Tuesday, August 21, 2018
Katibu Mkuu wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Prof. Petteri Taalas awasili nchini kwa ziara ya kikazi
Katibu Mkuu Shirika la Hali ya Hewa Duniani Prof. Petteri Taalas awasili nchini kwa ziara ya kikazi. Pichani akipokelewa na mwenyeji wake Mkurugenzi Mkuu wa TMA dkt. Agnes Kijazi na Mkurugenzi Mkuu wa TCAA bw. Hamza Johari.
Monday, August 20, 2018
UZINDUZI WA MFUMO WA TAIFA WA HUDUMA ZA HALI YA HEWA
Tarehe 21 Agosti, 2018 Mhe. Jenista Mhagama, Waziri wa Nchi Ofisi ya
Waziri Mkuu anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa mfumo wa
Taifa wa Huduma za Hali ya Hewa, utakaofanyika katika kituo cha mikutano
cha kimataifa cha Mwl. Julius Nyerere, Dar es salaam kuanzia saa
saba(7) mchana.
TMA YAWA MWENYEJI WA MAFUNZO YA UTUMIAJI WA MFUMO WA TEKNOLOJIA YA KUBORESHA HUDUMA ZA UTABIRI WA HALI YA HEWA.
Washiriki wa mafunzo ya kozi ya (OSCAR/SURFACE) kwenye picha ya pamoja na Mgeni rasmi Mhe, Mr. Mrisho Gambo aliyeketi katikati (mstari wa mbele).
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA YAWA MWENYEJI WA MAFUNZO YA UTUMIAJI WA MFUMO WA TEKNOLOJIA YA KUBORESHA HUDUMA ZA UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA NCHI 23 ZINAZOONGEA LUGHA YA KINGEREZA BARANI AFRIKA.
Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) imekuwa mwenyeji wa mafunzo ya utumiaji wa mfumo wa teknolojia ya kuboresha huduma za utabiri wa hali ya hewa kwa nchi 23 zinazoongea lugha ya kingereza barani Afrika (Observing Systems Capability Analysis and Review Tool for the Metadata of surface - based observing systems ( OSCAR/SURFACE)). Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo washiriki jinsi ya kutumia mfumo huo katika nchi zao. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo, mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo ambaye pia alikuwa mgeni rasmi, aliwashukuru Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) kwa kufadhili mafunzo hayo na kuchagua Arusha kuwa sehemu ya kufanyia mafunzo. Aidha aliwataka washiriki wote kutumia taaluma watakayoipata katika kuongeza ujuzi wa kukabiliana na changamoto zinazoikumba bara la Afrika ili kuhakikisha Afrika haiachwi nyuma katika maendeleo endelevu. Amesisitiza umuhimu wa mchango wa huduma za hali ya hewa kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii wakiwa pamoja na sekta za kilimo, nishati, utalii, afya n.k
Mafunzo hayo yamefanyika Mkoani Arusha kuanzia tarehe 15 hadi 17 Agosti 2018.
Imetolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.
Tuesday, August 14, 2018
TMA YAWA MWENYEJI WA MKUTANO WA MRADI WA HIGH IMPACT WEATHER LAKE SYSTEM (HIGHWAY)”
Mamlaka
ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imekuwa mwenyeji wa mkutano wa Mradi wa HIGH Impact Weather lAke sYstem (HIGHWAY)” unaojadili namna ya
kuongeza uwezo za nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) zilizoko kwenye
eneo la bonde la Ziwa Victoria katika kupima na kufuatilia mifumo ya hali ya
hewa hususani ile inayosababisha hali mbaya ya hewa ndani ya Ziwa Victoria kwa
lengo la kuokoa maisha ya watu na mali zao "HIGH Impact Weather lAke sYstem (HIGHWAY) Gap Analysis". Mradi wa HIGHWAY
unafadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Nchini Uingereza (DFID) kupitia program
yake ya Weather and Climate Information Services for Africa (WISER)” na kutekelezwa
kwa ushirikiano na Sekretariet ya EAC, Shirika la Hali ya hewa Duniani(WMO), na
Taasisi za Hali ya Hewa za nchi wanachama wa EAC. Mkutano huu unafanyika Jijini Arusha kuanzia
tarehe 13 hadi 14 Agosti 2018.
Monday, August 6, 2018
DKT.TIZEBA ASISITIZA USHIRIKISHWAJI WA TMA KWENYE MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO YA KILIMO
TMA YAENDELEA KUTOA ELIMU YA HUDUMA ZA HALI YA HEWA KATIKA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI KWA MAENDELEO YA VIWANDA KUPITIA MAONESHO YA NANENANE 2018 NCHINI
| Mtaalam kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania Dkt. Habiba Mtongori akitoa elimu ya sayansi ya hali ya hewa kupitia satelaiti kwenye maonesho ya Nane Nane 2018 mkoani Morogoro |
|
|
![]() |
| Baadhi ya wananchi katika picha wakiendelea kufurika katika banda la Mamlaka ya Hali ya Hewa kwenye maonesho ya Nane Nane 2018 mkoani Simiyu |
![]() |
| Baadhi ya wananchi katika picha wakipata elimu ya upimaji kasi na mwelekeo wa upepo kwenye maonesho ya Nane Nane 2018 mkoani Mbeya |
Sunday, August 5, 2018
MKUU WA MKOA WA SIMIYU AFURAHISHWA NA JITIHADA ZA TMA ZA KUWATEMBELEA WANAFUNZI MASHULENI MKOANI SIMIYU IKIWA NI MOJA YA MKAKATI WA KUTOA ELIMU YA HALI YA HEWA KWA JAMII KUPITIA YA MAONESHO YA NANE NANE 2018
![]() |
| Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akipata maelezo kuhusiana na huduma mbalimbali zinazotolewa na TMA alipotembelea banda la Mamlaka kwenye viwanja vya Nyakabidi, Simiyu Tarehe 05 Agosti 2018. |
![]() |
| Mtaalam wa hali ya hewa kutoka TMA akitoa elimu kwa wananchi waliotembelea banda la TMA kwenye viwanja vya Nyakabidi, Simiyu |
![]() |
| Mtaalam wa hali ya hewa kutoka TMA akitoa elimu kwa wananchi waliotembelea banda la TMA kwenye viwanja vya Nyakabidi, Simiyu |
![]() |
| Wananchi mbalimbali wakiendelea kufurika katika banda la TMA kwenye viwanja vya Nyakabidi, Simiyu |
Subscribe to:
Posts (Atom)
Featured Post
DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.
Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...
-
Dar es Salaam, Tarehe 05/02/2026; Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa rasmi utabiri wa msimu wa mvua za Masika 202 6 kwa maeneo...
-
DODOMA; Tarehe 19 Agosti, 2024; Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imekutana na wadau kutoka sekta mbalimbali nchini ili kujipanga na...
-
Dar es Salaam, 22 /0 8 /202 4 ; Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa utabiri wa msimu wa mvua za VULI 202 4 kwa maeneo yanayopat...









