Wednesday, October 16, 2019

MHESHIMIWA ISSA HAJI USSI GAVU AITAKA TMA KUONGEZA MBINU ZA KUFIKISHA TAARIFA ZA HALI YA HEWA KWA WAKULIMA KWA WAKATI.

Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Baraza la Mapinduzi Zanzibar Mhe. Issa Haji Ussi Gavu akipata elimu kutoka kwa mtaalamu wa hali ya hewa ya namna taarifa za hali ya hewa zinavyoweza kusaidia kukuza sekta ya kilimo hapa nchini kupitia maonesho ya siku ya chakula duniani yanayofanyika katika viwanja vya Chamanangwe kisiwani Pemba Tarehe 10 hadi 16 Oktoba 2019.
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Baraza la Mapinduzi Zanzibar Mhe. Issa Haji Ussi Gavu akitoa maelekezo mara baada ya kupata elimu kutoka kwa mtaalamu wa hali ya hewa kupitia maonesho ya siku ya chakula duniani yanayofanyika katika viwanja vya Chamanangwe kisiwani Pemba Tarehe 10 hadi 16 Oktoba 2019.
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Baraza la Mapinduzi Zanzibar Mhe. Issa Haji Ussi Gavu akipokea zawadi toka kwa meneja wa hali ya hewa kituo cha Pemba Bi. Bishara Mdowe kupitia maonesho ya siku ya chakula duniani yanayofanyika katika viwanja vya Chamanangwe kisiwani Pemba Tarehe 10 hadi 16 Oktoba 2019


Tarehe 14/10/2019 Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Baraza la Mapinduzi Zanzibar Mhe. Issa Haji Ussi Gavu aliwataka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kuongeza mbinu za kufikisha taarifa za hali ya hewa kwa wakulima kwa wakati, alizungumza hayo alipotembelea banda la TMA lililopo kwenye maonesho ya siku ya chakula duniani yanayofanyika katika viwanja vya Chamanangwe kisiwani Pemba Tarehe 10 hadi 16 Oktoba 2019.                                                     
“Ninawataka muongeze mbinu za kuhakikisha taarifa zenu zinawafikia wakulima kwa wakati”  alisisitiza Mhe. Issa 

Aidha, Mheshimiwa Issa ameipongeza TMA kwa juhudi kubwa inayoifanya na kufanikiwa kuongeza usahihi wa taarifa za hali ya hewa hapa nchini. Maonesho hayo yamefungwa rasmi Tarehe 15 Oktoba 2019 na makamu wa pili wa Rais, baraza la mapinduzi Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...