazi insisted the participants to ensure they acquire new skills, become conversant with forecasting tools in order to enhance forecasting services at TMA as well as meeting increasing demand of quality weather forecast.

The aim of the training is to enhancing the capacity of TMA in accessing, understanding and use the Latest Long-Range Forecasting Tools. It is supported by Korean Meteorological Administration (KMA) through the Word Meteorological Organization (WMO) with technical support from IGAD Climate Prediction and Application Centre (ICPAC).



 

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...