Tuesday, September 17, 2019

DKT. KIJAZI: MKUTANO WA MAWAZIRI WA SADC WA SEKTA YA TEHAMA, HABARI, UCHUKUZI NA HALI YA HEWA NI FURSA KWA HUDUMA ZA HALI YA HEWA NCHINI

Waziri wa Ujenzi, uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe akisalimiana na wataalamu wa TMA alipotembelea banda la TMA kwenye mkutano wa mawaziri wa SADC wa sekta ya tehama, habari, uchukuzi na hali ya hewa unaofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere, Dar es Salaam.


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dkt. Agnes Kijazi akizungumza na TBC1 katika banda la TMA kwenye mkutano wa mawaziri wa SADC wa sekta ya tehama, habari, uchukuzi na hali ya hewa unaofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere, Dar es Salaam.





Wageni mbalimbali wakipata elimu kutoka kwa wataalamu katika banda la TMA kwenye mkutano wa mawaziri wa SADC wa sekta ya tehama, habari, uchukuzi na hali ya hewa unaofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere, Dar es Salaam.



Tarehe 16/09/2019:‘Mkutano huu ni fursa kwa huduma za hali ya hewa nchini kwa vile utajadili masuala mbalimbali yenye lengo la uboreshaji, hivyo Tanzania itatumia fursa hiyo kuongeza ufanisi’, Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Kijazi, alizungumza hayo wakati wa mkutano wa mawaziri wa SADC wa sekta ya tehama, habari, uchukuzi na hali ya hewa, ulioanza nchini, katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere, Dar es Salaam.

Aliongezea kwa kusema kuwa Tanzania kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imekuwa ikifanya vizuri katika ukanda wa nchi za SADC ikiwa ni pamoja na kusaidia nchi zingine wanachama wa SADC katika kuboresha huduma za hali ya hewa kama vile kuanzisha mifumo ya kiutendaji bado TMA inajikita katika kuongeza fursa za ajira na kuweka mazingira wezeshi katika ukuaji wa uchumi wa nchi na jumuiya kupitia huduma za hali ya hewa.

Aidha katika kuhakikisha TMA inashiriki kikamilifu mkutano huo, TMA imeweka banda maalumu kwaajili ya kuelimisha huduma inazozitoa na mifumo iliyopo sambamba na utabiri mahsusi kwa washiriki wa mkutano.

Mkutano huo umeanza rasmi leo tarehe 16 mpaka 20 Septemba 2019 ukijumuisha mawaziri na wataalamu mbalimbali wa sekta husika kutoka nchi za SADC. Kauli mbiu ya mkutano huo ni ‘Mazingira Wezeshi kwa Ukuaji wa Uchumi Jumuishi na Endelevu, Kukuza Biashara katik Jumuiya na Kuongeza Fursa ya Ajira’

1 comment:

  1. HONGERENI SANA TMA KWA KAZI NZURI. MUNGU IBARIKI TMA, MUNGU IBARIKI TANZANIA.

    ReplyDelete

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...