Friday, February 11, 2022

TMA KUENDELEA KUTOA HUDUMA MAHSUSI ZA HALI YA HEWA KWA FAIDA ZA KIUCHUMI.


Wadau kutoka sekta mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi katika mkutano wa wadau, kujadili Utabiri wa Mvua za Msimu wa Masika (Machi hadi Mei, 2022) , katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 17 Februari 2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.


Mgeni rasmi, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Mkurugenzi wa Matumizi na Utafiti Dkt. Ladislaus Chang'a akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi wakati akifungua rasmi Mkutano wa Wadau wa Utabiri wa Mvua za Masika (Machi hadi Mei, 2022) , katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 17 Februari 2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.



Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri wa TMA, Dkt. Hamza Kabelwa  akiongea kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Dkt. Ladislaus Chang'a kufungua Mkutano wa Wadau wa Utabiri wa Mvua za Masika (Machi hadi Mei, 2022) , katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 17 Februari 2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.


Mtaalam wa Hali ya hewa kutoka TMA, Bi. Rose Senyagwa akiwasilisha mada katika Mkutano wa Wadau wa Utabiri wa Mvua za Masika (Machi hadi Mei, 2022) , katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 17 Februari 2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.

Mtaalam wa Hali ya hewa kutoka TMA, Bw. Ramadhani Omary akiwasilisha mada katika  Mkutano wa Wadau wa Utabiri wa Mvua za Masika (Machi hadi Mei, 2022) , katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 17 Februari 2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.









Wadau kutoka sekta mbalimbali wakiwasilisha mada katika  Mkutano wa Wadau wa Utabiri wa Mvua za Masika (Machi hadi Mei, 2022) , katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 17 Februari 2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.





Wadau kutoka sekta ya mbalimbali wakichangia mada katika  Mkutano wa Wadau wa Utabiri wa Mvua za Masika (Machi hadi Mei, 2022), katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 17 Februari 2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.










Wataalam bingwa wa hali ya hewa pamoja na wadau kutoka sekta mbalimbali wakiwa katika makundi wakijadili athari na ushauri kwa msimu wa mvua za Masika 2022 kupitia  Mkutano wa Wadau wa Utabiri wa Mvua za Masika (Machi hadi Mei, 2022), katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 17 Februari 2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.





Matukio kwa picha wakati wadau wakisikiliza mada mbalimbali zilizowasilishwa katika Mkutano wa Wadau wa Utabiri wa Mvua za Masika (Machi hadi Mei, 2022), katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 17 Februari 2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.



Dar es Salaam; Tarehe 11 Februari, 2022;

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imesema itaendelea kuimarisha utoaji wa  huduma mahususi za hali ya hewa ili kuongeza tija na ufanisi katika shughuli za kijamii na kiuchumi. Hayo yalizungumzwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Mkurugenzi wa Matumizi na Utafiti Dkt. Ladislaus Chang’a wakati akifungua rasmi Mkutano wa Wadau wa Utabiri wa Mvua za Masika 2022 kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi katika Ukumbi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT), Dar es Salaam, Tarehe 11/02/2022.

“Matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa na hasa katika kipindi ambapo dunia inakabiliwa na changamoto ya mabadiliko ya hali ya hewa na Tabianchi ni muhimu sana na  yatasaidia kufikiwa kwa malengo ya  mpango wa Taifa wa kujenga uchumi wa viwanda nchini na mikakati mingine ya kuleta maendeleo katika jamii na Taifa. TMA itaendelea kuimairisha utoaji wa  huduma mahsusi za hali ya hali ya hewa ili kuhakikisha malengo yanafikiwa”. Alisema Dkt. Chang’a.

Aidha, katika mkutano huo TMA ilitoa tathimini ya usahihi wa utabiri wa Msimu wa mvua za vuli 2021 zilizoisha mwezi Desemba 2021, ambapo tathmini hiyo ilionesha kuwa utabiri ulikuwa sahihi kwa asilimia 93.8, hivyo mamlaka inaendelea kuweka msisitizo wa matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa kwa kila sekta ili kuongeza tija na uzalishaji.

Kwa upande wa mdau kutoka Wizara ya Kilimo, Bw. Juma Makandi alisema mara baada ya kupata taarifa za utabiri wa msimu wa mvua za Vuli, Wizara iliaandaa na kutoa  tafsiri ya utabiri huo katika shughuli za kilimo kwa mawaziri pamoja na wakuu wa mikoa kwa ajili ya kuwawezesha kuweka mipango stahiki ya kukabiliana na athari za utabiri huo..

Naye, mdau wa Kilimo kutoka Zanzibar Bw. Nasoro Mkarafuu alieleza kuwa utabiri ulikuwa kama ulivyotabiriwa hivyo mipango iliyowekwa ya kushirikisha maafisa ugani ilienda kama ilivyopangwa.

Mdau kutoka ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Maafa alisema baada ya kupokea utabiri huo, idara iliandaa kikao kazi cha kujadili mpango wa dharura wa ukame unaoweza kujitokeza kutokana na utabiri uliotolewa sambamba na kuandaa vipindi vya elimu kwa umma kupitia vyombo mbalimbali va habari.

Katika Mkutano huo, wadau walipata fursa ya kuona rasimu ya utabiri wa hali ya hewa katika kipindi cha mwezi Machi hadi Mei 2022 na kuweza kutoa ushauri utaowezesha kuandaa mbinu na mipango ya kukabiliana na athari za utabiri huo. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania inatarajia kutoa rasmi utabiri wa msimu wa mvua za MASIKA 2022 kupitia vyombo vya habari, tarehe 17 Februari 2022.




No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...