Thursday, February 17, 2022

TMA YATOA UTABIRI WA MSIMU WA MVUA ZA MASIKA 2022 KWA MAENEO YANAYOPATA MVUA MARA MBILI KWA MWAKA.


 Dar es Salaam 17 Februari, 2022.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa rasmi utabiri wa msimu wa mvua za Masika 2022 kwa maeneo yanayopata mvua mara mbili kwa mwaka. Akizungumza wakati wa mkutano na vyombo vya habari katika Makao Makuu ya TMA, Ubungo Plaza, tarehe 17/02/2022, Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu wa tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), Dkt. Agnes Kijazi alisema maeneo ya nchi yanayopata misimu miwili ya mvua yanatarajiwa kupata mvua za wastani hadi juu ya wastani.

 

Mvua za Masika kwa kipindi cha Machi hadi Mei, 2022 zinatarajiwa kuwa za wastani hadi juu ya wastani, aidha mvua hizo zinatarajiwa kuanza mapema kati ya wiki ya tatu na ya nne ya mwezi Februari2022 na kuisha mwezi Mei 20202 katika maeneo mapema”. Alisema Dkt. Kijazi

 

“Mikoa inayopata mvua mara mbili kwa mwaka ni Mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro, Mikoa ya Dar es Salaam, Pwani ikijumuisha kisiwa cha Mafia Tanga na maeneo ya kaskazini mwa mkoa wa Morogoro pamoja na  visiwa vya Unguja na Pemba, Mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Mara pamoja na kaskazini mwa mkoa wa Kigoma”. Aliendelea Dkt. Kijazi.

 

Vilevile, taarifa hiyo imeeleza pia ongezeko la mvua linatarajiwa katika kipindi cha mwezi Machi 2022 katika maeneo ya pwani ya kaskazini na mwezi  Aprili katika maeneo ya tya nyanda za juu kaskazini mashariki.

 

Akizungumzia athari zinazoweza kujitokeza, Dkt. Kijazi alisema vipindi vifupi vya mvua kubwa vinaweza kujitokeza hivyo kuweza kusababisha mafuriko, uharibifu wa miundombinu, upotevu wa mali na maisha, milipuko ya magonjwa pamoja na athari nyingine zitokanazo na mvua nyingi.

 

Ilikupata taarifa zaidi za utabiri tembelea https://www.meteo.go.tz/weather_forecasts/seasonal-weather-forecast

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...