Tuesday, August 25, 2020

MKURUGENZI MKUU WA TMA ASISITIZA NCHI WANACHAMA WA SADC KUPATA CHETI CHA UBORA WA KIMATAIFA-ISO 9001:2015.

Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa WMO, Dkt. Agnes Kijazi akieleza mafanikio katika mkutano wa SADC-SCOM.



Dar es Salaam: Tarehe 20 Agosti 2020

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ndogo ya Sekta ya Hali ya Hewa ya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) – “SADC Sub-Sectoral Committee on Meteorology (SADC SCOM)”, Dkt. Agnes Kijazi, amesisitiza nchi wanachama kuweka nguvu zaidi katika mpango wa kuhakikisha zinapata cheti cha ubora wa kimataifa kwenye utoaji wa huduma za hali ya hewa katika sekta ya usafiri wa anga (QMS, ISO 9001:2015 ). 

Dkt. Kijazi alizungumza hayo katika mkutano wa Kamati hiyo uliofanyika tarehe 20 na 21 Agosti 2020 kwa njia ya mtandao alipokuwa akitoa taarifa fupi ya utekelezaji wa shughuli za sekta ya hali ya hewa katika kipindi cha Uenyekiti wake katika sekta hiyo kuanzia Agosti 2019 hadi Agosti 2020.

”Mpaka hivi sasa ni nchi saba (7) tu kati ya kumi na sita (16) za SADC ambazo zimepata cheti cha ubora wa kimataifa katika utoaji wa huduma za hali ya hewa kwenye sekta ya usafiri wa anga. Nchi hizo ni pamoja na Tanzania, Afrika ya Kusini, Angola, Botswana, Mauritius, Msumbiji na Zimbabwe. Kwa kuwa hili ni moja ya malengo tuliyojiwekea na yanayoendana na matakwa ya utoaji wa huduma za hali ya hewa Kimataifa, ni vyema tuweke msisitizo zaidi kuhakikisha kuwa nchi zote za SADC zinafikia lengo hili”. Alisema Dkt. Kijazi

Aidha, Dkt. Kijazi alielezea mafanikio yaliyopatikana kwa kipindi cha mwaka mmoja wakati Tanzania ikiwa Mwenyekiti wa SADC licha ya changamoto za ugonjwa wa COVID-19, ikiwa ni pamoja na: 

  • Utekelezaji wa miradi mbalimbali itakayochangia kuboresha huduma za hali ya hewa hususani uboreshaji wa miundombinu. Miradi hii ni pamoja na mradi wa kikanda wa ”Southern African Regional Climate Information Service for Disaster Resilience Development (SARCIS-DR)” ambao umefanikisha upatikanaji wa vituo vinavyojiendesha vyenyewe ”Automatic Weather Stations-(AWS)" na Kompyuta mahsusi za uchakataji wa taarifa za hali ya hewa ”High Perfoming Computers (HPC)” ambazo zitasaidia katika juhudi za nchi wanachama kukabiliana na majanga ya hali mbaya ya hewa.
  • Wataalamu wa hali ya hewa walipata mafunzo mbalimbali kupitia warsha zilizoandaliwa na Sekretariati ya SADC. Mfano ni warsha ya mafunzo ya kujenga uwezo wa wataalamu wa hali ya hewa ili waweze kutoa utabiri bora zaidi wa msimu yaliyoendeshwa sambamba na kongamano la 23 la nchi za SADC la utoaji wa utabiri wa hali ya hewa wa msimu linalojulikana kama “Southern Africa Climate Outlook Forum (SARCOF)”. Mafunzo haya yalifanyika kuanzia tarehe 19 hadi 27 Agosti 2020, Luanda, Angola. Utabiri huo wa hali ya hewa wa msimu-kikanda husaidia kila nchi mwanachama kuandaa utabiri wa hali ya hewa wa msimu katika eneo la nchi zao.
  • Kuendelea kufanyika kwa mikutano muhimu iliyochangia katika maamuzi ya uendelezaji wa sekta ya hali ya hewa kwa nchi wanachama wa SADC kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Mikutano hiyo ni pamoja na Mkutano wa Mawaziri wa Sekta za Uchukuzi, TEHAMA, na Hali ya Hewa, Mkutano wa Mawaziri wanaoratibu Maafa na Mikutano ya Wakuu wa Taasisi za hali ya hewa za SADC.

Mkutano huo wa SCOM ulihudhuriwa na Wakuu wa Taasisi za Hali ya Hewa za Nchi Wanachama wa SADC, Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) na Umoja wa Taasisi za Hali ya Hewa za Kusini mwa Afrika (Meteorological Association of Southern Africa (MASA).


Thursday, August 13, 2020

HALI YA BAHARI KUFUATIA TETEMEKO LA ARDHI CHINI YA BAHARI YA HINDI.

 

Dar es Salaam, 12 Agosti 2020:

 Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inatoa taarifa kuhusu hali ya bahari

kufuatia tetemeko la ardhi chini ya bahari ya Hindi. Leo tarehe 12/08/2020 majira ya saa mbili (2) usiku, tumepokea taarifa zilizothibitishwa na “Geological Survey of Tanzania” (GST) kuhusu tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa kipimo cha 5.9 katika eneo la kusini mashariki mwa Mkoa wa Pwani katika bahari ya Hindi.

 Kutokana na Tetemeko hilo kutokea katika eneo la chini ya bahari, Mamlaka ya Hali yaHewa Tanzania imefanya uchambuzi wa taarifa za tetemeko hilo katika kituo chake cha Tahadhari ya Tsunami ili kuona iwapo kuna uwezekano wowote wa tetemeko hilo kusababisha mawimbi ya Tsunami baharini. Matokeo ya uchambuzi huo yanaonesha kuwa hakuna tishio la Tsunami kutokana na tetemeko hilo. Tetemeko hilo halikuwa nguvu kubwa na hakuna maporomoko ya ardhi yaliyojitokeza baharini ambayo yangeweza kuzalisha tsunami.

 TMA inaendelea kufuatilia mifumo ya hali ya hewa baharini na kutoa taarifa endapo kutajitokeza mwendelezo wa matetemeko katika eneo la Bahari.

 ATHARI: Hakuna adhari zilizojitokeza au zinazotarajiwa katika mifumo ya hali ya hewa ya bahari kutokana na tetemeko hilo.

 USHAURI: Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania inawashauri watumiaji wa eneo la bahari ikiwa ni pamoja wananchi wanaoishi katika maeneo yaliyokaribu na bahari ya Hindi kutokuwa na hofu na kuendelea na shughuli kwa kuzingatia taarifa ya hali ya hewa Baharini kama ilivyotolewa awali na Mamlaka.

Sunday, August 9, 2020

NAIBU KATIBU MKUU WA WIZARA YA KILIMO, MALIASILI, MIFUGO NA UVUVI – ZANZIBAR, BI. MANSURA KASSIM ASISITIZA KUIMARISHA USHIRIKIANO BAINA YA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA(TMA) NA WIZARA YA KILIMO, MALIASILI, MIFUGO NA UVUVI – ZANZIBAR.

 

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi - Zanzibar, Bi. Mansura Kassim akisisitiza jambo kwa Mkurugenzi wa TMA - Zanzibar, Ndg. Mohamed Ngwali mara baada ya kupata elimu ya Sayansi ya hali ya hewa alipotembelea banda la TMA katika maonesho ya NaneNane 2020, Zanzibar

Mkurugenzi wa TMA - Zanzibar, Ndg. Mohamed Ngwali akifafanua jambo kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi - Zanzibar, aliyetembelea banda la TMA katika maonesho ya NaneNane 2020, Zanzibar.













Matukio mbalimbali katika picha wakati wageni kutoka katika sekta mbalimbali wakipata elimu ya sayansi ya hali ya hewa, walipotembelea banda la TMA katika maonesho ya NaneNane 2020, Zanzibar.






Baadhi ya wageni kutoka katika sekta mbalimbali wakipokea zawadi mbalimbali kutoka TMA, walipotembelea banda lake lililopo katika maonesho ya NaneNane 2020, Zanzibar.
 
 
ZANZIBAR, TAREHE 08/08/202

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi - Zanzibar, Bi. Mansura Kassim asisitiza TMA na Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi - Zanzibar kuimarisha zaidi  ushirikiano wa kiutendaji , aliyasema hayo alipotembelea banda la TMA  lililopo katika maonesho ya NaneNane, yanayofanyika katika viwanja vya Dole, Kizimbani – Unguja, kuanzia  tarehe 04 – 08 Agosti, 2020.

“Kutokana na TMA kuwa mdau muhimu wa Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi - Zanzibar ni vyema kufanya kazi kwa karibu, japo najua hivi sasa tunashirikiana lakini hapa ninamaanisha kuimarisha  zaidi ushirikiano wetu huku mkitambua kuwa taarifa za hali ya hewa  kama vile hali ya unyevu, mvua, joto na uangazi wa jua zinahitajika sana katika kuendesha mifumo ya kiutendaji (simulation Model) ambayo husaidia kutoa utabiri wa makadirio ya uzalishaji wa mazao.” Alielezea Bi. Mansura Kassim.

Bi. Mansura Kassim aliishauri TMA kutafuta njia ya kuhakikisha taarifa za hali ya hewa zilizo sahihi zinawafikia wadau kama wakulima na wafugaji kwa wakati ili kupanga mipango yao mapema. Alitolea mfano kuwa wakulima kama wakipata utabiri wa hali ya hewa mapema wanaweza kupanga muda mzuri wa kupiga dawa za kuangamiza wadudu hatarishi kwa mimea bila kuathiriwa na uwepo wa mvua.

Aidha, Mkurugenzi wa TMA - Zanzibar Ndg. Mohamed Ngwali alitolea ufafanuzi moja ya mapendekezo ya Bi. Mansura Kassim juu ya utekelezaji wa majukukumu ya TMA ikiwemo njia zitakazotumika katika usambazaji wa taarifa za hali ya hewa ili kuwafikia watumiaji kwa wakati kwa mujibu wa sheria mpya ya Mamlaka, namba 2 ya mwaka 2019. Kupitia maonesho hayo wageni mbalimbali wameendelea kumiminika katika banda la TMA na kupatiwa elimu ya sayansi ya hali ya hewa.

Friday, August 7, 2020

HERI YA SIKUKUU YA WAKULIMA NANENANE 2020

 

KATIBU MKUU WA WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO ( SEKTA YA UCHUKUZI) MHANDISI. LEONARD CHAMRIHO ATEMBELEA BANDA LA TMA NANENANE 2020, SIMIYU.

 
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano( Sekta ya Uchukuzi) Mhandisi. Leonard Chamriho akikaribishwa na watumishi wa TMA alipotembelea banda la TMA katika maonesho ya NaneNane 2020, Simiyu.



Mkurugenzi wa Utafiti na Matumizi Dkt. Ladislaus Chang'a akifafanua jambo kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano( Sekta ya Uchukuzi) Mhandisi. Leonard Chamriho akitembelea banda la TMA katika maonesho ya NaneNane 2020, Simiyu.
 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano( Sekta ya Uchukuzi) Mhandisi. Leonard Chamriho akipokea zawadi kutoka TMA wakati alipotembelea banda la TMA katika maonesho ya NaneNane 2020, Simiyu.

NANENANE 2020,MOROGORO

 

Mkurugenzi Mkuu TMA, Dkt. Agnes Kijazi akitoa elimu kwa wanafunzi katika banda la maonyesho ya Nanenane 2020 Mkoa wa Morogoro.

Thursday, August 6, 2020

NANENANE 2020: WANANCHI WAMIMINIKA TMA NYAKABINDI.





 

Simiyu; Tarehe 04/08/2020

Wananchi mbalimbali katika mkoa wa Simiyu wametembelea banda la Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ili kupata elimu ya hali ya hewa inayotolewa na wataalam kutoka Mamlaka. Akizungumza wakati na wananchi hao kwa nyakati tofauti tofauti, Mkurugenzi wa Utafiti na Matumizi wa TMA, Dkt. Ladislaus Chang’a, alisema TMA ni taasisi yenye mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi hususan katika sekta zote za kiuchumi na kijamii.

“Basi mwananchi tunakuomba utumie taarifa zetu za hali ya hewa ili kuongeza tija na ufanisi katika shughuli zetu za kimaendeleo, na katika azma nzima ya kuifanya nchi yetu kuwa nchi ya viwanda”. Alisema Dkt. Chang’a.

Aidha, aliendelea kusisitiza kuwa matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa ni chachu kwa maendeleo endelevu ya kilimo, mifugo na uvuvi, huku akisisitiza wananchi kuchagua vingozi bora kwa maendeleo ya nchi yetu ambayo tayari imefikia uchumi wa kati.

Kwa upande wa Meneja wa Kanda ya Ziwa-TMA, Ndg. Augustine Nduganda aliwakaribisha wananchi wa Kanda ya Ziwa hususan Mashariki, kutembelea banda la TMA ili waweze kupata elimu ya sayansi ya hali ya hewa kwa ujumla ikiwa ni pamoja na kujionea vifaa vya hali ya hewa, jinsi uangazi, uchambuzi na utayarishaji wa taarifa za hali ya hewa ikiwemo utabiri unavyofanyika na pia kupata elimu kuhusus mabadiliko ya hali ya hewa.

WANANCHI WA ZANZIBAR WAFURAHISHWA NA NAMNA ELIMU YA HALI YA HEWA INAVYOTOLEWA KATIKA MAONESHO YA NANENANE 2020.












Matukio mbalimbali kwa picha wakati wageni wakiendelea kupata elimu ya sayansi ya hali ya hewa kutoka kwa wataalam wa hali ya hewa kwenye banda la TMA lililopo katika maonesho ya Nanenane yanayofanyika viwanja vya Dole, Kizambani - Unguja, kuanzia Tarehe 04 - 08 Agosti 2020.

Zanzibar; Tarehe 05/08/2020

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), inashiriki katika maonesho ya Nanenane yanayofanyika katika viwanja vya Dole, Kizimbani - Unguja, kuanzia Tarehe 04-08 Agosti, 2020, yenye kauli mbiu ya " tudumishe amani na utulivu kwa maendeleo endelevu ya Taifa letu la Tanzania."

Wageni mbalimbali waliotembelea banda la TMA wameonesha kufurahishwa na namna elimu ya hali ya hewa inavyotolewa bandani hapo na wengi wao wamesisitiza TMA kuendelea kubuni njia nyingine zaidi za kufikisha elimu hiyo kwa wananchi wa visiwani hapo.

Aidha, wataalam wa hali ya hewa toka TMA wameendelea kutoa elimu kwa wananchi kutoka sekta mbalimbali ikiwemo kilimo, uvuvi, usafiri wa anga na maji n.k ili kuelewa namna ya kutumia taarifa za hali  ya hewa kwa usahihi na kuongeza uzalishaji wa malighafi kupitia sekta zao na kujiepusha na majanga yatokanayo na hali mbaya ya hewa sambamba na kutambua njia zitumikazo na Mamlaka katika kusambaza taarifa za hali ya hewa kwa wananchi ikiwemo mitandao ya kijamii.

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...