Wednesday, March 18, 2020

MSAJILI WA HAZINA AAGIZA TMA KUCHANGIA MFUKO WA SERIKALI KUPITIA UKUSANYAJI WA MAPATO.

Washiriki wa mafunzo ya Udhibiti na Ukusanyaji wa Mapato yaliyoandaliwa mahususi kwa Menejiment ya TMA, Dodoma, Tarehe 13 Machi 2020 katika picha ya pamoja na mgeni rasmi.
Msajili wa Hazina Ndugu. Athumani Selemani Mbuttuka. akizungumza na washiriki wa mafunzo ya Udhibiti na Ukusanyaji wa Mapato yaliyoandaliwa mahususi kwa Menejiment ya TMA, Dodoma, Tarehe 13 Machi 2020
Mkurugenzi Mkuu Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) Dkt. Agnes Kijazi akiwasilisha maelezo ya awali wakati wa mafunzo ya Udhibiti na Ukusanyaji wa Mapato yaliyoandaliwa mahususi kwa Menejiment ya TMA, Dodoma, Tarehe 13 Machi 2020
Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Mafunzo kwa Njia ya Mtandao (TaGLA), Ndugu, Charles Senkondo akifafanua jambo wakati wa mafunzo ya Udhibiti na Ukusanyaji wa Mapato yaliyoandaliwa mahususi kwa Menejiment ya TMA, Dodoma, Tarehe 13 Machi 2020
Mwezeshaji kutoka Wakala wa Mafunzo kwa Njia ya Mtandao (TaGLA) Ndugu, Felix Ngamlagosi akitoa maelezo ya jinsi mafunzo yalivyoenda katika mafunzo ya Udhibiti na Ukusanyaji wa Mapato yaliyoandaliwa mahususi kwa Menejiment ya TMA, Dodoma, Tarehe 13 Machi 2020
Meneja wa Mazingira na Utafiti kutoka TMA, Dkt. Sarah Osima akiwasilisha mada kwa ufupi katika mafunzo ya Udhibiti na Ukusanyaji wa Mapato yaliyoandaliwa mahususi kwa Menejiment ya TMA, Dodoma, Tarehe 13 Machi 2020
Baadhi ya washiriki wa mafunzo wakipokea  vyeti vya ushiriki wa mafunzo ya Udhibiti na Ukusanyaji wa Mapato yaliyoandaliwa mahususi kwa Menejiment ya TMA, Dodoma, Tarehe 13 Machi 2020.





Dodoma, Tarehe: 13/03/2020;

Msajili wa Hazina Ndugu. Athumani Selemani Mbuttuka ameiagiza Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kuchangia katika mfuko wa serikali kupitia ukusanyaji wa mapato. Hayo yalizungumzwa wakati akifunga Mafunzo ya Udhibiti na Ukusanyaji wa Mapato yaliyoandaliwa mahususi kwa Menejiment ya TMA, Dodoma, Tarehe 13 Machi 2020.

“Kupitia Ofisi yangu tutaendelea kuwasaidia na kuwapa ushirikiano katika kutimiza majukumu yenu mapya mliyokasimiwa kisheria. Aidha, nawakumbusha jukumu kubwa la kuongeza mapato na kuchangia katika mfuko wa serikali”. Alisema Bw. Mbuttuka

Aliendelea kusisitiza kuwa, ujuzi uliopatikana utumike vizuri ili kusimamia vizuri zaidi jukumu jipya la udhibiti ambalo ni la kisheria pamoja na kuboresha majukumu ambayo TMA ilikuwa nayo kabla ya kuwa Mamlaka.
“Nipende kurudia tena kuwa, pale mtakapohitaji ushauri kutoka Ofisi ya Msajili wa Hazina msisite kuja kwani lengo letu ni pamoja na kujenga Tanzania ya viwanda na kukuza uchumi wetu ili kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 ambapo TMA ina mchango mkubwa”. Alisisitiza Msajili wa Hazina.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) Dkt. Agnes Kijazi alisema kuwa mafunzo yameongeza morali ya kuendelea kuboresha huduma za hali ya hewa hapa nchini ili kukidhi mahitaji ya wadau kote nchini na pia yametoa uelewa wa kutosha katika eneo la kudhibiti na kuongeza mapato.
“Napenda nikuahidi mheshimiwa mgeni rasmi kwamba tutayaweka mafunzo haya katika matendo na kuisimamia vyema sheria iliyoanzisha TMA ili kuhakikisha wote wanaotumia huduma za hali ya hewa kibiashara wanachangia huduma hizo”.Alieleza Dkt. Kijazi
Aliendelea kufafanua mafunzo yaliyofanyika yameongeza uelewa kwa Menejiment ya Mamlaka ya Hali ya Hewa kuhusu jukumu jipya walilopatiwa la kudhibiti huduma za hali ya hewa hapa nchini.
Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Mafunzo kwa Njia ya Mtandao (TaGLA), Ndugu, Charles Senkondo alifurahishwa na jinsi washiriki hao ambao ni viongozi kutoka TMA walivyoonesha kunufaika na mafunzo hayo ambapo ndiyo dhumuni la TaGLA kusikia hivyo na si vinginevyo.
Awali, Mwezeshaji kutoka Wakala wa Mafunzo kwa Njia ya Mtandao (TaGLA) Ndugu, Felix Ngamlagosi alieleza namna washiriki hao walivyoonesha dhamira (commitment) na ushirikiano wa hali ya juu katika kuhakikisha wanafikia lengo la mafunzo hayo
Mafunzo hayo ya siku tano yaliandaliwa na TMA kwa kushirikiana na TaGLA, yamejumuisha viongozi kutoka katika ofisi za TMA zilizoko kwenye kanda nane za Mamlaka ikiwa pamoja na Ofisi ya Zanzibar.


No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...