Tuesday, March 17, 2020

TMA YAPONGEZWA KUBORESHA HUDUMA ZA HALI YA HEWA KWA WATUMIAJI WA ZIWA VIKTORIA

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Mhe. Emmanuel Shilembi (Katikati) akizungumza wakati akifungua warsha ya “Utoaji Elimu Kuhusiana na usambazaji na matumizi ya Huduma na taarifa za Hali ya Hewa Zinazozingatia Athari (A workshop on the use and dissemination of Impact Based Early Warning products), iliyofanyika katika ukumbi za Halmashauri ya manispaa ya Muleba Tarehe 10 Machi 2020. Kushoto ni mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania Ndugu. Steven Malundo



Sengerema, 12/03/2020:
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) iliandaa warsha na kukutana na  wadau kutoka sekta ya uvuvi katika Ziwa Victoria, kwa wilaya ya Muleba il tarehe 10 Machi, 2020 na Sengerema tarehe 12 Machi, 2020. Lengo la warsha ilikuwa ni kutoa Elimu Kuhusiana na usambazaji na matumizi ya huduma na taarifa za Hali ya Hewa Zinazozingatia Athari (A workshop on dissemination and the use of Impact Based Early Warning products)

Katika ufunguzi wa warsha iliyofanyika wilayani Muleba mgeni rasmi alikuwa Mhe. Emmanuel Shilembi ambaye aliipongeza TMA kwa kazi nzuri inayoifanya ya kuendelea kuboresha utoaji wa huduma za hali ya hewa kwa wananchi hususan wavuvi wanaotumia Ziwa Victoria kama kitega uchumi cha kuendesha maisha yao ya kila siku.
“Ninawapongeza sana TMA kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kuendelea kuboresha huduma za hali ya hewa kwa wananchi hususan watumiaji wa Ziwa Viktoria, huduma hizo zimechangia kwa Kiasi kikubwa kupunguza majanga yatokanayo na hali mbaya ya hewa”. Alisisitiza Mhe. Emmanuel Shilembi

Aidha, mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa TMA ndugu. Steven Malundo aliwashukuru wadau kwa kuitikia wito wa kushiriki katika warsha hiyo muhimu pamoja na kuelezea kuwa warsha hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) wa kuboresha huduma za hali ya hewa kwa watumiaji wa Ziwa Viktoria uitwao “HIGH Impact Weather IAke sYstems (HIGHWAY), ambao kwa hapa Tanzania unatekelezwa katika wilaya za Sengerema-Mwanza na Muleba-Kagera kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Uingereza (DFID).

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...