Friday, August 5, 2022

TMA YAHIMIZWA KUONGEZA JITIHADA ZA KUIFIKISHIA JAMII TAARIFA ZA HALI YA HEWA KWA WAKATI

Mkuu wa Wilaya ya Songea, Mhe. Pololet Kamando Mgema akizungumza mara baada ya kupata elimu ya hali ya hewa alipotembelea banda la TMA, tarehe 5 Agosti 2022 kupitia maonesho ya NaneNane yanayoendelea kufanyika katika viwanja vya John Mwakangale, Uyole - Mbeya kuanzia tarehe 1 hadi 8 Agosti, 2022.

 


Ndg. Isack Yonah, Meneja wa Huduma za Hali ya Hewa Kilimo akitoa elimu ya hali ya hewa kwa Mkuu wa Wilaya ya Songea, Mhe. Pololet Kamando Mgema alipotembelea banda la TMA, tarehe 5 Agosti 2022 kupitia maonesho ya NaneNane yanayoendelea kufanyika katika viwanja vya John Mwakangale, Uyole - Mbeya kuanzia tarehe 1 hadi 8 Agosti, 2022.

Mkuu wa Wilaya ya Songea, Mhe. Pololet Kamando Mgema akisaini katika kitabu cha wageni alipotembelea banda la TMA, tarehe 5 Agosti 2022 kupitia maonesho ya NaneNane yanayoendelea kufanyika katika viwanja vya John Mwakangale, Uyole - Mbeya kuanzia tarehe 1 hadi 8 Agosti, 2022.

Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Mhe. Aziza Mangosongo akisaini katika kitabu cha wageni alipotembelea banda la TMA, tarehe 5 Agosti 2022 kupitia maonesho ya NaneNane yanayoendelea kufanyika katika viwanja vya John Mwakangale, Uyole - Mbeya kuanzia tarehe 1 hadi 8 Agosti, 2022.



Wageni mbalimbali wakipokea zawadi kutoka kwa ndg. Isack Yonah, Meneja wa Huduma za Hali ya Hewa Kilimo, walipotembelea banda la TMA, tarehe 5 Agosti 2022 kupitia maonesho ya NaneNane yanayoendelea kufanyika katika viwanja vya John Mwakangale, Uyole - Mbeya kuanzia tarehe 1 hadi 8 Agosti, 2022.

Ndg. Isack Yonah, Meneja wa Huduma za Hali ya Hewa Kilimo akizungumza na wananchi wa Mbeya kupitia vyombo mbalimbali vya habari katika banda la TMA, tarehe 5 Agosti 2022 kupitia maonesho ya NaneNane yanayoendelea kufanyika katika viwanja vya John Mwakangale, Uyole - Mbeya kuanzia tarehe 1 hadi 8 Agosti, 2022.




Wageni mbalimbali wakiendelea kupata elimu ya hali ya hewa walipotembelea banda la TMA kupitia maonesho ya NaneNane yanayoendelea kufanyika katika viwanja vya John Mwakangale, Uyole - Mbeya kuanzia tarehe 1 hadi 8 Agosti, 2022.


Mbeya; Tarehe 05 Agosti, 2022;

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imehimizwa kuongeza jitihada za kuifikishia jamii  taarifa za hali ya hewa kwa wakati, hayo yalizungumzwa na Mkuu wa Wilaya ya Songea, Mhe. Pololet Kamando Mgema akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe. Kanali Laban Elias Thomas alipotembelea banda la TMA, tarehe 5 Agosti 2022 kupitia maonesho ya NaneNane yanayoendelea kufanyika katika viwanja vya John Mwakangale, Uyole - Mbeya kuanzia tarehe 1 hadi 8 Agosti, 2022.

“Kazi yenu inajitangaza kwa kuwa mmekuwa mnafanya vizuri katika utabiri wenu wa msimu hivyo nawapongeza sana, lakini niwahimize kuongeza jitihada za kuwafikishia jamii taarifa hizo za hali ya hewa kwa wakati ziweze kutumika na kuwasaidia kwa wakati. Alisisitiza Mhe. Pololet Mgema.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Mhe. Aziza Mangosongo akiongozana na Mhe. Pololet Mgema aliongezea kwa kuipongeza TMA kwa utabiri mzuri wanaoutoa na kufanya wananchi kuwa na imani na taarifa za hali ya hewa kwa kuzitumia katika shughuli zao za kiuchumi na kijamii.

Aidha, akielezea namna TMA ilivyoboresha utabiri wa hali ya hewa katika ngazi ya wilaya kupitia vyombo vya habari, Ndg. Isack Yonah, Meneja wa Huduma za Hali ya Hewa Kilimo alisema, Sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, Namba 2 ya mwaka 2019 imeipa Mamlaka jukumu la kutoa huduma, kudhibiti na kuratibu shughuli za hali ya hewa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na tayari imeshaboresha vifaa na mitambo ya hali ya hewa inayotumia teknolojia ya kisasa inayosaidia upatikanaji wa taarifa za hali ya hewa zilizo sahihi zinazokusanywa katika vituo vya hali ya hewa ikiwemo kituo cha hali ya hewa kinachojiendesha chenyewe (Automatic Weather Station-AWS) ambacho kimeletwa kwenye maonesho hayo.

Ndg. Isack Yonah aliongezea kuwa katika uboreshaji wa huduma za hali ya hewa, TMA inatoa utabiri wa hali ya hewa hadi ngazi ya wilaya na hata kama ikitokea mkulima au mdau yeyote atahitaji kujua hali ya hewa ya eneo lake anaweza kuandaliwa taarifa mahususi kulingana na mahitaji yake kwa kuchangia huduma hiyo ili kufanya huduma hizo ziendelee kuwa endelevu. 


No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...