Friday, June 17, 2016
MJUMBE WA KAMATI KUU YA SHIRIKA LA HALI YA HEWA DUNIA DKT. AGNES KIJAZI ASHIRIKI MKUTANO WA 68 WA KAMATI KUU YA UTENDAJI YA SHIRIKA LA HALI YA HEWA DUNIANI(WMO, EC-68), GENEVA, USWISI.
Picha za pamoja wakati wa Ufunguzi
wa Mkutano wa Sitini na Nane wa Kamati Kuu ya Utendaji ya Shirika la
Hali ya Hewa Duniani (WMO-EC 68), tarehe 15-24 Juni 2016, Geneva,
Uswisi ambapo Dkt. Agnes Kijazi-Mkurgenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa, ambaye pia ni Mwakilishi wa Kudumu wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani
na Mjumbe wa "WMO Excecutive Council" anashiriki. Dkt. Kijazi anashiriki
katika Mkutano huo pamoja na Meneja wa Mahusiano ya Kimataifa wa TMA,
Bw. Wilbert Muruke.
Friday, June 10, 2016
Sensitization Workshop on the Role and Contribution of the Work of the Commission of Climatology and IPCC
Sensitization Workshop on the Role and Contribution of the Work of the WMO Commission of Climatology (CCL) and the Intergovernmental Panel on Climate Change (IPCC) in Effective Implementation of Global Framework for Climate Services (GFCS).
This workshop was held under the auspice of the Global Framework for Climate Services (GFCS) project in Tanzania entitled “Climate Services Adaptation Programme in Africa on Building Resilience in Disaster Risk Management, Food Security, Nutrition and Health”.
Tuesday, June 7, 2016
MAMLAKA YA HALI YA HEWA (TMA) YATOA MWELEKEO WA HALI YA HEWA KWA KIPINDI CHA JUNI HADI AGOSTI 2016.
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa utabiri
wa mwelekeo wa hali ya hewa kwa kipindi cha Juni hadi Agosti mwaka huu.
Akizungumzia kuhusiana na mwelekeo huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, Meneja
Kituo Kikuu cha Utabiri Bw. Samwel Mbuya alisema “Nchi yetu inatarajia kuwa na hali ya baridi kiasi katika
kipindi hiki sambamba na vipindi vifupi vya mvua vinavyotarajiwa kujitokeza
katika maeneo machache hususan ya ukanda wa Ziwa Viktoria na ukanda wa pwani ya
Kaskazini (Visiwa vya Unguja na Pemba). Katika kipindi cha mwezi Juni hadi Agosti 2016, maeneo mengi ya nchi
yanarajiwa kuwa makavu na yenye hali ya baridi kiasi katika majira haya ya kipupwe.
Mifumo ya hali ya hewa
inaonesha matarajio ya hali ya joto la wastani hadi chini ya wastani katika
maeneo yaliyopo Kusini-magharibi mwa nchi. Hata hivyo, katika msimu wa Kipupwe
wa mwaka huu maeneo mengi ya nchi yanatarajiwa kuwa na joto la wastani hadi juu
ya wastani. Aidha, izingatiwe kuwa hali ya ubaridi inatarajiwa zaidi nyakati za
usiku hadi mapema asubuhi.
“Aliendelea kueleza sababu za
hali hiyo kuwa ni pamoja na kupungua kwa joto la bahari katika eneo la
ukanda wa Tropiki la bahari ya Pasifiki sambamba na Joto la baharí katika eneo
la magharibi wa bahari ya Hindi kuwa la
wastani kwa kipindi cha miezi ya Juni hadi Agosti 2016”. Aidha, joto katika
bahari ya Atlantiki linatarajiwa kuwa chini ya wastani. Hali hiyo inatarajiwa
kusababisha upepo kuvuma kutoka magharibi ukielekea mashariki hususan katika
maeneo ya Ukanda wa Ziwa Viktoria. Joto la bahari la juu ya wastani
linatarajiwa katika eneo la ncha ya kusini ya bara la Afrika hivyo kuathiri
msukumo wa upepo wa kusi.
Kwa upande mwengine, Afisa
Uhusiano wa TMA, Bi. Monica Mutoni alitoa msisitizo kwa wananchi kufuatilia taarifa
hususan za tahadhari zinazotolewa na Mamlaka kupitia vyombo mbalimbali vya
habari, tovuti ya Mamlaka n.k ili kuokoa maisha na mali. Bi. Monica alisema “Hivi
karibuni TMA imekuwa ikitoa tahadhari mbalimbali ikiwa ni pamoja na za kuwepo
kwa upepo mkali na mawimbi makubwa kwenye ukanda wa Bahari Hindi, Maziwa na nchi
kavu hivyo ni vyema wananchi hasa wale watumiaji wa bahari na maziwa kuchukua
hatua stahiki pindi taarifa kama hizo zinapotolewa”.
Aidha, TMA ilipongeza sekta mbalimbali
pamoja na Taasisi, Mamlaka za Serikali na jamii kwa ujumla kwa hatua stahiki zilizochukuliwa katika kipindi
cha msimu wa mvua za Masika 2016 kwa
kutumia Taarifa, Agalizo na Tahadhari za utabiri zilizotolewa na Mamlaka. Ni
wazi kuwa kwa hatua hizo madhara ambayo yangeweza kujitokeza yalidhibitiwa na
hivyo kuchangia katika kufanikisha mipango na utekelezaji wa shuguli za
kiuchumi na kijamii katika kipindi husika.
Kwa tarifa ya kina kuhusiana na
mwelekeo wa hali ya hewa kwa mkoa wako ingia kwenye tovuti ya TMA www.meteo.go.tz au tembelea ofisi zetu
IMETOLEWA
NA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA
Monday, June 6, 2016
MHE. PROF. MBARAWA ATEMBELEA KITUO CHA HALI YA HEWA-IRINGA
Meneja
wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), Mkoani Iringa Bw. Haji Musa Usantu
akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa
Makame Mbarawa alipokagua Mamlaka hiyo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (Mwenye Kofia) akitazama moja ya kifaa kinachopima hali ya hewa ya udongo alipokagua kiwanja cha Ndege cha Nduli Mkoani Iringa.Kulia ni Meneja wa (TMA) Mkoani humo Bw. Haji Musa Usantu.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Iringa (Nduli), Bi. Hanna Kibupile alipokikagua.
Picha kwa hisani ya Kitengo cha Mawasiliano- Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (Mwenye Kofia) akitazama moja ya kifaa kinachopima hali ya hewa ya udongo alipokagua kiwanja cha Ndege cha Nduli Mkoani Iringa.Kulia ni Meneja wa (TMA) Mkoani humo Bw. Haji Musa Usantu.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Iringa (Nduli), Bi. Hanna Kibupile alipokikagua.
Picha kwa hisani ya Kitengo cha Mawasiliano- Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
Thursday, May 26, 2016
HALI YA HEWA TUGHE YAPATA UONGOZI MPYA
Uongozi mpya wa TUGHE katika picha ya pamoja.
Baadhi ya wanachama wa TUGHE wakiomba kura ili kuweza kupata nafasi mbali mbali za uongozi sambamba na zoezi la uchaguzi.
Wanachama wa TUGHE (Pichani) wachagua viongozi wapya katika uchaguzi uliofanyika
tarehe 24 Mei 2016 kwenye ukumbi wa Makao Makuu-TMA. Viongozi waliochaguliwa ni
pamoja na Mwenyekiti Bi. Aurelia Mwakalukwa, Katibu Bw. Benjamin
Bikulamchi, Mwenyekiti wa kinamama Bi. Zainab Gumbo, Katibu wa kinamama
Bi. Hamida Hassan na wajumbe.
Na. Monica Mutoni
Tuesday, May 24, 2016
TV JOURNALIST WEATHER TRAINING DAR ES SALAAM, TANZANIA ON 20th MAY, 2016
This Public Weather Services training for Azam Journalists aimed at strengthening the link between the providers and users of public weather services, so that individuals, communities and organizations can make effective use of the available products and services and foster a better understanding and awareness of public weather services in terms of their availability, the terminology used, the way they can be used to the greatest effect and their socio-economic benefits as well as to easier communication among societies. The training aimed to meet World Met. Organization (WMO) requirements.
Training participants were from AZAM pay TV and training facilitators were from TMA and WMO.
Wednesday, May 18, 2016
SEVERE WEATHER EVENTS- EFFECTIVE PLANNING (SWEEP) TRAINING WORKSHOP HELD FROM 16 TO 27 MAY, 2016, DAR ES SALAAM, TANZANIA
Workshop is held under the auspice of the Pilot Project
called “The Multi Hazard Early Warning Service (MHEWS)” which focuses on the
coastal zone of Tanzania and across sectors of Marine transport, Fishing,
Agriculture, and Oil & Gas. MHEWS project is being funded by DFID trough
the WISER program.
The
objective of SWEEP Workshop is to ensure all stakeholders have a shared
and consistent understanding of the features and benefits of the Multi-hazard
Early Warning Services to effective planning.
Expected output is to equip participants with all the necessary skills and provide information on
the characteristics of the extremes and enable improved warning messages,
timely and effective communication among actors which will solely serve lives
and property and enhance socio-economic development in the country.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Featured Post
DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.
Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...
-
Dar es Salaam, Tarehe 05/02/2026; Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa rasmi utabiri wa msimu wa mvua za Masika 202 6 kwa maeneo...
-
DODOMA; Tarehe 19 Agosti, 2024; Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imekutana na wadau kutoka sekta mbalimbali nchini ili kujipanga na...
-
Dar es Salaam, 22 /0 8 /202 4 ; Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa utabiri wa msimu wa mvua za VULI 202 4 kwa maeneo yanayopat...







