Monday, December 16, 2019

RC TANGA AIPONGEZA TMA KWA KUWA MFANO KATIKA UTUNZAJI WA MAZINGIRA.

Mkuu wa Mkoa Tanga Mhe. Martin Shigela akipokea zawadi toka kwa meneja TMA kituo cha Handeni Ndg. Fabian Severine, alipotembelea banda la TMA katika maonesho ya siku ya chakula duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Handeni Square, Tanga kuanzia Tarehe 09-14 Disemba, 2019.

Mkuu wa Mkoa Tanga Mhe. Martin Shigela akipata elimu kutoka kwa meneja TMA kituo cha Handeni Ndg. Fabian Severine, juu ya namna taarifa za hali ya hewa zinavyoweza kutumika katika kushauri wadau ili kukabiliana na changamoto mbalimbali kwenye sekta zao, kupitia maonesho ya "ONE STOP JAWABU" yaliyofanyika katika viwanja vya Handeni Square, Tanga kuanzia Tarehe 09-14 Disemba, 2019.




Matukio mbalimbali katika picha wakati wataalamu wa hali ya hewa kutoka TMA wakiendelea kutoa elimu kwa wadau, namna ya kutumia ushauri wa kitaalam kutoka TMA ili kukabiliana na changamoto mbalimbali kwenye sekta zao, kupitia maonesho ya "ONE STOP JAWABU" yaliyofanyika katika viwanja vya Handeni Square, Tanga kuanzia Tarehe 09-14 Disemba, 2019.







Matukio mbalimbali katika picha wakati wageni wakipokea zawadi mara walipotembelea banda la TMA kupitia maonesho ya "ONE STOP JAWABU" yaliyofanyika katika viwanja vya Handeni Square, Tanga kuanzia Tarehe 09-14 Disemba, 2019

Meneja TMA - Handeni Ndg. Fabian Severine, akipata nafasi ya upendeleo toka kwa mshereheshaji ili kutoa elimu ya hali ya hewa katika maonesho ya "ONE STOP JAWABU" yaliyofanyika katika viwanja vya Handeni Square, Tanga kuanzia Tarehe 09-14 Disemba, 2019


Handeni, 14/12/2019;
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Martin Shigela ameipongeza Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kwa kuwa mfano katika utunzaji wa mazingira. Pongezi hizo zilitolewa alipotembelea banda la TMA katika maonesho ya "ONE STOP JAWABU" ambayo yalifanyika katika viwanja vya Handeni Square, Tanga kuanzia Tarehe 09-14 Disemba, 2019.

"Nawapongeza kwa  kuwa mfano wa utunzaji wa mazingira kupitia utoaji zawadi za mifuko bora ambayo ni rafiki wa mazingira". Alisema Mhe. Shigela.

Kupitia maonesho hayo, wadau mbalimbali waliweza kutembelea banda la TMA na kupata ushauri wa kitaalam juu ya matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa katika kukabiliana na changamoto mbalimbali kwenye sekta zao.

Aidha, kupitia maonesho hayo zaidi ya wadau 160 waliweza kuelekezwa jinsi ya kupata taarifa za hali ya hewa kupitia njia mbalimbali za mawasiliano ikiwemo tovuti pamoja na mitandao ya kijamii ya TMA.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...