Friday, August 23, 2019

TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA 53 WA UTOAJI WA UTABIRI WA HALI YA HEWA WA MSIMU WA MVUA ZA VULI 2019 KATIKA NCHI ZA PEMBE YA AFRIKA




Tanzania kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inatarajia kuwa mwenyeji wa mkutano wa 53 wa Utoaji wa Utabiri wa Hali ya Hewa wa Msimu wa Mvua za Vuli 2019 “Fifty Third Greater Horn of Africa Climate Outlook Forum” (GHACOF 53) utakao fanyika katika  Hotel ya Kilimanjaro (Hyatt Regency) kuanzia tarehe 26 hadi 28 Agosti 2019 Dar es Salaam.

Lengo la mkutano huo ni kujadili na kuandaa kwa pamoja utabiri wa msimu wa mvua za vuli za mwezi Oktoba hadi Desemba 2019, pamoja na kuandaa mikakati ya kukabiliana na hali mbaya ya hewa kwa msimu huo kwa kulenga sekta muhimu za kijamii na kiuchumi ambazo ni pamoja na afya, kilimo na usalama wa chakula, maji, nishati n.k.

Mkutano huo utajumuisha nchi za Pembe ya Afrika ambazo ni Tanzania, Kenya, Somalia, Ethiopia, Sudan, Sudan ya Kusini, Uganda, Burundi, Rwanda, Djibouti na Eritrea

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...