Wednesday, February 12, 2020

TMA YASISITIZA USHIRIKIANO NA WANAHABARI KATIKA USAMBAZAJI WA TAARIFA ZA HALI YA HEWA NCHINI.

Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agnes Kijazi katika picha ya pamoja na wanahabari walioshiriki warsha ya kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Masika (Machi – Mei 2020) unaotarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 13 Februari 2020 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza – Dar es Salaam, Tanzania.



Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agnes Kijazi akifunga rasmi warsha ya kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Masika (Machi – Mei 2020) unaotarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 13 Februari 2020 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza – Dar es Salaam, Tanzania.


Mkurugenzi wa huduma za utabiri wa TMA, Dkt. Hamza Kabelwa akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kwa ajili ya ufunguzi wa warsha ya kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Masika (Machi – Mei 2020) unaotarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 13 Februari 2020 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza – Dar es Salaam, Tanzania.

Msimamizi wa Kitengo cha Uhusiano cha TMA Bi. Monica Mutoni akiwasilisha mada katika warsha ya kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Masika (Machi – Mei 2020) unaotarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 13 Februari 2020 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza – Dar es Salaam, Tanzania.

Mtaalamu wa hali ya hewa wa TMA, Bw. Abuubakar Lungo akielezea mwenendo wa mifumo ya hali ya hewa kwa wanahabari katika warsha ya kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Masika (Machi – Mei 2020) unaotarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 13 Februari 2020 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza – Dar es Salaam, Tanzania.










Wanahabari mbalimbali wakichangia mjadala katika warsha ya kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Masika (Machi – Mei 2020) unaotarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 13 Februari 2020 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza – Dar es Salaam, Tanzania.



Wanahabari mbalimbali wakisikiliza kwa makini mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa katika warsha ya kujadili utabiri wa msimu wa mvua za Masika (Machi – Mei 2020) unaotarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 13 Februari 2020 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza – Dar es Salaam, Tanzania.


Dar es Salaam; Tarehe 12 Februari, 2020

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imeendelea kuwasisitiza wanahabari kuwa na ushirikiano wa mara kwa mara na TMA katika usambazaji wa taarifa za hali ya hewa ili taarifa ziweze kufika kwa wakati.

Hayo yamezungumzwa na Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), Dkt. Agnes Kijazi wakati wa Warsha ya Wanahabari kuhusu Mwelekeo wa Msimu wa Mvua za Mwezi Machi hadi Mei 2020 (Masika), iliofanyika tarehe 12 Februari, 2020 katika ukumbi wa Mikutano- TMA, Ubungo Plaza, Dar es Salaam.

 Warsha hii ni muendelezo wa juhudi za mamlaka kutaka kuhakikisha taarifa za utabiri wa hali ya hewa zinawafikia walengwa ikiwemo jamii kwa uhakika, usahihi na kwa wakati”. Alizungumza Dkt. Kijazi.

Aidha, Dkt. Kijazi alisema taarifa za hali ya hewa zikiifikia jamii kwa wakati, uhakika na usahihi itaisaidia jamii kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya hali ya hewa pia itazisaidia mamlaka zinazohusika kupanga mipango endelevu ambayo haiwezi kuathiriwa na hali mbaya ya hewa, hivyo uelewa wa pamoja ni muhimu ili jamii iweze kunufaika na taarifa za hali ya hewa zinazotolewa.

TMA ikitoa tahadhari ya mvua kubwa na wewe mwanahabari ukakuta eneo lenye mafuriko, stori yako ianzie kwenye tahadhari iliyotolewa na hali halisi iliyotokea na hatua ambayo wananchi wangepaswa kuchukua na kumalizia na msisitizo wa kuzitumia vyema taarifa za hali ya hewa. Kwa njia hiyo utakuwa hukutoa tuu habari bali umeelimisha jamii”. Aliongezea Dkt. Kijazi
 
Mamlaka imekuwa ikihakikisha inakutana na wanahabari ambao ni daraja muhimu katika kuwafikia wananchi wote kwa ujumla ili kupata uelewa wa pamoja na namna bora ya kusambaza taarifa za hali ya hewa ambapo katika warsha hiyo wanahabari wanapata nafasi ya kupitia rasimu ya mwelekeo wa mvua za masika na viashiria vilivyopelekea kupatikana kwa utabiri wa hali ya hewa kwa msimu  huo wa mwezi Machi hadi Mei 2020.

Taarifa rasmi ya Mwelekeo wa Msimu wa Mvua za Masika kwa kipindi cha mwezi Machi hadi Mei 2020 itatolewa rasmi kwa vyombo vya habari, Tarehe 13 Februari 2020, Siku ya Alhamis, Ofisi za TMA-Makao Makuu, Ubungo Plaza, Dar es Salaam.


No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...