Wednesday, April 15, 2026

TMA ENHANCES REGIONAL COOPERATION AND CAPACITY BUILDING IN METEOROLOGICAL SERVICES THROUGH WMO CAPACITY-BUILDING PROGRAMME

 TMA ENHANCES REGIONAL COOPERATION AND CAPACITY BUILDING IN METEOROLOGICAL SERVICES THROUGH WMO CAPACITY-BUILDING PROGRAMME 










Dodoma, 13 April 2026


The Tanzania Meteorological Authority (TMA) through the World Meteorological Organization (WMO) capacity building programne, hosted a regional delegation from the Institut Géographique du Burundi (IGEBU) and the South Sudan Meteorological Services (SSMS) for Practical training and capacity building on Numerical Weather Prediction (NWP), Severe Weather Forecasting, and Quality Management Systems (QMS) held from 12th to 17th April 2026 in Tanzania.


Organised through WMO Climate Risk and Early Warning Systems  (CREWS) Project,  the visit aimed at strengthening technical capacity of  IGEBU and SSMS Experts  in meteorological service delivery, particularly in the areas of NWP, QMS and Severe Weather Forecasting.


Opening the programme, TMA Director General and Vice-Chair of the Intergovernmental Panel on Climate change (IPCC) Dr. Ladislaus Chang’a, underscored Tanzania’s commitment in strengthening  regional cooperation and in providing training and technical support to  other NMHS including through various WMO programme.


“This practical visit demonstrates our strong commitment to advancing meteorological services not only in Tanzania, but across Africa, including through sharing our experience, knowledge and technical capacity in various aspects of meteorological services. Through South-South Collaboration and Cross-Learning, we can accelerate the enhancement of our service delivery in the continent and build resilience against weather and climate challenges. We are honored to host you here at TMA, both in Dodoma and Dar es Salaam.” Said Dr Chang'a


 Zablon Shilenje a representative  from WMO regional office for Africa(RA I) on behalf of Director of WMO Africa, Dr. Agnes Kijazi expressed the appreciation for Tanzania leadership and commitment to regional collaboration. 

“We are grateful to Tanzania for its leadership and for sharing its expertise, as well as for its continued support to South Sudan and Burundi. It is important that we move forward together and ensure that no one is left behind. Capacity building plays a critical role in strengthening meteorological services".Saidi Mr. Zablon


Permanent representative of Burundi with WMO, Mr Deogratias Babonwanayo commended the initiative and thanked TMA for providing technical support to Burundi “We are grateful for the opportunity to come to TMA and learn from their experience in implementing Quality Management Systems. This visit and the knowledge tha we get,  will greatly support the enhancement of our services in Burundi.”


Mr Mojwok Ogawi Modo who is the Permanent representative for South Sudan with WMO  also highlighted the importance of the Visit. 

“This visit will provide valuable practical insights and strengthen our capacity in QMS, NWP and in Severe Weather Forecasting. We are confident that the lessons learned here will contribute to improving meteorological services in South Sudan.”


This practical visit reflects Tanzania’s ongoing leadership in fostering regional integration and cooperation in meteorological services reinforcing efforts and commitment to strengthening climate services for sustainable development.

TMA YAENDELEA KUWAJENGEA UWEZO TAASISI ZA HALI YA HEWA BARANI AFRIKA KUPITIA PROGRAMU ZA WMO

 TMA YAENDELEA KUWAJENGEA UWEZO TAASISI ZA HALI YA HEWA BARANI AFRIKA KUPITIA PROGRAMU ZA WMO









Dodoma, 13 Aprili 2026


Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imewapokea na Viongozi na Wataalamu wa hali ya hewa kutoka Taasisi ya Hali ya Hewa ya Burundi (IGEBU) na Taasisi ya Hali ya Hewa ya Sudan Kusini (SSMS) kwa ajili ya mafunzo ya vitendo  kuhusu Utabiri wa Hali ya Hewa kwa Njia za Mahesabu (NWP), utabiri wa hali mbaya ya hewa, na mifumo ya usimamizi wa ubora (QMS). Mafunzo hayo yanafanyika kuanzia tarehe 13 hadi 17 Aprili 2026 Tanzania.


Mafunzo haya yameandaliwa kwa ushirikiano na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) kupitia Mradi wa Kuboresha Mfumo wa Utoaji wa Tahadhari za Hali Mbaya ya Hewa (CREWS). Mafunzo  yanalenga kuwajengea uwezo wa utaalamu na mbinu bora katika utoaji wa huduma za hali ya hewa katika ukanda wa Afrika Mashariki.


Akifungua programu ya mafunzo hayo kwa vitendo, Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi, Dkt. Ladislaus Chang’a, alisisitiza dhamira ya Tanzania kupitia TMA katika kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika masuala ya huduma za hali ya hewa.


“Mafunzo haya yanaonesha dhamira yetu thabiti ya kuboresha huduma za hali ya hewa si tu nchini Tanzania bali katika ukanda mzima wa Afrika. Kupitia ushirikiano na mafunzo haya, tunaweza kuboresha utoaji wa huduma na kujenga uimara na ustaimilivu dhidi ya changamoto za mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi. Tunafuraha kubwa kuwakaribisha hapa TMA katika Ofisi zetu za Dodoma na Dar es Salaam.”Alizungumza Dkt. Chang'a.


Akizungumza kwa niaba ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani, Bw. Zablon Shilenje alitoa shukrani kwaniaba ya Mkurugenzia wa WMO Afrika, Dkt.Agnes Kijazi kwa uongozi wa Tanzania na dhamira yake katika kutoa ushirikiano wa kikanda.


“Tunashukuru Tanzania kwa kuendeleza ushirikiano hususani katika eneo la kuwajengea uwezo wataalamu wa hali ya hewa kutoka Afrika ikiwemo Sudan Kusini na Burundi. Ni muhimu tusonge mbele pamoja na kuhakikisha hakuna anayebaki nyuma katika uboreshaji huduma za hali ya hewa".Alisema Bw. Zablon


Naye, Mkurugenzi Mkuu wa IGEBU, Bw. Deogratias Babonwanayo, alipongeza mpango huo:“Tunashukuru kwa fursa ya kushirikiana na TMA na kujifunza kutokana na uzoefu wao katika utekelezaji wa mifumo ya usimamizi wa ubora. Mafunzo haya yatachangia kwa kiasi kikubwa kuboresha huduma zetu nchini Burundi.”


Kwa upande wake, Bw. Mojwok Ogawi Modo, Mkurugenzi Mkuu SSMS, alieleza umuhimu wa ziara hiyo:“Ziara hii itatoa nyenzo muhimu kwa vitendo na kuendelea kuimarisha ushirikiano wetu na washirika wa kikanda hususani Tanzania. Tunaamini kwamba mafunzo tunayoyapata hapa yatachangia kuboresha huduma za hali ya hewa nchini Sudan Kusini".


Ziara hii ya vitendo inaakisi uwekezaji endelevu wa Tanzania katika kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika sekta ya hali ya hewa, na kuboresha miundombinu ya utoaji huduma za hali ya hewa kwa maendeleo endelevu.

Sunday, April 12, 2026

TANZANIA YAJIPANGA NA UTEKELEZAJI WA MRADI WA SOFF AWAMU YA TATU.

 















Morogoro, Tanzania; 09 Aprili 2025.

 

Mwenyekiti Mwenza wa Kamati Tendaji ya Mradi wa SOFF na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dkt. Ladislaus Chang’a alifungua rasmi Mkutano wa Tatu wa Kamati Tendaji ya Mradi wa Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Kuimarisha Uangazi wa Hali ya Hewa - SOFF (PSC-3) tarehe 9 Aprili 2026 katika Hoteli ya Morena, Morogoro, na kusisitiza dhamira ya Tanzania ya kufikia malengo ya utekelezaji wa Mradi wa SOFF nchini ili kukidhi mahitaji ya Mtandao wa Kidunia wa Uangazi wa Hali ya Hewa (GBON)

 

Akizungumza na wajumbe wa Kamati, Dkt. Chang’a alisema, Mradi wa SOFF unaingia mwaka wa tatu. Hivyo, shughuli zilizopangwa chini ya mradi huu zinakusudia kuhakikisha kuwa ifikapo Desemba 2027, Tanzania itakuwa imefikia malengo ya mradi ya kuhakikisha miundombinu ya hali ya hewa na mifumo yake imesimikwa sambamba na kuwajengea uwezo wataalamu.

 

Mkutano huo ulitoa fursa ya kutathimini maendeleo ya mradi na kufanya maamuzi yatakayoainisha njia na namna bora ya kusonga mbele. "Katika kikao hiki wajumbe wa PSC watapitia taarifa ya maendeleo ya mradi, mpango kazi wa mwaka 2026, na kutoa maelekezo ya kuhakikisha Mradi unafikia malengo ya GBON ifikapo Desemba 2027.". Alisisitiza Dkt. Chang’a

 

Vilevile aliipongeza Sekretarieti na Timu ya Utekelezaji wa Mradi kwa hatua nzuri iliyofikiwa na kuhimiza kuongeza bidii ili kufikia malengo ya mradi na kulinda sifa kubwa ya Tanzania kikanda na kimataifa katika sayansi ya hali ya hewa.

 

"Hatua na mafanikio yaliyofikiwa hadi sasa ni matokeo ya juhudi za pamoja baina ya wadau wote wa Mradi, lazima tuendelee kufanya kazi kwa bidii ili Tanzania iendelee kuwa mfano wa kuigwa katika ukanda huu," alisema Dkt. Chang’a.

 

Awali Mwenyekiti Mwenza na Mwakilishi Mkazi Msaidizi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Bw. Amon Manyama alisema kipaumbele cha UNDP ni kuhakikisha kazi zilizopangwa zinakamilika kwa wakati, ikiwemo ununuzi na ufungaji wa vifaa pamoja na kuwezesha mifumo ya uendeshaji ili kuhakikisha kuwa vifaa hivyo vya hali ya hewa vinafanya kazi katika viwango vya ubora.

 

SOFF ni Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Kuimarisha Uangazi wa Hali ya Hewa kwa Nchi zinazoendelea na Nchi za Visiwa vidogo. Lengo la Mradi ni kuimarisha huduma za hali ya hewa katika kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi ili kulinda maisha ya watu na mali ikiwemo kuboresha zaidi miundombinu ya uangazi wa hali ya hewa na kuhakikisha Tanzania inakidhi mahitaji ya wadau wa Kitaifa na Kimataifa. Mradi huu unatekelezwa kwa muda wa miaka minne kuanzia Julai 2024 hadi Desemba 2027.

 

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...