Monday, September 9, 2019

DKT. KIJAZI ASISITIZA UMUHIMU WA MICHEZO KWA WAFANYAKAZI.

Matukio mbalimbali kwa picha katika kikao cha TUGHE kilichofanyika tarehe 07Septemba 2019 katika ukumbi wa TMA, Ubungo Plaza - Dar es salaam 

” Natambua umuhimu wa michezo kwa wafanyakazi kwani inaleta umoja kazini (team work) pamoja na kuleta afya, hivyo kuifanya Mamlaka kuwa juu” aliyasema hayo Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) Dkt. Agnes Kijazi wakati akitoa nasaha zake katika kikao cha TUGHE kilichofanyikia tarehe 07 Septemba 2019 katika ukumbi wa TMA, Ubungo plaza - Dar es salaam.

Katika kikao hicho Dkt. Kijazi alipokea zawadi mbalimbali toka kwa wanachama wa TUGHE kwa kushika nafasi ya umakamu wa tatu wa Rais wa WMO kwa kipindi cha miaka minne kuanzia 2019 hadi 2022.

Aidha, Katibu wa TUGHE Kinondoni, Ndg. Litson Magawa alimpongeza Dkt. Kijazi kwa kufanikisha TMA kuwa Mamlaka Kamili pamoja na kushika nafasi ya umakamu wa tatu wa Rais wa WMO.

Naye Kaimu Katibu wa Uchukuzi Sports Club, Ndg. Joseph Peter aliipongeza menejimenti ya TMA kwa kuwawezesha wachezaji wake kufika kwenye mashindano kwa wakati na hatimaye kufanikisha kuchukua vikombe vya ushindi mara kadhaa. 

Awali, Kaimu Mwenyekiti wa TUGHE mkoa wa Dar es salaam, Dkt. Peter Kibacha aliwasilisha mada iliyolenga kuokoa na kupunguza vifo kwa wamama wajawazito ambaye baadae aliwakumbusha viongozi kufuatilia utekelezaji wa mkataba wa hali bora kwa wafanyakazi.  

Aidha washiriki wengine katika kikao hicho ni pamoja na viongozi wa menejimenti ya TMA, viongozi wa Tughe ndani ya Mamlaka pamoja na wanachama wengine wa Tughe.


2 comments:

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...