Thursday, March 19, 2020

MHE. NDITIYE AAGIZA BARAZA LA TMA KUANDAA MIONGOZO NA MAFANIKO YENYE TIJA KWA SERIKALI.

Mhe. Mhandisi. Atashasta Nditiye akihutubia Baraza la Wafanyakazi, TMA, lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020.
Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Bodi ya TMA Bi. Jane Kikunya, akitoa neno kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi wa Baraza la Wafanyakazi  TMA, lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020.

Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) Dkt. Agnes Kijazi akizungumza katika Baraza la Wafanyakazi TMA, lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020

Meneja Rasilimali Watu na msimamizi wa Divisheni ya Huduma Saidizi wa TMA, akitoa maelezo mafupi katika Baraza la Wafanyakazi  TMA, lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020.

Mwenyekiti wa TUGHE - TMA, Bi. Aurelia Mwakalukwa akiwasilisha taarifa ya TUGHE - Makao Makuu TMA katika Baraza la Wafanyakazi  TMA, lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020

Mwenyekiti wa TUGHE – Zanzibar  Ndg. Awesi Kheri Awesi akiwasilisha Salamu za TUGHE - Zanzibar katika Baraza la Wafanyakazi  TMA, lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020

Mwenyekiti kinamama Zanzibar  Bi. Zaituni Khamis akiwasilisha Salamu za kinamama Zanzibar katika Baraza la Wafanyakazi  TMA, lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020

Mwenyekiti kinamama TMA - Makao Makuu, Bi. Zainab Gumbo akiwasilisha Salamu za kinamama wa TMA katika Baraza la Wafanyakazi TMA, lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020

Mfanyakazi bora wa TMA, Ndg. Kisumo Msangi kutoka kituo cha TMA - Arusha akizungumza katika Baraza la Wafanyakazi TMA, lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020

Mwakilishi toka TUGHE  akimtambulisha mfanyakazi bora wa TMA 2020 katika Baraza la Wafanyakazi TMA, lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020



Watoa mada wakiwasilisha mada za mkataba mpya wa baraza na mkataba mpya wa hali bora kazini, Ukimwi na Korona katika Baraza la Wafanyakazi TMA, lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020

Katibu wa Baraza la Wafanyakazi TMA, Ndg. Chuki Sangalugembe  akitambulishwa kwa ajumbe wa Baraza la Wafanyakazi TMA, mara baada ya uchaguzi katika Baraza la Wafanyakazi TMA, lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020

Katibu msaidizi wa Baraza la Wafanyakazi TMA, Bi. Meklina Merchedez akitambulishwa kwa ajumbe wa Baraza la Wafanyakazi TMA, mara baada ya uchaguzi katika Baraza la Wafanyakazi TMA, lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020


Waalikwa wa Baraza la Wafanyakazi la TMA wanaotarajia kustaafu mwaka huu 2020 wakiaga wajumbe wa Baraza hilo katika Baraza la Wafanyakazi TMA, lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020

Meza Kuu, wakati wa ufunguzi rasmi wa Baraza la Wafanyakazi TMA, lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020

Meza Kuu, wakati wa uchaguzi wa mfanyakazi bora katika Baraza la Wafanyakazi TMA, lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020




Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi TMA, wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa katika baraza  hilo lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020

Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi TMA, wakiwakumbuka wajumbe wa Baraza hilo waliofariki katika baraza  hilo lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020


Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi TMA, wakiimba wimbo wa mshikamano “ Solidarity Forever” kwa kutumia ishara ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Korona katika baraza  hilo lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020


Wajumbe wa Baraza la wafanyakazi la TMA katika picha ya pamoja na mgeni Rasmi Mhe. Mhandisi. Atashasta Nditiye katika baraza  hilo lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020

Mjumbe wa Baraza, Meneja wa Kanda ya Nyanda za juu Kusini Ndg. Issa Hamad akiwasilisha maazimio ya Baraza la wafanyakazi wa TMA katika baraza  hilo lililofanyika Dodoma Tarehe 16 na 17 Machi, 2020


Dodoma, Tarehe: 16/03/2020;
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Uchukuzi na Mawasiliano) Mhe. Mhandisi. Atashasta Nditiye ameagiza wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kuandaa miongozo na mafanikio yenye tija kwa Mamlaka  na Serikali kupitia mijadala ya Baraza hilo.

Mhe. Mhandisi. Nditiye alitoa maagizo hayo wakati akifungua Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) linalofanyika katika Ukumbi wa Takwimu, Dodoma, Tarehe 16 na 17 Machi 2020.

Hakikisheni kwamba mnaweka vyema vipaumbele vyenu, na kutimiza mambo ya msingi kwanza ili kukabiliana na tatizo la ufinyu wa bajeti lililopo”. Alisema Mhe. Mhandisi. Nditiye

Aidha Mhe. Naibu Waziri aliitaka Mamlaka kuharakisha upatikanaji wa kanuni ili sheria ianze kufanya kazi kurahisisha ufanisi wa majukumu ya  Mamlaka.
 Endeleeni kuboresha utabiri na kutoa tahadhari za hali mbaya ya hewa kwa wakati na kwa usahihi kwa jamii ya watanzania na wageni wanaotembelea nchini, kwa kusema hivi naamini michango yenu katika mkutano huu wa Baraza lenu la wafanyakazi, itatoa matokeo makubwa yatakayoendeleza sekta ya hali ya hewa nchini na pia kuliwezesha Taifa letu kusonga mbele kiuchumi na kimaendeleo”. Alisisitiza Mhe. Mhandsi. Nditiye.
Naye, Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) Dkt. Agnes Kijazi alimshukuru Mhe. Naibu Waziri kwa kujumuika na wajumbe wa Baraza katika ufunguzi wa Baraza hilo na Wizara kwa ujumla kwa ushirikiano mkubwa iliyoonesha katika kuboresha muundo mpya wa Mamlaka unaolenga kuboresha maslahi ya wafanyakazi..
“Uwepo wako umetupa nguvu na ari mpya katika kutekeleza majukumu yetu kwa ufanisi zaidi hasa katika kipindi hiki ambacho TMA imekuwa Mamlaka kamili”.Alieleza Dkt. Kijazi
Aliendelea kwa kumueleza kuwa Baraza la mwaka huu ni kwa mujibu wa mkataba mpya kati ya Menejiment na TUGHE na linajumuisha wajumbe 98 kutoka vituo mbali mbali vya hali ya hewa hapa nchini ikijumuisha viongozi na wawakilishi wa wafanyakazi.                                      
Kwa upande wake mwakilishi wa Mwenyekiti wa Bodi ya TMA, Bi Jane Kikunya alimuomba Mhe. Naibu Waziri kusaidia katika kutatua changamoto ya ufinyu wa bajeti kwa kuongeza zaidi bajeti kwaajili ya kusaidia uboreshaji wa vifaa vya hali ya hewa
Mkutano huo wa Baraza ulianza na elimu ya namna ya kukabiliana na maambukizi ya virusi vya Korona katika maeneo yao ya kazi na jamii kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...