Tuesday, June 2, 2026

NAIBU WAZIRI AHIMIZA USHIRIKIANO KUSAMBAZA TAARIFA ZA HALI YA HEWA KWA WANANCHI WA VIJIJINI

Dodoma, Juni 1, 2026.





Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Reuben Nhamanilo Kwagilwa, ameitaka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kuendelea kuimarisha ushirikiano na wadau mbalimbali ili kuhakikisha taarifa za hali ya hewa zinawafikia wananchi wote, hususan wanaoishi katika maeneo ya vijijini na maeneo ya mbali yanayokabiliwa na changamoto za upatikanaji wa huduma za mawasiliano.


Mhe. Kwagilwa ameyasema hayo alipotembelea banda la TMA wakati wa Ufunguzi wa Maonesho ya Siku ya Mazingira Duniani 2026 yanayofanyika kuanzia tarehe 1 hadi 5 Juni 2026 katika Viwanja vya Jakaya Kikwete Convention Centre (JKCC), jijini Dodoma, chini ya kauli mbiu isemayo "Dira 2050: Tuwajibike Kukijanisha Tanzania"


Akizungumza na wataalamu wa TMA, Mhe. Kwagilwa ameipongeza mamlaka hiyo kwa kazi kubwa inayoendelea kufanya katika utoaji wa huduma za hali ya hewa na kusisitiza umuhimu wa kuhakikisha taarifa hizo zinawafikia wananchi wanaozitegemea katika shughuli zao za kila siku, hususan sekta ya kilimo.

“Nawapongeza kwa kazi nzuri mnayoifanya na tunaona matokeo yake. Hata hivyo, kuna umuhimu wa kuhakikisha taarifa hizi zinawafikia wananchi waliopo kwenye maeneo ya mbali ambao wanategemea utabiri wa hali ya hewa katika shughuli zao za kimsimu, hasa kilimo,” amesema Mhe. Kwagilwa.


Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya TMA na Vituo vya Kijamii vya Uhimilivu dhidi ya Mabadiliko ya Tabianchi (CCCRC) ili vituo hivyo viwe daraja muhimu la kufikisha taarifa za hali ya hewa kwa wananchi ngazi ya jamii na kuwawezesha kupata taarifa sahihi zinazohusu maeneo yao pamoja na mwongozo wa hatua stahiki za kuchukua katika misimu mbalimbali.


Ushiriki wa TMA katika maonesho hayo ni sehemu ya juhudi za Mamlaka kuendelea kusogeza huduma za hali ya hewa kwa wananchi, kuongeza uelewa wa matumizi ya taarifa za hali ya hewa katika sekta mbalimbali za maendeleo na kuimarisha ushirikiano na wadau

TMA inawakaribisha wananchi, wadau wa mazingira, watafiti, wanafunzi na washiriki wote wa maonesho hayo kutembelea banda la TMA ili kujifunza zaidi kuhusu huduma za hali ya hewa na mifumo ya utoaji wa utabiri wa hali ya hewa.

Monday, May 25, 2026

KIPUPWE 2026: UPEPO ULIOPUNGUA NGUVU KIDOGO UNATARJIWA KATIKA MAENEO MENGI YA NCHI.


 Dar es Salaam,Tarehe 25/05/2026:

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa rasmi mwelekeo wa hali ya hewa katika kipindi cha mwezi Juni hadi Agosti 2026 (Kipupwe). Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC), Dkt. Ladislaus Chang’a aliwataka wananchi kufuatilia na kuutumia ipasavyo utabiri wa msimu wa Kipupwe 2026, hasa ikizingatiwa kuwa katika kipindi hicho baadhi ya maeneo yanatarajia kupata vipindi vichache vya upepo mkali mwezi Juni na Julai 2026.

 

“Msimu wa Kipupwe 2026 unatarajiwa kutawaliwa na upepo uliopungua nguvu kidogo kama ilivyo kawaida, utakaovuma kutoka Kusini Mashariki kwa maeneo mengi ya nchi, na vipindi vichache vya upepo mkali utakaovuma kutoka kusini hususan katika kipindi cha miezi ya Juni na Julai 2026 hususani katika maeneo ya ukanda wa pwani ya Bahari ya Hindi na maeneo ya nchi kavu”. Alisema Dkt. Chang’a

Akizungumzia hali ya baridi Dkt. Chang’a alisema vipindi vya baridi zaidi vikitarajiwa kujitokeza katika mwezi Julai 2026, aidha, baridi ya wastani hadi joto kiasi inatarajiwa katika baadhi ya maeneo ya nchi.

“Hali ya baridi ya wastani hadi joto kiasi inatarajiwa katika maeneo ya Kanda ya Ziwa Victoria, Kanda ya magharibi, Kanda ya kusini, Nyanda za juu kusini- magharibi pamoja na Mkoa wa Singida. Hata hivyo, hali ya joto kiasi hadi baridi ya wastani ikitarajiwa katika maeneo ya Ukanda wa pwani ya kaskazini na maeneo ya nchi kavu, Nyanda za juu kaskazini mashariki, Ukanda wa pwani ya kusini pamoja na mkoa wa Dodoma huku vipindi vya baridi zaidi vikitarajiwa kujitokeza katika mwezi Julai 2026.” Alisema Dkt. Chang’a.

Akielezea kuhusu mwenendo wa mvua Dkt. Chang’a alisema vipindi vya mvua za nje ya msimu vinatarajiwa katika maeneo ya ukanda wa Ziwa Victoria hususan Mkoa wa Mara, ukanda wa mwambao wa pwani na maeneo ya nchi kavu pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba, na sehemu zenye miinuko za nyanda za juu kaskazini mashariki.

Kwa upande wa Athari zinazoweza kujitokeza Dkt. Chang’a alisema Magonjwa yanayohusiana na hali ya hewa ya baridi kama vile homa ya mapafu na magonjwa ya mifugo yanaweza kujitokeza. Hali ya vumbi linalosababishwa na upepo linaweza kupelekea uwepo wa magonjwa kama vile ya macho, mafua na magonjwa mengine yanayohusiana nayo, huku upungufu wa maji na malisho yakitarajiwa kujitokeza, na mwishoni alishauri Mamlaka husika pamoja na jamii kuchukua hatua stahiki kulingana na ushauri wa kitaalamu kutoka kwa wataalamu katika sekta zao.

Kwa taarifa zaidi tembeleahttps://www.meteo.go.tz/uploads/text-editor/files/Mwelekeo%20wa%20msimu%20wa%20Kipupwe%20(Juni-Agosti)%20-2026_1779700325.pdf

Thursday, May 21, 2026

TMA YATOA ELIMU YA HALI YA HEWA KWA WAVUVI KUPITIA MRADI WA ECOFISH

Pemba, 20 Mei 2026.




















7





Mradi wa ECOFISH unaotekelezwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Denmark kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Shirika la Denmark la Maendeleo ya Kimataifa (DANIDA), unaendelea kuboresha shughuli za uvuvi kwa jamii ya Pwani na kuimarisha huduma za tahadhari za mapema za hali ya hewa nchini.


Katika utekelezaji wa mradi huo, wataalamu kutoka TMA walikutana na wavuvi pamoja na wakulima wa Mwani kwa lengo la kujionea hali halisi ya shughuli zao za kiuchumi na changamoto zitokanazo na mabadiliko ya hali ya hewa  wanazokabiliana nazo, sambamba na kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa katika shughuli za uvuvi na kilimo cha Mwani. Ziara hiyo iliambatana na semina maalum iliyowakutanisha wavuvi na wakulima wa Mwani ikiwa ni sehemu ya juhudi za mradi huo katika kuongeza uelewa wa jamii kuhusu umuhimu wa matumizi ya taarifa za hali ya hewa katika kufanya maamuzi sahihi na salama.


Akizungumza katika semina hiyo, Mtaalamu wa Hali ya Hewa kutoka TMA na msimamizi wa mradi, Dkt. Sarah Emerald Osima, alisema mradi wa ECOFISH una mchango mkubwa katika kuimarisha huduma za hali ya hewa na ustahimilivu wa jamii za Pwani kupitia tafiti, elimu na teknolojia za tahadhari za mapema.


Dkt. Sarah aliendelea kusema mradi huo pia umewezesha udhamini wa masomo kwa wanafunzi saba wa shahada za uzamili na uzamivu kutoka Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI), Taasisi ya Sayansi za Bahari ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (IMS) pamoja na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), ambapo mmoja wao ni mfanyakazi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA). Alisema hatua hiyo inalenga kujenga wataalamu watakaosaidia sekta ya uvuvi na hali ya hewa kwa siku zijazo.


Aidha, wananchi wa kisiwani hapoo wamepongeza mradi huu wa ECOFISH na TMA kwa kuwapatia elimu hiyo, wakisema imewasaidia kuelewa na kutumia taarifa za hali ya hewa katika kupanga shughuli zao za uvuvi.


“Sasa tunajua umuhimu wa kutafuta na kutumia taarifa za hali ya hewa, jambo ambalo hapo awali tulikuwa tunalifanya kwa uelewa mdogo. Kwa sasa tumejifunza mambo mengi ikiwemo namna ya kutafsiri taarifa hizo kama zinavyotolewa na wataalamu,” alisema Afisa Uvuvi kutoka Wilaya ya Wete, Ndugu,Suleiman Ali Amadi.

Monday, May 18, 2026

TMA NA BRAC MAENDELEO TANZANIA WAJADILI MIKAKATI YA KUIMARISHA USAMBAZAJI NA MATUMIZI YA TAARIFA ZA HALI YA HEWA.





Dodoma, Mei 15, 2026 

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)  na BRAC Maendeleo Tanzania walifanya kikao Makao Makuu ya TMA jijini Dodoma, wakijadili mikakati ya kuimarisha usambazaji na matumizi ya taarifa za hali ya hewa nchini. 


Kikao hicho kiliongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC), Dkt. Ladislaus Chang’a, kwa kuwakaribisha wajumbe wa BRAC Maendeleo Tanzania na kueleza kuwa TMA inathamini ushirikiano na wadau katika kuboresha huduma za hali ya hewa. Alisema mkutano huo unatoa fursa ya taasisi hizo mbili kuelewana na kuchunguza maeneo ya ushirikiano katika huduma za hali ya hewa, tahadhari za mapema na hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Pia alieleza kuwa TMA ipo katika mageuzi ya kidigitali yanayolenga kuboresha utoaji wa huduma kwa njia za kisasa.


Dkt. Chang’a Alieleza dhamira ya TMA kuendelea kuboresha huduma za hali ya hewa na ushawishi wa Tanzania katika maduala ya hali ya hewa katika bara la Africa na ukanda wa Nchi zinazoendelea.  Aliwashukuru BRAC kwa majadiliano yenye tija na kwa mchango wao katika kuelimisha Jamii na kuimarisha usambazaji wa Taarifa za hali ya hewa kwa jamii. Alisisitiza na kuhamasisha ushiriki wa WADAU wengi katika Mkutano wa nne wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) Unaolenga kuboresha miongozo ya Utabiri wa Hali ya Hewa (Operational Climate Prediction OCP-4) na Unatarajiwa kufanyika Arusha kuanzia 29 Juni hadi 3 Julai 2026.


Kwa upande wake Bw. Degefu Getachew Kelbiso, Meneja Mwandamizi wa Programu ya Hali ya Hewa ya Kimataifa na BRAC Maendeleo Tanzania, alieleza kuhusu mpango wa “BigBet” unaolenga kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kupitia huduma za taarifa za hali ya hewa, kilimo kinachozingatia mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi, masoko na uimarishaji wa maisha ya jamii katika nchi kadhaa ikiwemo Tanzania. 


Bw. Degefu alieleza haja ya kuimarisha ushirikiano katika kuendelea kuboresha upatikanaji, usambazaji,  tafsiri  na matumizi ya taarifa za hali ya hewa  kwa watumiaji wa mwisho na katika sekta zote za kiuchumi na kijamii  na katika miradi ya jamii na maendeleo.

Saturday, May 16, 2026

KAMATI YA URATIBU YA MRADI WA SOFF YAKUTANA JIJINI DODOMA








Dodoma, 14 Mei 2026

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), kwa kushirikiana na Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), walifanya kikao kazi cha tano cha Kamati ya Uratibu  wa Mradi wa SOFF (Systematic Observations Financing Facilit)  katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.

Kikao hicho kiliwakutanisha wataalamu muhimu ili kupitia maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa SOFF na kujadili vipaumbele vya kimkakati kwa mwaka 2026, vinavyolenga kuhakikisha ufanisi katika utekelezaji wa shughuli za mradi.


Majadiliano yalijikita katika utekelezaji wa Mpango Kazi wa Mwaka 2026,  ufuatiliaji na tathmini ya mradi, pamoja na shughuli za mawasiliano na uhamasishaji zilizopangwa kwa mwaka 2026. Kamati pia ilipitia maamuzi na maelekezo kutoka kikao cha Tatu cha Kamati Tendaji ya Mradi wa SOFF kilihofanyika Aprili 2026.


Wakizungumza katika ufunguzi, Wenyeviti wenza wa kamati hiyo, Dkt. Paschal Waniha kutoka TMA na Dkt.Abbas Kitogo kutoka UNDP, walisisitiza umuhimu wa kuendelea kushirikiana kikamilifu ili kuhakikisha utekelezaji unafanyika kwa wakati katika shughuli zote zilizopangwa za mradi wa SOFF Tanzania.Aidha,

kikao kilihitimishwa kwa wajumbe kutoa dhamira ya pamoja ya kuimarisha uratibu, kuharakisha utekelezaji wa shughuli zilizopangwa, na kuongeza ufanisi wa jumla wa mradi wa SOFF nchini Tanzania.

THE FIFTH SOFF PROJECT TECHNICAL COORDINATION COMMITTEE IN TANZANIA CONVENES IN DODOMA

Dodoma, 14th May 2026;

The Tanzania Meteorological Authority in collaboration with the United Nations Development Programme (UNDP)  convened for the Fifth Meeting of the Systematic Observations Financing Facility (SOFF) Project Technical Coordination Committee (PTCC-5) at Morena Hotel in Dodoma.

The meetin








g brought together Members of the PTCC and key experts to deliberate on the implementation progress of the SOFF project and to discuss strategic priorities for implementation of the project in 2026 aimed at ensuring efficiency in the implementation of project activities.


The agenda of the meeting focused more on the implementation of the approved 2026 SOFF Project Annual Workplan, project monitoring report, as well as planned monitoring, communication and outreach activities for 2026. The committee also strategized on the implementation of decisions and directives by the SOFF Project Steering Committee (PSC), which were given by the PSC at the 3rd meeting held on 9th April 2026.


Speaking during the opening session, the PTCC Co-Chairs, Dr. Paschal Waniha and Dr. Abbas Kitogo from TMA and UNDP respectively, emphasized the importance of continued effective collaboration to ensure timely implementation of all planned SOFF project activities. 


Also the PTCC-5 meeting concluded with a shared commitment among PTCC members to strengthen coordination, accelerate the implementation of planned activities, and enhance the overall effectiveness of the SOFF project in Tanzania

Wednesday, April 15, 2026

TMA ENHANCES REGIONAL COOPERATION AND CAPACITY BUILDING IN METEOROLOGICAL SERVICES THROUGH WMO CAPACITY-BUILDING PROGRAMME

 TMA ENHANCES REGIONAL COOPERATION AND CAPACITY BUILDING IN METEOROLOGICAL SERVICES THROUGH WMO CAPACITY-BUILDING PROGRAMME 










Dodoma, 13 April 2026


The Tanzania Meteorological Authority (TMA) through the World Meteorological Organization (WMO) capacity building programne, hosted a regional delegation from the Institut Géographique du Burundi (IGEBU) and the South Sudan Meteorological Services (SSMS) for Practical training and capacity building on Numerical Weather Prediction (NWP), Severe Weather Forecasting, and Quality Management Systems (QMS) held from 12th to 17th April 2026 in Tanzania.


Organised through WMO Climate Risk and Early Warning Systems  (CREWS) Project,  the visit aimed at strengthening technical capacity of  IGEBU and SSMS Experts  in meteorological service delivery, particularly in the areas of NWP, QMS and Severe Weather Forecasting.


Opening the programme, TMA Director General and Vice-Chair of the Intergovernmental Panel on Climate change (IPCC) Dr. Ladislaus Chang’a, underscored Tanzania’s commitment in strengthening  regional cooperation and in providing training and technical support to  other NMHS including through various WMO programme.


“This practical visit demonstrates our strong commitment to advancing meteorological services not only in Tanzania, but across Africa, including through sharing our experience, knowledge and technical capacity in various aspects of meteorological services. Through South-South Collaboration and Cross-Learning, we can accelerate the enhancement of our service delivery in the continent and build resilience against weather and climate challenges. We are honored to host you here at TMA, both in Dodoma and Dar es Salaam.” Said Dr Chang'a


 Zablon Shilenje a representative  from WMO regional office for Africa(RA I) on behalf of Director of WMO Africa, Dr. Agnes Kijazi expressed the appreciation for Tanzania leadership and commitment to regional collaboration. 

“We are grateful to Tanzania for its leadership and for sharing its expertise, as well as for its continued support to South Sudan and Burundi. It is important that we move forward together and ensure that no one is left behind. Capacity building plays a critical role in strengthening meteorological services".Saidi Mr. Zablon


Permanent representative of Burundi with WMO, Mr Deogratias Babonwanayo commended the initiative and thanked TMA for providing technical support to Burundi “We are grateful for the opportunity to come to TMA and learn from their experience in implementing Quality Management Systems. This visit and the knowledge tha we get,  will greatly support the enhancement of our services in Burundi.”


Mr Mojwok Ogawi Modo who is the Permanent representative for South Sudan with WMO  also highlighted the importance of the Visit. 

“This visit will provide valuable practical insights and strengthen our capacity in QMS, NWP and in Severe Weather Forecasting. We are confident that the lessons learned here will contribute to improving meteorological services in South Sudan.”


This practical visit reflects Tanzania’s ongoing leadership in fostering regional integration and cooperation in meteorological services reinforcing efforts and commitment to strengthening climate services for sustainable development.

TMA YAENDELEA KUWAJENGEA UWEZO TAASISI ZA HALI YA HEWA BARANI AFRIKA KUPITIA PROGRAMU ZA WMO

 TMA YAENDELEA KUWAJENGEA UWEZO TAASISI ZA HALI YA HEWA BARANI AFRIKA KUPITIA PROGRAMU ZA WMO









Dodoma, 13 Aprili 2026


Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imewapokea na Viongozi na Wataalamu wa hali ya hewa kutoka Taasisi ya Hali ya Hewa ya Burundi (IGEBU) na Taasisi ya Hali ya Hewa ya Sudan Kusini (SSMS) kwa ajili ya mafunzo ya vitendo  kuhusu Utabiri wa Hali ya Hewa kwa Njia za Mahesabu (NWP), utabiri wa hali mbaya ya hewa, na mifumo ya usimamizi wa ubora (QMS). Mafunzo hayo yanafanyika kuanzia tarehe 13 hadi 17 Aprili 2026 Tanzania.


Mafunzo haya yameandaliwa kwa ushirikiano na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) kupitia Mradi wa Kuboresha Mfumo wa Utoaji wa Tahadhari za Hali Mbaya ya Hewa (CREWS). Mafunzo  yanalenga kuwajengea uwezo wa utaalamu na mbinu bora katika utoaji wa huduma za hali ya hewa katika ukanda wa Afrika Mashariki.


Akifungua programu ya mafunzo hayo kwa vitendo, Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi, Dkt. Ladislaus Chang’a, alisisitiza dhamira ya Tanzania kupitia TMA katika kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika masuala ya huduma za hali ya hewa.


“Mafunzo haya yanaonesha dhamira yetu thabiti ya kuboresha huduma za hali ya hewa si tu nchini Tanzania bali katika ukanda mzima wa Afrika. Kupitia ushirikiano na mafunzo haya, tunaweza kuboresha utoaji wa huduma na kujenga uimara na ustaimilivu dhidi ya changamoto za mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi. Tunafuraha kubwa kuwakaribisha hapa TMA katika Ofisi zetu za Dodoma na Dar es Salaam.”Alizungumza Dkt. Chang'a.


Akizungumza kwa niaba ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani, Bw. Zablon Shilenje alitoa shukrani kwaniaba ya Mkurugenzia wa WMO Afrika, Dkt.Agnes Kijazi kwa uongozi wa Tanzania na dhamira yake katika kutoa ushirikiano wa kikanda.


“Tunashukuru Tanzania kwa kuendeleza ushirikiano hususani katika eneo la kuwajengea uwezo wataalamu wa hali ya hewa kutoka Afrika ikiwemo Sudan Kusini na Burundi. Ni muhimu tusonge mbele pamoja na kuhakikisha hakuna anayebaki nyuma katika uboreshaji huduma za hali ya hewa".Alisema Bw. Zablon


Naye, Mkurugenzi Mkuu wa IGEBU, Bw. Deogratias Babonwanayo, alipongeza mpango huo:“Tunashukuru kwa fursa ya kushirikiana na TMA na kujifunza kutokana na uzoefu wao katika utekelezaji wa mifumo ya usimamizi wa ubora. Mafunzo haya yatachangia kwa kiasi kikubwa kuboresha huduma zetu nchini Burundi.”


Kwa upande wake, Bw. Mojwok Ogawi Modo, Mkurugenzi Mkuu SSMS, alieleza umuhimu wa ziara hiyo:“Ziara hii itatoa nyenzo muhimu kwa vitendo na kuendelea kuimarisha ushirikiano wetu na washirika wa kikanda hususani Tanzania. Tunaamini kwamba mafunzo tunayoyapata hapa yatachangia kuboresha huduma za hali ya hewa nchini Sudan Kusini".


Ziara hii ya vitendo inaakisi uwekezaji endelevu wa Tanzania katika kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika sekta ya hali ya hewa, na kuboresha miundombinu ya utoaji huduma za hali ya hewa kwa maendeleo endelevu.

Sunday, April 12, 2026

TANZANIA YAJIPANGA NA UTEKELEZAJI WA MRADI WA SOFF AWAMU YA TATU.

 















Morogoro, Tanzania; 09 Aprili 2025.

 

Mwenyekiti Mwenza wa Kamati Tendaji ya Mradi wa SOFF na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dkt. Ladislaus Chang’a alifungua rasmi Mkutano wa Tatu wa Kamati Tendaji ya Mradi wa Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Kuimarisha Uangazi wa Hali ya Hewa - SOFF (PSC-3) tarehe 9 Aprili 2026 katika Hoteli ya Morena, Morogoro, na kusisitiza dhamira ya Tanzania ya kufikia malengo ya utekelezaji wa Mradi wa SOFF nchini ili kukidhi mahitaji ya Mtandao wa Kidunia wa Uangazi wa Hali ya Hewa (GBON)

 

Akizungumza na wajumbe wa Kamati, Dkt. Chang’a alisema, Mradi wa SOFF unaingia mwaka wa tatu. Hivyo, shughuli zilizopangwa chini ya mradi huu zinakusudia kuhakikisha kuwa ifikapo Desemba 2027, Tanzania itakuwa imefikia malengo ya mradi ya kuhakikisha miundombinu ya hali ya hewa na mifumo yake imesimikwa sambamba na kuwajengea uwezo wataalamu.

 

Mkutano huo ulitoa fursa ya kutathimini maendeleo ya mradi na kufanya maamuzi yatakayoainisha njia na namna bora ya kusonga mbele. "Katika kikao hiki wajumbe wa PSC watapitia taarifa ya maendeleo ya mradi, mpango kazi wa mwaka 2026, na kutoa maelekezo ya kuhakikisha Mradi unafikia malengo ya GBON ifikapo Desemba 2027.". Alisisitiza Dkt. Chang’a

 

Vilevile aliipongeza Sekretarieti na Timu ya Utekelezaji wa Mradi kwa hatua nzuri iliyofikiwa na kuhimiza kuongeza bidii ili kufikia malengo ya mradi na kulinda sifa kubwa ya Tanzania kikanda na kimataifa katika sayansi ya hali ya hewa.

 

"Hatua na mafanikio yaliyofikiwa hadi sasa ni matokeo ya juhudi za pamoja baina ya wadau wote wa Mradi, lazima tuendelee kufanya kazi kwa bidii ili Tanzania iendelee kuwa mfano wa kuigwa katika ukanda huu," alisema Dkt. Chang’a.

 

Awali Mwenyekiti Mwenza na Mwakilishi Mkazi Msaidizi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Bw. Amon Manyama alisema kipaumbele cha UNDP ni kuhakikisha kazi zilizopangwa zinakamilika kwa wakati, ikiwemo ununuzi na ufungaji wa vifaa pamoja na kuwezesha mifumo ya uendeshaji ili kuhakikisha kuwa vifaa hivyo vya hali ya hewa vinafanya kazi katika viwango vya ubora.

 

SOFF ni Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Kuimarisha Uangazi wa Hali ya Hewa kwa Nchi zinazoendelea na Nchi za Visiwa vidogo. Lengo la Mradi ni kuimarisha huduma za hali ya hewa katika kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi ili kulinda maisha ya watu na mali ikiwemo kuboresha zaidi miundombinu ya uangazi wa hali ya hewa na kuhakikisha Tanzania inakidhi mahitaji ya wadau wa Kitaifa na Kimataifa. Mradi huu unatekelezwa kwa muda wa miaka minne kuanzia Julai 2024 hadi Desemba 2027.

 

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...