Wednesday, April 21, 2021

KIMBUNGA JOBO KATIKA BAHARI YA HINDI KASKAZINI MWA MADAGASCAR



Dar es Salaam, 21 Aprili 2021:

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inatoa taarifa kuhusu kimbunga Jobo
kaskazini mwa kisiwa cha Madagascar.
Kumejitokeza mgandamizo mdogo wa hewa ambao umefikia kiwango cha kimbunga 
hafifu kwa jina Jobo. Kimbunga hicho kipo kaskazini mwa Kisiwa cha Madagascar
katika Bahari ya Hindi umbali wa Kilometa 930 na kilometa 1030 kutoka pwani ya Lindi 
na Mtwara. Aidha, uwepo wa kimbunga hicho unatarajiwa kusababisha ongezeko la 
upepo na mawimbi katika bahari ya Hindi hususan katika Pwani ya mwambao wa mikoa ya Mtwara na Lindi. 

Mamlaka inaendelea kufuatiliia mwenendo na mwelekeo wa kimbunga Jobo kwa 
kuzingatia mifumo mingine ya hali ya hewa iliyo jirani zaidi na kimbunga hicho ambayo 
inaweza kubadili nguvu na mwelekeo wa kimbunga Jobo katika wakati ujao.
Wananchi waendelee kuzingatia tahadhari ya upepo na mawimbi iliyotolewa na 
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania katika maeneo husika. Mamlaka ya Hali ya Hewa 
itaendelea kutoa taarifa kila inapobidi. 

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...