Thursday, January 11, 2024

WANANCHI WAFURAHISHWA NA ELIMU YA HALI YA HEWA, ZANZIBAR.

 








Zanzibar; Tarehe 10/01/2024

Wananchi kutoka maeneo mbalimbali Zanzibar, wamefurahishwa na elimu ya hali ya hewa inayotolewa katika maonesho ya Maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, yanayofanyika katika viwanja vya Maonesho ya Biashara, Nyamanzi, Mjini Magharibi, Zanzibar kuanzia Tarehe 07 - 19 Januari, 2024.

Wageni mbalimbali waliweza kutembelea banda la TMA wakiwemo viongozi wa Taasis za serikali zilizo chini ya Wizara ya Uchukuzi ikiwa ni pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) Prof. Ulingeta Mbamba, Shirika la Reli Tanzania Bw. Masanja Kadogosa, Mkurugenzi wa Huduma za Taasis kutoka Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Bw. Hamidu Mbegu, Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) Bw. Teophoy Mbilinyi ambao waliipongeza TMA kwa huduma nzuri ya usahihi wa Utabiri inayotolewa .

Aidha, wataalam wa hali ya hewa kutoka TMA wameendelea kutoa elimu kwa wadau mbalimbali ili kutumia huduma mahususi zinazotolewa na TMA pamoja na kuelewa namna ya kutumia taarifa za hali ya hewa kwa usahihi ili kukabiliana na athari zitokanazo na hali mbaya ya hewa.


No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...