Tuesday, August 9, 2022

TMA YATAKIWA KUONGEZA WIGO WA KUTOA ELIMU KWA JAMII KUHUSU TAARIFA ZA HALI YA HEWA.

Waziri wa Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe.Suleiman Masoud Makame akizungumza alipotembelea banda la TMA, Tarehe 08 Agosti, 2022 kwenye maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Kizimbani, Mjini Unguja kuanzia tarehe 6 hadi 15 Agosti, 2022.

  


Mwakilishi wa Jimbo la Mtambile Pemba Seif Salim Seif   alipotembelea banda la TMA, Tarehe 08 Agosti, 2022 kwenye maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Kizimbani, Mjini Unguja kuanzia tarehe 6 hadi 15 Agosti, 2022. 
                            







Wageni mbalimbali wakiendelea kupata elimu ya hali ya hewa walipotembelea banda la TMA  kwenye maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Kizimbani, Mjini Unguja kuanzia tarehe 6 hadi 15 Agosti, 2022.
                                        
Wafanyakazi wa TMA wakiwa katika picha ya pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa TMA ofisi ya Zanzibar kwenye maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Kizimbani, Mjini Unguja kuanzia tarehe 6 hadi 15 Agosti, 2022.
  

Zanzibar; Tarehe 08 Agosti, 2022;

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imeombwa kuongeza wigo wa kutoa elimu kwa jamii kuhusu taarifa za hali ya hewa kwa makundi mbali mbali hususani wadau ambao wanahusika moja kwa moja ili waweze kusikiliza na kutekezeleza taarifa  zinazotolewa na Mamlaka. Hayo yalizungumzwa na Waziri wa Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe.Suleiman Masoud Makame alipotembelea banda la TMA, Tarehe 08 Agosti, 2022 kwenye maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Kizimbani, Mjini Unguja kuanzia tarehe 6 hadi 15 Agosti, 2022. 

“Mamlaka inatakiwa kuongeza wigo wa kutoa elimu kwa jamii kuhusu taarifa za hali ya hewa kwani tunawatu wasiopungua elfu 37000 wanaokwenda baharini kwa shughuli mbalimbali kila siku hivyo inatupasa tubadilike kidogo kwenye kutoa elimu tutumie wataalamu,wasanii,mikutano mbalimbali,kuwajuza watu kuhusu taarifa za hali ya hewa”. Alisema Mhe. Makame

Wakati akielezea hayo Waziri Makame aliongezea kuwa wananchi pia wanapaswa kuwa tayari kusikiliza taarifa za hali ya hewa na kuzifanyia kazi kwa usalama wao na mali zao kwani majanga mbali mbali yanatokea mara kwa mara, hivyo bila kufuatilia taarifa hizi majanga yanaweza kuongezeka na Serikali pia ipo tayari kuwahimiza wananchi na wadau husika  kutumia taarifa za hali ya hewa ili kupunguza majanga hayo. 

Nao wageni waliotembelea katika Banda la Mamlaka waliiomba TMA kuongeza njia za kuwafikia wakulima wa hali ya chini kabisa ambao hawana uwezo wa kupata taarifa hizi kwa njia zinazotumika ambazo ni televisheni, radio na mitandao ya kijamii, hivyo njia ya kupatata taarifa kupitia meseji za kawaida za simu za mkononi iboreshwe kwaajili ya  kurahisisha upatikanaji wa taarifa hizo.

“Hapo mwanzo tulikuwa tukipata taarifa za hali ya hewa kilimo mara nyingi kupitia meseji kwenye simu bure kabisa sasa hivi hatupati taarifa zile na zile tunazozipata baada ya taarifa ya habari hazilingani na zile za meseji hivyo tunaomba mturahisishie taarifa hizi ilitupate taarifa kwa urahisi”. Alisema Bwana Abdu Abdalla ambae ni mkulima kutoka Zanzibar.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Ofisi ya Mamalaka ya hali ya hewa Zanzibar Bw. Masoud M. Faki alieleza kuwa pamoja na kuwepo njia mbali mbali zinazotumiwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania katika kusambaza taarifa za hali ya hewa inawapasa wananchi pia kufatilia taarifa za hali ya hewa ili waweze kuepukana na majanga na usumbufu unaoweza kujitokeza hasa kipindi hiki tunapoelekea siku ya SENSA ya watu na makazi.

 

 

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...