Tuesday, February 11, 2020

WITO WATOLEWA KWA WADAU KUJENGA TABIA YA KUFUATILIA TAARIFA ZA MREJEO ZA HALI YA HEWA KUTOKA TMA.

Wadau kutoka sekta mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi kwenye warsha ya wadau kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Masika (Machi - Mei 2020) unaotarajiwa kutolewa rasmi tarehe 13 Februari 2020 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania

Mgeni rasmi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya TMA Dkt. Buruhani Nyenzi akizungumza wakati akifungua warsha ya wadau kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Masika (Machi - Mei 2020) unaotarajiwa kutolewa rasmi tarehe 13 Februari 2020 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi  akiongea kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kwa ajili ya ufunguzi wa warsha ya wadau kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Masika (Machi - Mei 2020) unaotarajiwa kutolewa rasmi tarehe 13 Februari 2020 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.

Mratibu kutoka FAO Bw. Diomedes Kalisa akizungumza katika warsha ya wadau kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Masika (Machi - Mei 2020) unaotarajiwa kutolewa rasmi tarehe 13 Februari 2020 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.








Wadau kutoka sekta mbalimbali hapa nchini wakiwasilisha mada kupitia warsha ya wadau kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Masika (Machi - Mei 2020) unaotarajiwa kutolewa rasmi tarehe 13 Februari 2020 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.












Wadau mbalimbali wakichangia mada katika warsha ya wadau kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Masika (Machi - Mei 2020) unaotarajiwa kutolewa rasmi tarehe 13 Februari 2020 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.
 



Wadau kutoka sekta mbalimbali wakiwa katika makundi makundi, wakijadiliana na wataalamu wa hali ya hewa kupitia warsha ya wadau kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Masika (Machi - Mei 2020) unaotarajiwa kutolewa rasmi tarehe 13 Februari 2020 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.




Matukio kwa picha wakati wadau wakisikiliza mada mbalimbali zilizowasilishwa katika warsha ya wadau kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Masika (Machi - Mei 2020) unaotarajiwa kutolewa rasmi tarehe 13 Februari 2020 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.


Dar es Salaam; Tarehe 11 Februari, 2020;

Wadau kutoka sekta mbalimbali nchini wametakiwa kujenga tabia ya kufuatilia taarifa za hali ya hewa za mrejeo kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA). Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Bodi ya TMA, Dkt. Buruhani Nyenzi ambaye pia alikuwa mgeni rasmi wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Wadau wa Kujadili jinsi Utabiri wa Mvua za Msimu wa Machi hadi Mei 2020 (MASIKA) utakavyotumika katika Sekta Mbalimbali, uliofanyika tarehe 11 Februari, 2020 katika ukumbi wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (The Law School of Tanzania), Dar es Salaam.

"Baada ya mkutano huu, natoa wito kwa wadau kujenga tabia ya kufuatilia mrejeo wa taarifa za hali ya hewa zinazotolewa baada ya utabiri wa awali kutolewa, nasema hivi kwa vile hii ni hali ya hewa, upepo ukibadilika tu na hali ya hewa inabadilika hivyo ni vyema kufuatilia taarifa hizo kwa ukaribu". Alizungumza Dkt. Nyenzi

Vile vile, Dkt. Nyenzi alionesha imani yake kwa wadau hao kwamba anatarajia matokeo ya mkutano huo, yatatoa nafasi kwa watanzania kupata utabiri uliokamilika inavyotarajiwa, matumizi yake kiuchumi na kijamii pamoja na athari zinazoweza kutokea na hivyo kuwapa wananchi wasaa wa kujipanga ili kupunguza au kuepusha kabisa madhara.



Awali, wakati akikaribisha wadau hao, Dkt. Agnes Kijazi, Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) aliwashukuru wadau kwa kuitikia mwaliko wa TMA na kuwaeleza kuwa, TMA imejiwekea utaratibu wa kukutana na wadau kipindi cha misimu wa mvua ili utabiri utakaotolewa ukatumike vizuri. Aidha, kulingana na lengo la mkutano huo, Dkt. Kijazi alielezea kwa kina maeneo yanayotarajiwa kupata mvua za msimu wa MASIKA, huku akisisitiza utabiri utakaotolewa kutumika kwa faida.



Dkt. Kijazi pia aliwajulisha wadau kuhusiana na mabadiliko ya TMA kisheria na kufafanua jukumu jipya la Mamlaka la kudhibiti shughuli za hali ya hewa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hivyo kutokana na mabadiliko hayo, TMA inaendelea na uboreshaji wa huduma kwa sekta mbali mbali nchini. “Wadau wote wenye vifaa vya hali ya hew ani jukumu lao kisheria kuhakikisha vifaa hivyo vimesajiliwa na TMA” alisema Dkt. Kijazi.



“Mkihitaji utabiri maalum kwa ajili ya sekta zenu ni vyema wadau mkatuona ili tuweze kuwaandalia kwa vile huduma hii ipo kwaajili ya maendeleo ya nchi yetu na  ni vyema tukaitumia fursa hii, sisi pale ofisini tunautambua kama utabiri mahususi kwa sekta mbalimbali”. Alisema Dkt. Kijazi



Naye, Mratibu kutoka FAO, Ndugu. Diomedes Kalisa alielezea umuhimu wa taarifa za hali ya hewa katika sekta ya kilimo. Alisisitiza umuhimu wa kufuatilia taarifa za mrejeo huku akitoa wa mkulima aliyebadilisha aina ya mazao ya kupanda kutokana na taarifa za mrejeo za hali ya hewa  zilizotolewa na TMA na hatimaye alipata faida ukilinganisha na wakulima wengine.



Mkutano huu umeandaliwa na TMA kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) na hivyo kutoa wigo wa ufadhili  wa ushiriki wa wadau kutoka ngazi ya wilaya, ambapo maafisa kilimo kutoka ngazi ya wilaya walishiriki mkutano huo.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...