Thursday, September 5, 2019

MAMLAKA YA HALI YA HEWA YAZINDULIWA RASMI

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Isack Kamwele akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kutoka kuwa Wakala (Agency) katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) Dkt. Agnes Kijazi akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kutoka kuwa Wakala (Agency) katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam

Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Dkt. Leonard Chamuriho akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kutoka kuwa Wakala (Agency) katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam

Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar Ndugu, Mustafa Aboud Jumbe akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kutoka kuwa Wakala (Agency) katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam


Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania iliyomaliza muda wake Dkt. Buruhani Nyenzi  akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kutoka kuwa Wakala (Agency) katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam

Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Miundombinu ndugu Zuberi Mohamed Kuchauka akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kutoka kuwa Wakala (Agency) katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam

Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania iliyomaliza muda wake, katika picha ya pamoja na mgeni rasmi wakati wa uzinduzi rasmi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kutoka kuwa Wakala (Agency) katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam

Wawakilishi wa Wizara mbalimbali za Serikali katika picha ya pamoja na mgeni rasmi wakati wa uzinduzi rasmi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kutoka kuwa Wakala (Agency) katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam

Viongozi wastaafu wa TMA katika picha ya pamoja na Mgeni rasmi wakati wa uzinduzi rasmi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kutoka kuwa Wakala (Agency) katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam


Wadau wa Maendeleo katika picha ya pamoja na mgeni rasmi wakati wa uzinduzi rasmi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kutoka kuwa Wakala (Agency) katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam

Kamati ya hafla ya uzinduzi katika picha ya pamoja na mgeni rasmi wakati wa uzinduzi rasmi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kutoka kuwa Wakala (Agency) katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam


Baadhi ya Wafanyakazi wa Makao Makuu - TMA katika picha ya pamoja na mgeni rasmi wakati wa uzinduzi rasmi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kutoka kuwa Wakala (Agency) katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam

Baadhi ya Wafanyakazi wa Kituo Kikuu cha Utabiri na Kituo cha Kibaha - TMA katika picha ya pamoja na mgeni rasmi wakati wa uzinduzi rasmi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kutoka kuwa Wakala (Agency) katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam


Baadhi ya wafanyakazi wa kituo cha JNIA na Bandarini - TMA katika picha ya pamoja na mgeni rasmi wakati wa uzinduzi rasmi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kutoka kuwa Wakala (Agency) katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam


Tarehe 05/09/2019: Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Isack Kamwele amezindua rasmi Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kutoka kuwa Wakala (Agency) katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam.
Uzinduzi wa Mamlaka umetokana na sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa “Tanzania Meteorological Authority Act No.2 of 2019” iliyopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kusainiwa tarehe 13 Februari, 2019 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, awali Wakala huo ulianzishwa baada ya iliyokuwa Idara Kuu ya Hali ya Hewa kubadilishwa na kuwa Wakala wa Serikali mnamo mwaka 1999 kwa Sheria yaw akala wa Serikali sura 245 marejeo ya 2002.
 Idara Kuu ya Hali ya Hewa (Directorate of Meteorology) ambayo ilianzishwa mwaka 1977 baada ya kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, ilikuwa na jukumu la kuangaza na kutoa taarifa za hali ya hewa nchini. Kabla ya hapo huduma hizo zilikuwa zikitolewa na Idara ya Hali ya Hewa ya Afrika Mashariki (EAMD). 
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mhe. Kamwelwe aliwajulisha washiriki kwamba ndege yetu iliyokuwa inashikiliwa Afrika Kusini imekwishawasili nchini baada ya Serikali kushinda kesi. Mheshimiwa Kamwelwe alimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi kwa kuchaguliwa kuwa Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani.
Aidha, alimpongeza Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TMA, Dkt. Buruhani Nyenzi kwa usimamizi mzuri wa Mamlaka. Akizungumzia uzinduzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania Mheshimiwa Kamwelwe alisema  Wakala wa Hali ya Hewa Tanzania ‘Tanzania Meteorological Agency’ imepandishwa hadhi na kuwa Mamlaka, hivyo kuweza kukidhi pande zote mbili za Tanzania Bara na Visiwani 
Wakati akitoa neno la ukaribisho, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Leonard Chamuriho alisema huduma za hali ya hewa ni mtambuka zinahitajika katika sekta zote ikiwemo ya viwanda, kwa hiyo wageni wote waalikwa wako katika uzinduzi huo kutokana na umuhimu wa huduma hizo za hali ya hewa
Aidha, wakati akiwasilisha taarifa ya uzinduzi TMA na mifumo mbalimbali ya kiutendaji, Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi alielezea kuwa Mamlaka imeongezewa jukumu la kudhibiti na kuratibu utoaji na utumiaji wa huduma za hali ya hewa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na alikabidhi hati kutoka Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) za kutambua rasmi vituo vya Songea na Bukoba kuwa na takwimu za muda mrefu za zaidi ya miaka 100.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Ndugu. Mustafa A. Jumbe aliwasisitiza kuwa hali ya hewa haina mipaka na kudhihirisha jinsi Tanzania Visiwani wanavyozingatia tahadhari zinazotolewa na TMA kwa usafiri wa baharini. 
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TMA, Dkt. Buruhani Nyenzi alielezea mafanikio ya uongozi wa Bodi anayoiongoza ikiwa ni kupatikana kwa sheria iliyopelekea kuzindua Mamlaka hiyo.
Uzinduzi huo ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, wakurugenzi wa taasisi, wawakilishi wa sekta binafsi, asasi za kiraia, mashirika ya kimaendeleo, wanahabari na wafanyakazi wa TMA. Ulienda sambamba na uzinduzi wa nembo mpya, tovuti mpya na mifumo ya “TMA Digital Meteorological Observatory (TMA-DMO)” kwa ajili ya kurahisisha mawasiliano ya Data za Hali ya Hewa; “Meteorological Aviation Information System (MAIS)” kwaajili ya kurahisisha utoaji wa huduma za hali ya hewa katika usafiri wa anga na “ Marine Meteorological Information System (MMIS)” unaosaidia sana katika utoaji wa huduma za hali ya hewa kwa sekta ya kwenye maji yaani bahari, maziwa na mito

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...