Wednesday, November 19, 2014

TMA CALLS FOR TANZANIA SCIENTISTS TO PARTICIPATE ON CLIMATE CHANGE RELATED RESEARCH AND IN IPCC PROCESS.




Picture: Guest of Honour Eng. James Ngeleja (  2nd from left) on behalf of the Chairperson of TMA Ministerial Advisory Board, TMA-Director General Dr. Agnes Kijazi,  (3rd  from Left) on a group photo with workshop participants on the Workshop on the latest findings of IPCC (IPCC AR5) held on 18th November 2014, Blue Pearl Hotel.

Tanzania Meteorological Agency (TMA) held a sensitization workshop on the latest Iintergovernmental Panel on Climate Change (IPCC) findings (IPCC fifth assessment report), on 18th November 2014, at Blue Pearl hotel, Dar es Salaam. When officiating the opening of the workshop, the guest of Honour Eng. James Ngeleja, who represented the chairman of the Ministerial Advisory Board of Tanzania Meteorological Agency Mr. Morisson Mlaki called for scientists in Tanzania to actively participate on climate change related research and IPCC process. On his speech he noted the low participation of Africa scientists in the IPCC Process, and the low number of scientific research on climate change in peer reviewed journals.  I am aware that we have a large research gaps in many thematic areas including in climate change and marine ecosystem, climate change and Agriculture, climate change and Health, and climate change and livelihoods. More studies need to be conducted focusing on climate change attributions in the respective thematic areas. I therefore pose a challenge to all scientists present here today to come up with recommendations that will ensure enhanced participation of our scientists in the IPCC process, and enhance involvement of Tanzanian scientists in climate change related research. This endeavor will in turn contribute to the next IPCC Assessment cycle (Sixth Assessment Report, AR6)’. Said Mr. Morisson Mlaki in his speech.
Dr. Agnes L. Kijazi, the Director General of Tanzania Meteorological Agency and Permanent Representative of the United Republic of Tanzania with the World Meteorological Organization (WMO) welcomed all workshop participants and thanked WMO for supporting the workshop through the GFCS programme. Dr. Kijazi said such workshop is of its kind and the first to be held in Tanzania where scientists and decision makers sat together under the same roof to discuss the findings and the implications of the latest IPCC report (AR5).
           
The Intergovernmental Panel on Climate Change (IPCC) is the leading international body for the assessment of climate change. It was established by the United Nations Environment Programme (UNEP) and the World Meteorological Organization (WMO) in 1988 to provide the world with a clear scientific view on the current state of knowledge in climate change and its potential environmental and socio-economic impacts. The workshop was attended by participant  from higher learning institutions  government ministries and NGO’s that included scientists and decision makers from Commission for science and Technology (COSTECH), Sokoine University of Agriculture (SUA), University of Dar es Salaam (UDSM), University of Dodoma (UDOM), Ardhi University (ARU) Vice President Office (Environment), Ministry of Agriculture and Food Security, Ministry of Health, Tanzania RedCross Society, World Food Programme(WFP), Centre for Weather Climate and Research (CWCAR) Climate Consult, National Environment Management Council (NEMC), Environment Protection and Management Services (EPMS), the Prime Minister – Disaster Management Department.

RELEASED BY: MONICA MUTONI; PUBLIC RELATION OFFICER, TANZANIA METEOROLOGICAL AGENCY

TMA YAWAHAMASISHA WANASAYANSI WA KITANZANIA KUJIKITA KATIKA TAFITI ZA MABADILIKO YA HALI YA HEWA


Picha: Mgeni rasmi Mhandisi James Ngeleja aliyemuwakilisha Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA)(wa pili kutoka kushoto waliokaa ) na Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi (wa tatu kutoka kushoto waliokaa) katika picha ya pamoja na washiriki wa warsha ya kuhamasisha wanasayansi kufanya tafiti za mabadiliko ya hali ya hewa ili kuchangia katika ripoti ya kimataifa(IPCC report), iliyofanyika katika ukumbi wa hotel ya Blue Pearl, Tarehe 18 Novemba 2014.

Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini imeandaa warsha ya kuhamasisha wanasayansi wa kitanzania kufanya utafiti wa mabadiliko ya hali ya hewa ikizingatia matokeo na taarifa za hivi karibuni za Jopo la Kimataifa linaloshughulikia Sayansi ya mabadiliko ya hali ya hewa duniani (IPCC). Warsha hiyo imefanyika katika Hoteli ya Blue Pearl, Dar es Salaam, Tarehe 18 Novemba 2014. Warsha hiyo ilifunguliwa na Mhandisi James Ngeleja ambaye alimwakilisha mwenyekiti  wa Bodi ya Ushauri ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Bw. Morisson Mlaki.  Ushiriki wa watanzania katika tafiti za mabadiliko ya hali ya hewa dunia ni mdogo hivyo naomba kutoa rai kwa wanasayansi wote mliopo hapa na nje ya warsha hii kushiriki katika utafiti hususan katika ripoti ya sita ya IPCC itakayoanza kuandaliwa hapo baadae’alisema Bwana Morisson Mlaki katika hotuba yake.
Aidha, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dkt. Agnes Kijazi aliwakariribisha washiriki wote na kuwashukuru Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) kwa kufadhili warsha hiyo kupitia programu ya GFCS. ‘napenda kuchukua fursa hii kuwakaribisha wote mliohudhuria warsha hii, aidha nawasihi taasis za elimu ya juu hapa nchini kuwahimiza wanasayansi kufanya tafiti katika mabadiliko ya hali ya hewa ili taarifa za mabadiliko ya hali ya hewa kwa nchi yetu na Afrika kwa ujumla ziweze kuingia katika ripoti ya IPCC’ alisema Dkt.Kijazi.
Jopo la Kimataifa linaloshughulikia Sayansi ya mabadiliko ya Hali ya Hewa Duniani  (IPCC) ni chombo cha kimataifa kilichoundwa ili kutathimini mabadiliko ya hali ya hewa duniani. Warsha hiyo ilikuwa na washiriki kutoka COSTECH, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu Dodoma (UDOM) chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA),Chuo Kikuu cha Ardhi (ARU), wasomi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira, Ofisi ya Waziri Mkuu,-Kitengo cha Maafa, Wizara ya Kilimo na Usalama wa Chakula, World Food Programme (WFP),Kituo cha Utafiti wa Masuala ya hali ya hewa (CWCAR), Climate Consult, Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Chama cha Msalaba mwekundu (RedCross) na taasisi mbalimbali za mazingira. 
Imetolewa na : Monica Mutoni, Ofisi ya Uhusiano- Mamlaka ya Hali ya Hewa





Tuesday, November 18, 2014

TMA DIRECTOR GENERAL OFFICIATED 2ND AERONAUTICAL METEOROLOGY TRAINING

Dr. Agnes Kijazi, Director General of TMA gave her remarks during 2nd Aeronautical Meteorology Training opening ceremony held at TMA Headquarter, Ubungo Plaza-Dar es Salaam.

Training participants during 2nd Aeronautical Meteorology Training opening ceremony held at TMA Headquarter, Ubungo Plaza-Dar es Salaam.
Guest of Honour, Director General of TMA Dr. Kijazi and Director of Support Services (1st from right with black suit) on a group photo during 2nd Aeronautical Meteorology Training opening ceremony held at TMA Headquarter, Ubungo Plaza-Dar es Salaam from 15th -30th November 2014.

Wednesday, November 12, 2014

Rais Kikwete katika Mkutano wa Jinsia wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO)

Mkutano wa Jinsia kuhusu huduma za hali ya hewa ulioandaliwa na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) ulifanyika Geneva Uswis kuanzia  tarehe 5-7 Novemba 2014. Mkutano uliazimia mambo mbalimbali ikiwa pamoja na jinsi ya kuhakikisha wanawake wanajiunga kwa wingi katika fani ya sayansi ya hali ya hewa na maji. Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania alialikwa kutoa hotuba katika ufunguzi wa mkutano huo.
Katika hotuba yake ambayo imenukuliwa katika hadidu za mkutano Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete alisema upo uhusiano wa wazi kabisa kati ya athari za mabadiliko ya hali ya hewa na usawa wa kijinsia. Alisema,  wanawake wanaoishi katika maeneo ya vijijini ndio ambao kwa kiwango kikubwa wanakumbwa na athari za mabadiliko ya hali ya hewa. Hii ni kutokana na ukweli kwamba wanakabiliwa na changamoto zinazotokana na mazingira au mila ambazo zinawazuia kuwa na uwezo wa kumiliki rasilimali na pia kuwanyimwa haki na sauti ya kushiriki katika kutoa maamuzi mbalimbali. “Ni muhimu masuala ya jinsia yakajumuishwa na kupewa kipaumbele katika huduma za hali ya hewa ili kuhakikisha kwamba wanawake  wanakuwa na sauti katika kutoa maamuzi ya hatua zinazopaswa kuchukuliwa katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya hali ya hewa” ilieleza hotuba hiyo ya mheshimiwa Rais.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Shirika la hali ya Hewa Duniani (WMO), Bwana Michael Jarraud alisema kwa kiasi kikubwa Shirika la Hali ya Hewa Duniani limepata mafanikio kwa kuongeza utoaji wa huduma zenye mtazamo wa kijinsia kwa wakati na kwa ufanisi. “Hilo limewezekana kwa kupitia dhamira ya WMO ya kuzingatia mahitaji maalum ya wanawake na wanaume, pia ushirikishwaji wa wanawake na wanaume katika kuandaa na kubuni huduma mbalimbali kwa  kuzingatia usawa wa kijinsia”. Aliongeza Bwana Jarraud. Katika hotuba yake ya kufunga mkutano huo, Katibu Mkuu huyo wa WMO alitoa pongezi maalum kwa Bara la Afrika kwa kuongoza Duniani katika kuteua wanawake kuwa wakuu wa Taasisi za Hali ya Hewa. Mpaka sasa  kuna takribani jumla ya nchi sita za Afrika ikiwemo Tanzania ambazo wakuu wa Taasisi za Hali ya Hewa ni wanawakwe.
“ Athari za mabadiliko ya hali ya hewa zinawapata wanawake na wanaume kwa wakati mmoja ingawa wanaoathirika zaidi ni wanawake kutokana na kukosa elimu ya namna ya kujikinga”, alisema  Dkt. Elena Manaenkova, Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Shirika la hali ya Hewa Duniani (WMO). Bi. Elena Manaekova aliongeza kuwa, wanawake na wanaume wanahitaji kuwa na haki sawa katika kupata ujuzi wa namna ya kutumia taarifa za hali ya hewa, hivyo kuwawezesha wanawake ni muhimu ili kuwajengea uwezo katika kukabiliana na na athari zinazotokana na mabadiliko ya hali ya hewa.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na mwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) Dkt. Agnes Kijazi alisema kuna haja ya kuwatia moyo wasichana wenye ndoto za kuwa wanasayansi mahiri wa baadae ili waweze  kutimiza ndoto zao na kufikia malengo waliyojiwekea.  “Vijana wa kike wanahitaji kukataa kukatishwa tamaa bali waangalie wanawake ambao wamepata mafanikio katika sayansi na kufuata mifano yao” aliongeza Bi. Agnes Kijazi akizungumza katika mkutano huo.
“Sekta ya Afya inatakiwa kuwa mstari wa mbele katika kueleza huduma wanazohitaji kutoka Taasisi za hali ya hewa ili kuziwezesha Taasisi hizo kutoa huduma zinazokidhi mahitaji ya watumiaji. Aidha, Taasisi  za hali ya hewa zinapaswa kuanzisha mfumo mahususi wa usambazaji wa taarifa za hali ya hewa ili ziwafikie walengwa kwa wakati” alisema Bi. Hellen Msemo mwanasayansi  kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa  wakati akitoa mada katika Mkutano huo.
Mkutano huo  ulitoa mapendekezo mbalimbali ikiwa pamoja na kuwaongezea uwezo wanawake ili waweze kupata na kuzitumia taarifa za hali ya hewa, kuhamasisha Taasisi za Hali ya Hewa Duniani kuandaa mikakati ya mafunzo na kampeni zinazolenga kuhamasisha wanawake kusoma masomo ya sayansi ili kujiunga katika fani ya hali ya hewa na kuboresha njia za usambazaji wa taarifa za hali ya hewa ili taarifa hizo ziwafikie wanawake wengi. Aidha Taasis za Hali ya Hewa zimetakiwa kuhakikisha taarifa zinatolewa katika lugha nyepesi ya kueleweka kwa wanawake na wanaume.

Imetolewa na : Monica Mutoni Afisa Mahusiano wa TMA.

Sunday, November 2, 2014

TMA TAKES PART ON 40TH SESSION OF THE INTERNATIONAL PANEL ON CLIMATE CHANGE (IPCC) IN COPENHAGEN, DENMARK



Picture 1: TMA Director General,Dr Agnes Kijazi and Director of Research and Applied Meteorology, Dr. Ladislaus Chang’a during the 40th Session of the International Panel on Climate Change (IPCC)    Session held in Copenhagen, Denmark from 27 to 31 October 2014.



Picture 2: TMA Director General, Dr Agnes Kijazi and the World Meteorological Organization (WMO) Deputy Secretary General, Mr. Jeremiah Lengoasa exchanging some ideas during the 40th Session of the International Panel on Climate Change (IPCC) Session held in Copenhagen, Denmark from 27 to 31 October 2014.

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...