Tuesday, December 17, 2019

MVUA KUBWA KATIKA MAENEO MENGI NCHINI.



 Dar es Salaam, 17 Disemba 2019:
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inatoa taarifa ya mrejeo kuhusu uwepo wa vipindi vya mvua kubwa katika maeneo mengi nchini. Mvua zinaendelea kusambaa katika maeneo ya Pwani ya kaskazini pamoja na kanda kati. 

Hivyo, tahadhari ya kuendelea kwa vipindi vya mvua kubwa inatolewa katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Pwani, Dar es salaam, Tanga, Morogoro, Dodoma, Singida pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba. Hali hiyo imetokana na kuimarika kwa ukanda mvua na kusogea katika maeneo hayo kutokana na mwenendo wa mkondo baridi katika eneo la kusini mwa Afrika. Hali hiyo ya vipindi vya mvua kubwa inatarajiwa kuendelea hadi alasiri ya leo tarehe 17 Disemba, 2019.

Aidha, Angalizo lililotolewa la vipindi vya mvua kubwa zinazoendelea katika baadhi ya maeneo ya Nyanda za juu kusini magharibi (Mikoa ya Rukwa, Songwe, Mbeya, Iringa), Mikoa wa Ruvuma, Lindi, Mtwara pamoja na maeneo ya kusini mwa mkoa wa Morogoro liendelee kuzingatiwa.

USHAURI: Wananchi wanashauriwa kuendelea kufuatilia utabiri wa saa 24 pamoja na tahadhari kila zinapotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania na kuchukua hatua.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...