Thursday, September 12, 2024

MHE. MWIGULU: SERIKALI ITAENDELEA KUIPA KIPAUMBELE TMA

 



12 Septemba 2024, Arusha: Waziri wa Fedha, Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba ameipongeza Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na kuahidi kuwa Serikali kupitia Wizara ya Fedha itaendelea kuipa kipaumbele kwa kuwa huduma za hali ya hewa zinasaidia katika mipango mbalimbali ya maendeleo.

“Wataalam wa hali ya hewa mnafanya kazi nzuri, utabiri unaotolewa hivi sasa ni wa usahihi na umesaidia sana katika masuala ya kiuchumi na kijamii na mipango ya nchi kwa ujumla”. Alizungumza Dkt. Mwigulu alipotembelea banda la TMA katika viwanja vya AICC, Arusha wakati akifunga rasmi Jukwaa la 16 la Ununuzi la Afrika Mashariki. 

Matumizi sahihi ya huduma za hali ya hewa ni suala mtambuka kwani husaidia katika mipango na uendeshaji wa shughuli za kiuchumi na kijamiii hususani katika kupunguza madhara yatokanayo na hali mbaya ya hewa kwa umma

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...