Monday, August 28, 2023

MRADI WA UJENZI WA OFISI YA TMA, KANDA YA MASHARIKI NA KITUO CHA KUTOA TAHADHARI ZA TSUNAMI NCHINI WAKAGULIWA



Dar es Salaam;Tarehe 28 Agosti, 2022;

Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dkt. Buruhani Nyenzi amekagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Ofisi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, Kanda ya Mashariki na Kituo cha kutoa tahadhari za TSUNAMI nchini, unaotekelezwa katika maeneo ya SIMU 2000, Jijini Dar es Salaam. 

Mradi huo ambao utagharimu zaidi ya shilingi Bilioni 9 za kitanzania, unatarajiwa kukamilika mwezi Julai,2024. Akizungumza wakati wa ziara yake, Dkt. Nyenzi alisema, chini ya Serikali ya Awamu wa Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, Mamlaka imekuwa wanufaika wakubwa katika uboreshaji wa huduma za hali ya hewa nchini ukiwemo mradi huo ambao utahusika moja kwa moja katika utoaji wa tahadhari za TSUNAMI nchini na hivyo kuongeza tija katika mipango ya nchi. 

Aidha, Dkt. Nyenzi alifurahishwa na kasi ya ujenzi unavyoendelea kutokana na hatua mbalimbali ambazo mkandarasi amezichukua ikiwa ni pamoja na kufanya kazi muda wa ziada na kuongeza nguvu kazi ili kuhakikisha makubaliano ya kimkataba yaliyowekwa yanafikiwa kwa wakati. Dkt. Nyenzi alisisitiza matumizi ya malighafi zenye ubora na kutoa fursa za ajira kwa wazawa katika mradi huo.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...