Wednesday, February 13, 2019

WANAHABARI NA WATAALAM WA HALI YA HEWA WAKAA MEZA MOJA KUJADILI UTABIRI WA MVUA ZA MASIKA.

Washiriki wa warsha ya wanahabari kuhusu msimu wa mvua za masika,  mwezi Machi hadi Mei 2019 katika picha ya pamoja


Tarehe 13 Februari 2019

Ikiwa ni mwendelezo wa ushirikishwaji wa wadau mbalimbali katika kuhakikisha huduma za hali ya hewa zinawafikia wananchi kwa wakati na kwa lugha inayoeleweka. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imekutana na wanahabari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini kujadili mwelekeo wa msimu wa mvua za MASIKA kwa 2019 kabla ya kutolewa rasmi kwa umma tarehe 14 Februari 2019.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo katika ukumbi wa mikutano wa ‘Law School’, Dkt. Ladislaus Chang’a ambaye ni Mkurugenzi wa Utafiti na Matumizi ya tarifa za hali ya hewa wa TMA alisema kuwa dhamira ya kukutana na wanahabari ni muendelezo wa dhamira na utaratibu wa TMA wa kuimarisha ushilikishwaji na kuendelea kuwajengea uwezo wanahabari ili wazielewe vizuri zaidi taaarifa za hali ya hewa na hususani utabiri na hivyo waweze kuzifikisha taarifa, kuhabarisha na kuelimisha jamii kwa ufasaha na ufanisi zaidi.

Aidha wanahabari walitumia fursa hiyo kujadili na kutoa mapendekezo ya kuboresha ufungashwaji na usambazaji wa tarifa za hali ya hewa ili ziendelee kuwafikia walengwa kwa wakati na kwa ufasaha zaidi. Pia walielezea umuhimu wa kuwajengea uwezo wanahabari kuzielewa kwa kina tarifa za hali ya hewa na mabadiliko yake.

Mkutano huo wa siku moja umeandaliwa chini ya mwamvuli wa Awamu ya Pili ya Programu ya Kidunia ya Utoaji wa Huduma za Hali ya Hewa ya GFCS yaani “Global Framework for Climate Services Adaptation Programme in Africa (APA) II” hapa Tanzania yenye lengo la kuimarisha huduma za hali ya hewa katika nyanja ya utoaji, usamabazaji na utumiaji wa huduma hizo. Mkutano huu ulijumuisha wanahabari kutoka kwenye vituo vya televisheni, redio, magazeti, blogs na mitandao ya kijamii

IMETOLEWA NA MONICA MUTONI
OFISI YA UHUSIANO
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA

Sunday, February 10, 2019

WATAALAMU WA HALI YA HEWA KUHAKIKISHA USAHIHI WA UTABIRI WA MVUA ZA MASIKA UNAKUWA WA HALI YA JUU


Katikati ya waliokaa ni mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa dkt. Agnes Kijazi kwenye picha ya pamoja na wataalam wa hali ya hewa, wakati akifungua warsha ya wataalamu wa hali ya hewa katika kuandaa utabiri wa mvua za msimu wa Masika (Machi hadi Mei 2019).





Matukio mbalimbali kwa picha wakati wataalam wa hali ya hewa wakichambua mifumo ya hali ya hewa katika maandarizi ya utabiri wa hali ya hewa kwa msimu wa masika (Machi hadi Mei 2019)

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dkt. Agnes Kijazi amewata wataalam wa hali ya hewa kutumia utalaam wao walionao kuhakikisha maandalizi ya utabiri wa hali ya hewa kwa msimu wa mvua za masika (Machi hadi Mei2019) unaendelea kuwa sahihi zaidi katika kiwango cha juu na wenye ubora utakaosaidia maendeleo ya kiuchumi katika taifa letu. Dkt. Kijazi alizungumza hayo wakati wa kufungua warsha ya wataalamu wa hali ya hewa katika kuandaa utabiri huo. 
 Warsha hiyo itafuatiwa na warsha ya wataalamu mabingwa wote wa hali ya hewa pamoja warsha ya wadau wa huduma za hali ya hewa na warsha ya wanahabari kabla ya kutoa  rasmi mwelekeo wa msimu wa mvua za MASIKA 2019 tarehe 14 Februari 2019.

Wednesday, January 30, 2019

THE 17TH GFCS PROJECT DELIVERY TEAM (PDT) INVITED DEVELOPMENT PARTNERS, NGO’s AND SECTOR MINISTRIES TO BRAINSTORM ON IMPLEMENTATION OF NATIONAL FRAMEWORK FOR CLIMATE SERVICES.

The PDT members and other invited participants on the group photo during a 17th PDT meeting which took place on 17th January 2019 at Ubungo Plaza, 
Dar es Salaam.


On 17th January 2019, The Global Framework for Climate Services (GFCS), Tanzania Project Delivery Team (PDT) organized an extended PDT with invitees from UN agencies, NGO’s and Sector Ministries with the aim of obtaining needs and suggestions for effective implementation of the NFCS.
During the opening of the meeting, the acting PDT Chair Mr. Juvenal Kisanga appreciated the participation of the invited participants ‘I appreciate the participation of  NGOs, Sector Ministries, and Development partners as I believe they have crucia role in succesfuly implementation of the NFCS, and  their presence will assist in gathering needs, ideas and suggestions for  efective implementation of the NFCS’ said Mr. Kisanga.
Invited participants were from President Offices’-Regional,Administration and Local Government (PO-RALG), Ministry of Livestock and Fisheries (MoLF), World Bank, TANESCO,  Tanzania Renewable Energy Association (TAREA) and Climate Action Network TZ (CANTZ) and Centre for Community Initiatives TZ (CCItz) .       

           
On the other hand, PDT received progress reports on implementation of GFCS APA phase II from Tanzania Red Cross Society (TRCS), Tanzania Meteorological Agency (TMA), World Food Programme (WFP) and Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children (MoHCDGEC), and encourage other project partners to speed up implementation of agreed activities.  The PDT was also briefed about the TADMAC meeting, which was held on 4th January 2019. Dr. Agnes Kijazi, the Director General of Tanzania Meteorological Agency, and Ms. Mecklina Merchades, the GFCS Desk Officer attended the meeting and presented a progress report on the implementation of GFCS Phase II.


PDT is responsible for monitoring progress on programme activities, planning and implementing joint activities, which normally meets quarterly and consists of  participants from Tanzania Prime Minister’s Office (PMO), Vice President Office (VPO), Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children (MoHCDGEC), Ministry of Agriculture (MoA), World Health Organization (WHO), World Food Program (WFP-TZ), Tanzania RedCross Society (TRCS) and Tanzania Meteorological Agency (TMA).


Released by: Monica Mutoni, Communication Officer, TMA

Wednesday, January 16, 2019

TMA YASHIRIKI VIKAO VYA KAMATI ZA BUNGE ZA MIUNDOMBINU.

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu wakiwa katika kikao  kilichofanyika katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dkt. Agnes Kijazi wakati akiwasilisha mada katika kikao cha Kamati hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dkt. Agnes Kijazi wakati akiwasilisha mada katika kikao cha Kamati ya Bunge ya Mindombinu katika kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika Bungeni Jijini Dodoma, kushoto kwake ni mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Moshi Kakoso.
Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu wakiwa katika kikao kilichofanyika katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma wakimsikiliza Mwanasheria wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Bw. Emmanuel Ntenga wakati akiwasilisha mada katika kikao cha Kamati hiyo.
Mwanasheria wa Bunge, Ndugu Thomas Shawa akiwapitisha wajumbe wa Kamati ya Miundombinu katika Muswada Sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania wa mwaka 2018 unaotarajiwa kuwasilishwa na Serikali katika Kamati hiyo Januari 16, 2019. Wa kwanza ni mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Moshi Kakoso.Kikao hicho cha Kamati kimefanyika katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma.

Chanzo: Michuzi blog


Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...