Friday, February 11, 2022

TMA KUENDELEA KUTOA HUDUMA MAHSUSI ZA HALI YA HEWA KWA FAIDA ZA KIUCHUMI.


Wadau kutoka sekta mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi katika mkutano wa wadau, kujadili Utabiri wa Mvua za Msimu wa Masika (Machi hadi Mei, 2022) , katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 17 Februari 2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.


Mgeni rasmi, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Mkurugenzi wa Matumizi na Utafiti Dkt. Ladislaus Chang'a akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi wakati akifungua rasmi Mkutano wa Wadau wa Utabiri wa Mvua za Masika (Machi hadi Mei, 2022) , katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 17 Februari 2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.



Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri wa TMA, Dkt. Hamza Kabelwa  akiongea kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Dkt. Ladislaus Chang'a kufungua Mkutano wa Wadau wa Utabiri wa Mvua za Masika (Machi hadi Mei, 2022) , katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 17 Februari 2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.


Mtaalam wa Hali ya hewa kutoka TMA, Bi. Rose Senyagwa akiwasilisha mada katika Mkutano wa Wadau wa Utabiri wa Mvua za Masika (Machi hadi Mei, 2022) , katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 17 Februari 2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.

Mtaalam wa Hali ya hewa kutoka TMA, Bw. Ramadhani Omary akiwasilisha mada katika  Mkutano wa Wadau wa Utabiri wa Mvua za Masika (Machi hadi Mei, 2022) , katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 17 Februari 2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.









Wadau kutoka sekta mbalimbali wakiwasilisha mada katika  Mkutano wa Wadau wa Utabiri wa Mvua za Masika (Machi hadi Mei, 2022) , katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 17 Februari 2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.





Wadau kutoka sekta ya mbalimbali wakichangia mada katika  Mkutano wa Wadau wa Utabiri wa Mvua za Masika (Machi hadi Mei, 2022), katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 17 Februari 2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.










Wataalam bingwa wa hali ya hewa pamoja na wadau kutoka sekta mbalimbali wakiwa katika makundi wakijadili athari na ushauri kwa msimu wa mvua za Masika 2022 kupitia  Mkutano wa Wadau wa Utabiri wa Mvua za Masika (Machi hadi Mei, 2022), katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 17 Februari 2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.





Matukio kwa picha wakati wadau wakisikiliza mada mbalimbali zilizowasilishwa katika Mkutano wa Wadau wa Utabiri wa Mvua za Masika (Machi hadi Mei, 2022), katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 17 Februari 2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.



Dar es Salaam; Tarehe 11 Februari, 2022;

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imesema itaendelea kuimarisha utoaji wa  huduma mahususi za hali ya hewa ili kuongeza tija na ufanisi katika shughuli za kijamii na kiuchumi. Hayo yalizungumzwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Mkurugenzi wa Matumizi na Utafiti Dkt. Ladislaus Chang’a wakati akifungua rasmi Mkutano wa Wadau wa Utabiri wa Mvua za Masika 2022 kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi katika Ukumbi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT), Dar es Salaam, Tarehe 11/02/2022.

“Matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa na hasa katika kipindi ambapo dunia inakabiliwa na changamoto ya mabadiliko ya hali ya hewa na Tabianchi ni muhimu sana na  yatasaidia kufikiwa kwa malengo ya  mpango wa Taifa wa kujenga uchumi wa viwanda nchini na mikakati mingine ya kuleta maendeleo katika jamii na Taifa. TMA itaendelea kuimairisha utoaji wa  huduma mahsusi za hali ya hali ya hewa ili kuhakikisha malengo yanafikiwa”. Alisema Dkt. Chang’a.

Aidha, katika mkutano huo TMA ilitoa tathimini ya usahihi wa utabiri wa Msimu wa mvua za vuli 2021 zilizoisha mwezi Desemba 2021, ambapo tathmini hiyo ilionesha kuwa utabiri ulikuwa sahihi kwa asilimia 93.8, hivyo mamlaka inaendelea kuweka msisitizo wa matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa kwa kila sekta ili kuongeza tija na uzalishaji.

Kwa upande wa mdau kutoka Wizara ya Kilimo, Bw. Juma Makandi alisema mara baada ya kupata taarifa za utabiri wa msimu wa mvua za Vuli, Wizara iliaandaa na kutoa  tafsiri ya utabiri huo katika shughuli za kilimo kwa mawaziri pamoja na wakuu wa mikoa kwa ajili ya kuwawezesha kuweka mipango stahiki ya kukabiliana na athari za utabiri huo..

Naye, mdau wa Kilimo kutoka Zanzibar Bw. Nasoro Mkarafuu alieleza kuwa utabiri ulikuwa kama ulivyotabiriwa hivyo mipango iliyowekwa ya kushirikisha maafisa ugani ilienda kama ilivyopangwa.

Mdau kutoka ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Maafa alisema baada ya kupokea utabiri huo, idara iliandaa kikao kazi cha kujadili mpango wa dharura wa ukame unaoweza kujitokeza kutokana na utabiri uliotolewa sambamba na kuandaa vipindi vya elimu kwa umma kupitia vyombo mbalimbali va habari.

Katika Mkutano huo, wadau walipata fursa ya kuona rasimu ya utabiri wa hali ya hewa katika kipindi cha mwezi Machi hadi Mei 2022 na kuweza kutoa ushauri utaowezesha kuandaa mbinu na mipango ya kukabiliana na athari za utabiri huo. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania inatarajia kutoa rasmi utabiri wa msimu wa mvua za MASIKA 2022 kupitia vyombo vya habari, tarehe 17 Februari 2022.




Tuesday, February 8, 2022

TMA YATAKIWA KUBUNI VYANZO ENDELEVU VYA MAPATO



                

Naibu Katibu Mkuu wa Ujenzi na Uchukuzi, Dkt. Ally Possy akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea Makao Makuu ya TMA, katika ukumbi wa mikutano ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Ubungo Plaza, Tarehe 07/02/2022.

               

Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agnes Kijazi ambale pia ni Makamu wa tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), akifafanua jambo wakati Naibu Katibu Mkuu wa Ujenzi na Uchukuzi, Dkt. Ally Possy  alipotembelea Ofisi za TMA, Makao Makuu, Ubungo Plaza, Tarehe 07/02/2022.

             

           
                                   
                                  
         
     
      
Matukio kwa picha wakati Mhe.Dkt. Ally Possy akipata ufafanunuzi kutoka vitengo mbalimbali vya TMA wakati wa ziara ya kutembelea Makao Makuu ya TMA, Ubungo Plaza, Tarehe 08/02/2022.
 
   

Naibu Katibu Mkuu wa Ujenzi na Uchukuzi, Dkt. Ally Possy akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi mkuu na wafanyakazi wengine wa TMA baada ya ziara yake  Makao Makuu ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Ubungo Plaza, Tarehe 07/02/2022.

Dar es Salaam; Tarehe 07 Februari, 2022;

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), yatakiwa kubuni vyanzo endelevu vya mapato ili taasisi iweze kujiendesha na kuisaidia serikali katika uendeshaji wake. Hayo yalizungumzwa na Naibu Katibu Mkuu wa Ujenzi na Uchukuzi, Dkt. Ally Possy wakati alipotembelea Ofisi za TMA, Makao Makuu, Ubungo Plaza, Tarehe 07/02/2022.

“Tusiendeshe Mamlaka kwa hasara, mnatakiwa kubuni vyanzo vya mapato ambavyo vipo “sustainable” bila kuathiri au kuidumaza taasisi, japo tusigeuke kuwa Mamlaka ya ukusanyaji mapato TRA, tutoe huduma lakini pia tukusanye mapato ili kuisaidia serikali katika uendeshaji wake”. Alisema Dkt. Possy.

Katika hatua nyingine, Dkt. Possy aliipongeza TMA kuwa ni taasisi ya tofauti inayofanya kazi kwa ushirikiano wa pamoja na kupelekea kufanya kazi nzuri ya kusaidia maendeleo ya kimkakati na kijamii nchini. Aidha, aliahidi kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kuendelea kutoa ushirikiano mkubwa kwa TMA pale itakapohitajika.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu wa tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), Dkt. Agnes Kijazi aliishukuru wizara na kumueleza Naibu Katibu Mkuu kuwa Mamlaka imeshaanza kutekeleza jukumu jipya la uratibu na udhibiti wa huduma za hali ya hewa nchini.

“ Baada ya kusainiwa kwa kanuni 7 za Sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania Na. 2 ya mwaka 2019, miongoni mwa jitihada kubwa zilizofanywa na Mamlaka ni pamoja na kuanza utekelezaji wa kanuni hizo kwa ajili ya uratibu na udhibiti wa huduma za hali ya hewa nchini ikiwa ni jukumu jipya ambalo Mamlaka imekasimiwa”. Alisema Dkt. Kijazi.

Friday, February 4, 2022

UWEPO WA KIMBUNGA “BATSIRAI” KATIKA BAHARI YA HINDI

 



Dar es Salaam, 04 Februari 2022:

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inatoa taarifa ya uwepo wa kimbunga Batsirai katika maeneo ya Kusini Magharibi mwa bahari ya Hindi. Mamlaka imeendelea kufuatilia kimbunga hicho tangu kilipojitokeza katika bahari ya Hindi tarehe 27/01/2022 na kwa sasa kimesogea katika maeneo ya kisiwa cha Madagascar.

Uchambuzi wa mifumo ya hali ya hewa unaonesha kutokuwepo kwa uwezekano wa kimbunga Batsirai kufika katika Pwani ya Tanzania. Hata hivyo uwepo wa kimbunga Batsirai baharini unatarajiwa kuathiri mifumo ya hali ya hewa kwa baadhi ya maeneo hapa nchini ikiwa ni pamoja na kusababisha ongezeko la mvua; vipindi vya upepo mkali unaofika na kuzidi km 40 kwa saa na mawimbi makubwa baharini yanayozidi mita 2 hasa kwa maeneo ya ukanda wa pwani.

Maeneo yanayotarajiwa kupata vipindi vya mvua kubwa kutokana na uwepo wa kimbunga hicho baharini kati ya tarehe 04 hadi 08/02/2022  ni pamoja na mikoa ya Mtwara, Lindi, Ruvuma, Morogoro, Pwani, Singida, Dodoma, Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe na Rukwa. Hata hivyo mvua za Msimu zinaendelea katika maeneo mengine yanayopata mvua hizo.

USHAURI: Wananchi wanashauriwa kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania pamoja na kupata ushauri na miongozo ya wataalam katika sekta husika ili kupunguza athari zinazoweza kujitokeza.

Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania inaendelea kufuatilia mwenendo wa kimbunga hicho na kutoa mrejeo kila itakapobidi.

Friday, January 28, 2022

UTABIRI WA TMA NI WA UHAKIKA.

 

Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhe. Atupele Fredy Mwakibete (MB) akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea Makao Makuu ya TMA, katika ukumbi wa mikutano ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Ubungo Plaza, Tarehe 28/01/2022. 

Mwenyekiti wa Bodi ya TMA, Dkt. Buruhani Nyenzi akitoa neno la ukaribisho kwa Mhe. Atupele Fredy Mwakibete (MB) wakati wa ziara ya kutembelea Makao Makuu ya TMA, katika ukumbi wa mikutano ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Ubungo Plaza, Tarehe 28/01/2022. 

 Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agnes Kijazi ambale pia ni Makamu wa tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), akifafanua jambo wakati Mhe. Atupele Fredy Mwakibete (MB) alipofanya zira ya kutembelea Makao Makuu ya TMA katika ukumbi wa mikutano ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Ubungo Plaza, Tarehe 28/01/2022. 




Matukio mbalimbali katika picha wakati wafanyakazi wa TMA wakimsikiliza Mhe. Atupele Fredy Mwakibete (MB) alipofanya ziara yake ya kutembelea Makao Makuu ya TMA, katika ukumbi wa mikutano ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Ubungo Plaza, Tarehe 28/01/2022. 




Matukio kwa picha wakati Mhe. Atupele Fredy Mwakibete (MB) akipata ufafanunuzi kutoka vitengo mbalimbali vya TMA wakati wa ziara ya kutembelea Makao Makuu ya TMA, Ubungo Plaza, Tarehe 28/01/2022. 

Mhe. Atupele Fredy Mwakibete (MB) akiwa katika chumba maalum cha kurekodi video za utabiri wa hali ya hewa wakati wa ziara ya kutembelea Makao Makuu ya TMA, Ubungo Plaza, Tarehe 28/01/2022. 

Mhe. Atupele Fredy Mwakibete (MB) akisaini katika daftari la wageni wakati wa ziara ya kutembelea Makao Makuu ya TMA, Ubungo Plaza, Tarehe 28/01/2022. 


Dar es Salaam; Tarehe 28 Januari, 2022;

Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhe. Atupele Fredy Mwakibete (MB) ametoa rai kwa watanzania kutumia vizuri taarifa zinazotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kwa kuwa taarifa hizo ni za uhakika. Mhe. Mwakibete, alizungumza hayo wakati wa ziara ya kutembelea Makao Makuu ya TMA, Ubungo Plaza, Tarehe 28/01/2022.

“kwa niaba ya Serikali na watanzania wengine na mimi binafsi, na kwa niaba ya waziri wangu mwenye kubeba dhamana ya wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Prof. Mbarawa, niwapongeze sana kwani taarifa zenu zimekuwa za uhakika na ni za kweli”. Alisema. Mhe. Mwakibete.

“Ni rai yangu kwa taasisi zingine na wizara zingine tutumie kikamilifu taarifa zinazotoka Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini, kwa namna hiyo tutakuwa tunaokoa hasara zilizo mbele yetu na kujipanga”. Aliongezea Mhe. Mwakibete. 

Akizungumzia suala la changamoto ya maslahi duni, mhe. Waziri alisema kuwa atalisimamia suala hilo kwa kumshirikisha waziri mwenye dhamana na Mamlaka zingine ili kuona namna gani litashughulikiwa ili kuhakikisha wataalamu bingwa wa TMA hawahamia taasisi nyingine.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mwakibete alisema, Serikali inatambua umuhimu wa TMA nchini, hivyo Mhe. Rais. Samia Suluhu Hassan kwenye bajeti ya mwaka huu wa fedha, ametenga jumla ya Tsh. Bil. 30 ili kukamilisha mtandao wa rada saba nchini.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya TMA, Dkt. Buruhani Nyenzi alisema Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania ni taasisi ya Muungano  iliyoanzishwa kwa sheria  Na. 2 ya mwaka 2019 ikifanya kazi zake Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar chini ya usimamizi wa  Bodi ya TMA (Governing Board).

“Bodi ina jumla ya wajumbe 8, Mwenyekiti na Makamu ni wateule wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo Mwenyekiti anatokea Tanzania Bara na Makamu wake anatokea Tanzania Zanzibar, Wajumbe wengine watano (5) wa Bodi ni wateule wa Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana ya masuala ya hali ya hewa ambapo Katibu wa Bodi hiyo ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka. Hawa wajumbe wanawakilisha sekta muhimu zinazotumia taarifa za hali ya hewa”. Alisema Dkt. Nyenzi.

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agnes Kijazi ambaye pia ni Makamu wa tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), alifafanua kuwa Mamlaka imejiwekea malengo yanayolenga kutoa huduma bora zaidi na mahsusi kwa wadau na jamii ili kuchangia katika kutoa maamuzi na hatimaye kuleta maendeleo endelevu.

 Katika kutimiza azma ya Mhe. Rais ya kuwatumikia Watanzania na kutekeleza mipango ya Nchi yetu na ile ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) ya utoaji wa huduma bora za hali ya hewa nchini, Mamlaka imejipanga kuboresha huduma za hali ya hewa na kuendelea kuboresha miundombinu ya hali ya hewa hapa nchini. Aidha mafunzo kwa wafanyakazi na uboreshaji wa mifumo ya menejimenti ya rasilimali fedha itaboreshwa zaidi. Katika kuongeza ubora wa huduma za hali ya hewa, Mamlaka imejiwekea malengo ya kushiriki na kuchangia katika shughuli za hali ya hewa za kitaifa, kikanda na kimataifa hususani katika Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO)”. Alieleza Dkt. Kijazi.

Dkt. Kijazi aliishukuru serikali kwa  kuendelea kuiwezesha Mamlaka kuwa na vitendea kazi vya kisasa na wataalamu wenye ujuzi ikiwa ni pamoja na kuipatia TMA Rada nyingine mbili ambazo ukamilikaji wake utapelekea kufikiwa kwa malengo ya muda mrefu ya kuwa na Rada 7 za hali ya hewa kwa nchi nzima.

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...