Tuesday, September 3, 2019

TMA YATOA MWELEKEO WA MSIMU WA MVUA ZA VULI KWA KIPINDI CHA MWEZI OKTOBA HADI DESEMBA 2019

Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania(TMA) na Makamu wa tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) Dkt. Agnes Kijazi, mbele ya waandishi wa habari  akichambua  mwenendo wa mifumo ya hali ya hewa na mwelekeo wa mvua za Msimu wa Vuli Oktoba - Desemba 2019
Bi. Veronica Mgalula akitoa tathmini ya mvua za msimu wa Masika 2019, kabla ya kutolewa rasmi mwelekeo wa msimu wa mvua za vuli kwa kipindi cha mwezi Oktoba hadi Desemba 2019.


Washiriki mbalimbali wakiwa kwenye mkutano wa wanahabari wa kutoa mwelekeo wa mvua za Msimu wa Vuli Oktoba - Desemba 2019.


Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa rasmi utabiri wa msimu kuanzia mwezi Oktoba 2019 hadi Desemba, 2019 katika mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika katika Ofisi za TMA. 

Taarifa inatoa uchambuzi wa mwenendo wa mifumo ya hali ya hewa na mwelekeo wa msimu wa mvua katika kipindi cha mwezi Oktoba hadi Desemba, 2019. Pia ushauri na tahadhari kwa wadau wa sekta mbali mbali wanaohitaji taarifa za hali ya hewa katika utekelezaji wa majukumu yao kama vile Kilimo na Usalama wa Chakula, Mifugo na Wanyamapori, Maliasili na Utalii, Uchukuzi na Mawasiliano, Nishati na Maji, Mamlaka za Miji, Afya pamoja na Menejimenti za Maafa. Muhtasari wa mwelekeo wa mvua hizo na athari zake ni kama ifuatavyo: Kusoma zaidi ingia humu http://meteo.go.tz/news/226

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...