Friday, September 2, 2016
Wednesday, August 31, 2016
CHUO CHA HALI YA HEWA KIGOMA CHA SHEREHEKEA MAHAFALI YA NNE YA KOZI YA 'AERONAUTICAL METEOROLOGY' YALIYOFANYIKA UBUNGO PLAZA, TMA TAREHE 26 AGOSTI 2016
| Mgeni rasmi na Mkurugenzi Mkuu TMA akigawa cheti kwa mmoja wa wahitimu |
| Mgeni rasmi na Mkurugenzi Mkuu TMA akigawa cheti na zawadi kwa mhitimu aliyefanya vizuri zaidi katika kozi hiyo |
| Kaimu Mkuu wa Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma Bw. Peter Mlonganile akitoa hotuba yake katika mahafali |
| Kiongozi wa wahitimu akisoma risala kwa mgeni rasmi kwa niaba ya wahitimu wengine |
Monday, August 22, 2016
KUPATWA KWA JUA TAREHE 01 SEPTEMBA, 2016
Hali
ya kupatwa kwa jua ni tukio la aina yake linatokea pale ambapo miali ya jua
hupungua hadi kutoonekana tena na kusababisha sehemu ya uso wa dunia kuwa giza
wakati wa mchana. Muda wa kufunikwa kabisa ni dakika chache tu katika eneo husika.
Kupatwa
kwa jua kunatokea wakati dunia, mwezi na jua vinapokaa kwenye mstari mmoja
mnyoofu wakati mwezi unakuwa kati ya dunia na jua. Hali hiyo inapotokea
kunajengeka kivuli cha mwezi kwenye uso wa dunia. Kivuli hicho hufunika
sehemu tu ya uso wa dunia. Kutokana na hali hiyo kupatwa
kwa jua kwa maeneo yaliyo mengi kunaonekana kwa watu wengi kama kupungua kwa
mwanga wa jua.
2.Maelezo ya Kisayansi
Wanasayansi
wanaelezea kupatwa kwa jua kama tukio linalotokea na kuonekana katika namna
tofauti tofauti mfano; ni kupatwa kwa
jua kikamilifu hali ambayo hutokea pale miali ya jua inapotea kabisa katika
eneo husika kwa kipindi kifupi. Hali hii inapotokea eneo husika linakosa kabisa
mwanga wa jua na kuwa giza.
Aina ya
pili ni kupatwa kwa jua kisehemu; hii hutokea wakati eneo kubwa linapopata upungufu
wa mwanga wa jua hali ambayo hupungua kadiri mtu anavyokuwa mbali na kitovu cha
mstari wa kupatwa kwa jua. Kiwango cha upungufu wa mwanga wa jua hutegemea
umbali mtu alipo kutoka kwenye kitovu cha kivuli kamili.
Aina
nyingine ni kupatwa kwa jua kipete;
hali hii inapotokea mwezi huzuia mwanga wa jua kufika kwenye dunia kwa vile huweka
duara la kivuli cha mwezi kwenye dunia na hivyo mwanga wa jua huonekana kama pete. Inatarajiwa kuwa aina
hii ya kupatwa kwa jua ndiyo itakayojitokeza
tarehe 1 Septemba 2016 katika baadhi ya maeneo ya Bara la Afrika. Kwa
hapa nchini hali hiyo inatarajiwa kujitokeza katika sehemu kubwa ya maeneo ya mikoa
ya Nyanda za juu kusini magharibi na maeneo ya kusini mwa nchi. Hata hivyo,
watu katika maeneo mengine ya nchi yaliyokaribu na ukanda huo wanatarajiwa kuona kupatwa kwa jua kisehemu yaani upungufu wa
mwanga wa jua kwa dakika kadhaa, imetabiriwa takriban kakika tatu (3). Jua linatarajiwa kupatwa wakati wa asubuhi
kati ya saa tatu asubuhi na saa sita.
3. Athari zake kwa Hali ya Hewa.
Kwa
ujumla hakuna athari zozote kubwa zinazotarajiwa kutokana na hali hiyo. Hata hivyo, upo uwezekano wa kupungua kwa
viwango vya joto katika maeneo ambapo kupatwa kwa jua Kipete kutajitokeza. Kwa kuwa tukio hilo la kupatwa kwa jua
huchukua muda wa dakika chache tu hali ya joto itapungua kwa haraka katika
kipindi kifupi na baadae kuongezeka kurudi katika hali yake ya kawaida. Viwango
vya kupungua kwa joto vitatofautiana kulingana na umbali kutoka eneo la kupatwa
kwa jua
4. Upekee wa tukio la kupatwa kwa jua
Tukio
hili hutokea au kujirudia mara chache sana katika eneo husika. Inakadiriwa kuwa
inaweza kuchukua kati ya miaka 350 hadi 400 kwa hali hiyo kujitokeza tena
katika eneo litakapotokea mwaka huu 2016. Hii ndio sababu kwa watu wa eneo
husika na wanasayansi hili ni tukio la
muhimu na kumbukumbu muhimu ya maisha.
Mamlaka ya hali ya hewa inaendelea
kufuatilia na itatoa taarifa za mabadiliko yoyote yanayoweza kujitokeza katika
hali ya hewa kulingana na tukio hili la kupatwa kwa jua.
Dk. Agnes L. Kijazi
MKURUGENZI MKUU
Wednesday, August 17, 2016
Friday, August 12, 2016
CLIMATE AND HEALTH WORKSHOP, RAMADA HOTEL RESORT,10 TO12 AUGUST 2016
| Participants of Climate and Health Workshop in a group photo aligned with he guest of honor Prof Suzan Nchimi Msola during an opening ceremony which took place on 10th August 2016 in Dar es Salaam. |
| Representative from NOAA Dr. Wasilla Thaiw adressing the audience during an opening ceremony which took place on 10th August 2016 in Dar es Salaam. |
| Workshop participants during an opening ceremony which took place on 10th August 2016 in Dar es Salaam. |
| Add caption |
| Dr. Ladisalus Chang'a TMA Director of Researh and Applied adressing the audience on behalf of TMA Director General during an opening ceremony which took place on 10th August 2016 in Dar es Salaam. |
| Workshop participants |
WADAU MBALIMBALI WAKUTANA KUJADILI UMUHIMU WA MATUMIZI YA TAARIFA ZA HALI YA HEWA KATIKA SEKTA YA AFYA
Mamlaka ya Hali ya Hali ya Hewa Tanzania TMA, wizara
ya afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto na Taasis ya kusimamia Anga
na Bahari kutoka Marekani (NOAA) wameandaa warsha ya siku tatu kuanzia tarehe
10 mpaka 12 Agosti 2016 yenye lengo la kuwakutanisha wadau mbalimbali katika
sekta ya hali ya hewa na sekta ya afya
ili kujadili changamoto zitokanazo na hali ya hewa zinazokabili sekkta ya afya.
Akifungua warsha hiyo katika ukumbi wa Ramada kwa
niaba ya mwenyekiti wa bodi ya ushauri ya TMA ambaye pia ni mjumbe wa Bodi
Prof. Msola alizungumzia umuhimu wa kukaa na wadau husika ili kuweza kusikia
mahitaji yao kwa maendeleo ya nchi na ulimwenguni kwa ujumla, ikizingatiwa
kwamba ulimwenguni kote kumekuwa na changamoto ya mabadiliko ya hali ya hewa
hivyo ni muhimu kutambua maeneo mahususi ya kutiliwa mkazo.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu kutoka TMA Dkt. Ladislaus Changa
alishukuru kwa niaba ya TMA na Serikali ya Tanzania kwa kupata hiyo nafasi ya kukutana na wadau
kupitia ufadhili wa NOAA na kuahidi ushirikiano mkubwa kati ya TMA na Wizara ya
afya,Maendeleo ya jamii, wazee, jinsia na watoto sambamba na taasisi zingine
zinazoshughulikia masuala ya afya, ushirikiano huo utasaidia uboreshaji wa
huduma zitolewazo za hali ya hewa kwa sekta ya afya.
Mwakilishi kutoka NOAA Dkt.Wassila Thaw alielezea
umuhimu wa wao kufadhili na kushiriki ni pamoja na kuhakikisha maazimio yote ya
warsha hii yanatafutia ufumbuzi kwa vile moja ya majukumu ya NOAA ni pamoja na
kuhakikisha taarifa za hali ya hewa zinatumika katika sekta za afya kwa matokea
chanya.
Warsha hii imejumuisha wadau kutoka Ofisi ya Makamu wa
Rais Mazingira, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto, Wizara
ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano,Wizara ya Kilimo na Mifugo, IRI,ICPAC
Kenya,NOAA, IRI, NASA, Chuo Kikuu Chicago kutoka Marekani, Taasisi ya Hali ya
Hewa Ethiopia, Madagascar,Kenya, Uganda,Mozambique, Wizara za Afya Kenya,
Ethiopia, Uganda, WMO, WHO pamoja na
Chuo Kikuu Muhimbili.
IMETOLEWA NA MONICA
MUTONI, AFISA UHUSIANO MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Featured Post
DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.
Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...
-
Dar es Salaam, Tarehe 05/02/2026; Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa rasmi utabiri wa msimu wa mvua za Masika 202 6 kwa maeneo...
-
DODOMA; Tarehe 19 Agosti, 2024; Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imekutana na wadau kutoka sekta mbalimbali nchini ili kujipanga na...
-
Dar es Salaam, 22 /0 8 /202 4 ; Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa utabiri wa msimu wa mvua za VULI 202 4 kwa maeneo yanayopat...
