Sunday, September 1, 2019

WADAU MBALIMBALI WATAKIWA KUCHOCHEA MATUMIZI YA TAARIFA ZA HALI YA HEWA KATIKA UCHUMI WA VIWANDA.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) akiongea wakati akifungua warsha ya wadau kujadili utabiri wa msimu wa mvua za vuli (Oktoba - Disemba 2019) unaotarajiwa kutolewa rasmi tarehe 03 Septemba 2019 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza, Dar es Salaam, Tanzania.
Rais wa TMS Dkt. Burhani Nyenzi (kushoto) akizungumza kabla ya ufunguzi wa warsha ya wadau kujadili utabiri wa msimu wa mvua za vuli (Oktoba - Disemba 2019) unaotarajiwa kutolewa rasmi tarehe 03 Septemba 2019 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza, Dar es Salaam, Tanzania.
Kaimu Mkurugenzi wa Huduma Saidizi Bi. Mariam Is-haaq akimkaribisha Mgeni rasmi kwa ajili ya ufunguzi wa warsha ya wadau kujadili utabiri wa msimu wa mvua za vuli (Oktoba - Desemba 2019) unaotarajiwa kutolewa rasmi tarehe 03 Septemba 2019 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.
Bw. Wilberforce Kikwasi akichangia mada kwenye warsha ya wadau kujadili utabiri wa msimu wa mvua za vuli (Oktoba - Desemba 2019) unaotarajiwa kutolewa rasmi tarehe 03 Septemba 2019 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.
Bw. Aloyce Swenya akiwasilisha mada kwenye warsha ya wadau kujadili utabiri wa msimu wa mvua za vuli (Oktoba - Desemba 2019) unaotarajiwa kutolewa rasmi tarehe 03 Septemba 2019 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.
Bi. Sabiha Mukubwa akiwasilisha mada kwenye warsha ya wadau kujadili utabiri wa msimu wa mvua za vuli (Oktoba - Desemba 2019) unaotarajiwa kutolewa rasmi tarehe 03 Septemba 2019 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.

Wadau mbalimbali wakichangia mada katika warsha ya wadau kujadili utabiri wa msimu wa mvua za vuli (Oktoba - Desemba 2019) unaotarajiwa kutolewa rasmi tarehe 03 Septemba 2019 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.

Wadau kutoka sekta mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi kwenye warsha ya wadau kujadili utabiri wa msimu wa mvua za vuli (Oktoba - Desemba 2019) unaotarajiwa kutolewa rasmi tarehe 03 Septemba 2019 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.


Tarehe 29/08/2019: Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kupitia programu ya Huduma za Hali ya Hewa ya kidunia (Global Framework for Climate Services (GFCS)) iliyo chini ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), imekutana na wadau wa sekta mbalimbali ili kujadili na kupata maoni yao jinsi watakavyoutumia utabiri wa msimu wa mvua za vuli (Oktoba hadi Disemba, 2019) unaotarajiwa kutolewa rasmi tarehe 03 Septemba 2019.

Akiongea wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo, mgeni rasmi ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa WMO, Dkt. Agnes Kijazi aliwakumbusha washiriki kutambua mabadiliko ya hali ya hewa ni changamoto kubwa katika sekta mbalimbali hivi sasa, hivyo aliwataka washiriki kufanya juhudi za pamoja ili kuhakikisha taarifa za hali ya hewa zinatumika ipasavyo na kuleta maendeleo endelevu hasa kuchochea uchumi wa viwanda katika Taifa letu kwa kuzalisha malighafi zitakazohitajika viwandani.

“Ni matumaini yangu baada ya kikao hiki TMA kwa kushirikiana na ninyi wadau kutoka katika sekta mbalimbali tutahakikisha watanzania wanapata taarifa za hali ya hewa kwa wakati na wanazitumia ipasavyo katika sekta mbali mbali ili kuleta maendeleo endelevu hasa kuchochea uchumi wa viwanda katika Taifa letu kwa kuzalisha malighafi zitakazohitajika viwandani ikiwemo mali ghafi kutoka sekta ya kilimo”, alifafanua Dkt. Kijazi

Aidha Dkt.Kijazi  alisisitiza wadau kupanga mipango ya sekta zao kulingana na utabiri wa hali ya hewa utakaotolewa hapo baadae wenye kujumuisha maoni yao, ikiwa ni moja ya utekelezaji wa maelekezo kutoka Shirika la hali ya hewa Duniani la kutaka taasisi za hali ya hewa kuwahusisha zaidi wadau ambao ndiyo watumiaji wa taarifa za hali ya hewa.

Washiriki wa mkutano huo ulijumuisha sekta ya afya, nishati, maafa, wanahabari, kilimo, uchukuzi, uvuvi, mifugo, NGO, na wataalamu wa lugha (BAKITA).

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...