Thursday, November 7, 2019

USAFIRI WA ANGA: TMA YAZIDI KUBORESHA HUDUMA ZA HALI YA HEWA.

Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi akifafanua jambo katika mkutano wa wadau wa huduma za hali ya hewa katika sekta ya usafiri wa anga uliyofanyika katika ukumbi wa TB II, JNIA - Dar es salaam, Tarehe 07/11/2019 

Mkurugenzi wa huduma za utabiri TMA, Dk. Hamza Kabelwa  akielezea lengo la kufanyika kwa mkutano  wa wadau wa huduma za hali ya hewa katika sekta ya usafiri wa anga, uliyofanyika katika ukumbi wa TB II, JNIA - Dar es salaam, Tarehe 07/11/2019.





Wataalamu kutoka TMA wakiwasilisha mada mbalimbali katika mkutano wa wadau wa huduma za hali ya hewa katika sekta ya usafiri wa anga uliyofanyika katika ukumbi wa TB II, JNIA - Dar es salaam, Tarehe 07/11/2019 .




Baadhi ya washiriki wakichangia mada katika mkutano wa wadau wa huduma za hali ya hewa katika sekta ya usafiri wa anga uliyofanyika katika ukumbi wa TB II, JNIA - Dar es salaam, Tarehe 07/11/2019.
Mkurugenzi mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano wa wadau wa huduma za hali ya hewa katika sekta ya usafiri wa anga uliyofanyika katika ukumbi wa TB II, JNIA - Dar es salaam, Tarehe 07/11/2019.


Dar es Salaam, Tarehe 07/11/2019: Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imekutana na wadau wa huduma za hali ya hewa katika sekta ya usafiri wa anga ili kupata mrejesho wa wadau na maoni yao katika kuendeleza uboreshaji wa huduma hizo kitaifa na kimataifa.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo, Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa WMO, Dkt. Agnes Kijazi alielezea jinsi TMA ilivyopiga hatua katika sehemu ya miundombinu ikiwa ni pamoja na kusimikwa kwa rada za hali ya hewa, kununuliwa vifaa vya kuhakiki ubora wa vifaa vya hali ya hewa na kubadilishwa kwa vifaa vinavyotumia zebaki. Aidha, aliongeza kusema uboreshaji huo ni pamoja na kuendelea kumiliki cheti cha ubora wa kimataifa (ISO 9001:2015), kuboreshwa kwa mfumo wa usambazaji wa taarifa za hali ya hewa na kuwajengea uwezo (competence) wataalam, hivyo kuchangia katika maboresho endelevu yanayoendelea katika Mamlaka katika utoaji huduma.

“TMA inatambua sana mchango wa wadau katika kuboresha huduma za hali ya hewa hususani kupitia maoni yanayotufikia kupitia njia mbalimbali, hivyo basi napenda kuwajulisha kwamba TMA imeendelea kupiga hatua chanya ikiwa ni pamoja na uboreshaji wa miundombinu, kumiliki cheti cha ubora cha kimataifa, kuboreshwa kwa mfumo wa usambazaji na kuhakikisha wataalam  wa TMA  wana weledi na maarifa ya kutosha katika kutoa huduma za hali ya hewa kwenye sekta ya usafiri wa anga”. Alisema Dkt. Kijazi

Aidha, wadau walipata fursa ya kupata mrejesho wa namna maoni yao yalivyofanyiwa kazi pamoja na kupata elimu juu ya matumizi na maboresho ya mfumo wa usambazaji taarifa za hali za hewa kwa wadau wa usafiri wa anga (MAIS) ambao ulibuniwa na wataalam wa TMA na kuzinduliwa rasmi na Mheshiwa Isack Kamwele, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Wadau waliendelea kusisitizwa umuhimu wa huduma za hali ya hewa  katika shughuli zao hususan sekta ya usafiri wa anga. 

Naye mmoja wa wadau kutoka Rwanda Air Bi. Umulisa Alice wakati wa mkutano huo alisema kuwa ni jambo jema TMA imefanya kukutana na wadau na kuahidi kutoa ushirikiano wa namna ya kupata maoni zaidi kutoka kwa marubani wa ndege hiyo ili kuongeza ufanisi wa huduma za Mamlaka.

Kwa kuzingatia umuhimu wa taarifa za hali ya hewa katika sekta ya usafiri wa anga na kwamba ndege haziwezi kuruka, kutua na hata kusafiri angani bila taarifa za hali ya hewa na kwa kutambua umuhimu wa sekta ya usafiri wa anga katika ukuaji wa uchumi wa taifa letu, TMA imejiwekea malengo ya kuboresha huduma zake inazotoa katika sekta ya usafiri wa anga ili kutoa mchango chanya katika Azma ya Mheshimiwa Rais ya kufikia uchumi wa kati ifikapo 2025. Katika kuhakikisha malengo ya kuwa karibu na wateja na kutoa huduma zinazokidhi matakwa ya wateja katika sekta ya usafiri wa anga, TMA imejiwekea utaratibu wa kukutana na wadau hao ana kwa ana na kujadili masuala mbalimbali ya kuboresha huduma kwa mustakabali wa maendeleo ya sekta hiyo na Taifa kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...