Tuesday, September 14, 2021

DKT. KIJAZI AELEZA FAIDA KWA NCHI WANACHAMA WA WMO KANDA YA AFRIKA

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), Dkt. Agnes Kijazi akiwasilisha mada kuhusiana na faida za mabadiliko ya kimuundo na majukumu ya kanda za WMO kwa Nchi za kanda ya Afrika. Aliwasilisha mada hiyo tarehe 23 Agost, 2021 katika mkutano wa 18 wa Nchi Wanacahma wa WMO kanda ya Afrika awamu ya pili “Eighteenth Session of WMO Regional Association 1-phase II (RA I – 18(II))”. Kulia kwake ni Meneja wa Mashirikiano ya Hali ya Hewa Kikanda na Kimataifa, Bw. Wilbert Muruke akimsaidia Mkurugenzi Mkuu Dr. Kijazi

 

Mkurugenzi wa Huduma za utabiri katika TMA, Dkt. Hamza Kabelwa aliwasilisha mwongozo wa WMO wa uchakataji wa data na utabiri “Manual on the Global Data Processing and Forecasting System (GDPFS)”katika mkutano wa 18 wa Nchi Wanacahma wa WMO kanda ya Afrika awamu ya pili “Eighteenth Session of WMO Regional Association 1-phase II (RA I – 18(II))”,terehe 24 Agosti, 2021


Mkurugenzi wa Huduma za utabiri katika TMA, Dkt. Hamza Kabelwa aliwasilisha mwongozo wa WMO wa uchakataji wa data na utabiri “Manual on the Global Data Processing and Forecasting System (GDPFS)” katika mkutano wa 18 wa Nchi Wanacahma wa WMO kanda ya Afrika awamu ya pili “Eighteenth Session of WMO Regional Association 1-phase II (RA I – 18(II))”,terehe 24 Agosti, 2021.

 

Dar es Salaam; Tarehe 23/08/2021

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), Dkt. Agnes Kijazi, ameeleza faida zitakazopatikana kwa  Nchi Wanachama wa WMO kanda ya Afrika“WMO Regional Association I – Africa (RA I)”kutokana na uboreshaji wa muundo na majukumu ya kanda za WMO unaotekelezwa na Shirika hilo. 

Dkt. Kijazi alieleza hayo tarehe 23 Agosti, 2021 katika mkutano wa 18 wa Nchi Wanachama wa WMO kanda ya Afrika awamu ya pili “Eighteenth Session of WMO Regional Association 1-phase II (RA I – 18(II))”,uliofanyika kwa njia ya mtandao kuanzia tarehe 23 hadi 26 Agosti, 2021. Dkt. Kijazi ambaye ni Mwenyekiti wa Kikosi kazi cha WMO cha kufanya mapitio ya muundo na majukumu ya kanda za WMO “(Executive Council Task Force to lead the Comprehensive Review of the WMO Regional Concept and Approaches)”, alieleza faida hizo alipowasilisha mada kuhusiana na namna Nchi Wanachama wa WMO kanda ya Afrika zitakavyofaidika na maboreho hayo, ambapo mada hiyo ililenga kutoa uelewa kuhusiana na manufaa ya maboresho hayo kwa kanda ya Afrika. 

Akiwasilisha mada hiyo, Dkt. Kijazi, alisema miongoni mwa faida zitakapatikana kwa Nchi za kanda ya Afrika ni pamoja na kuimarishwa kwa njia za kuibua na kushughulikia  vipaumbele vya kanda ya Afrika, ambapo vipaumbele hivyo vitaibuliwa kupitia mfumo maalumu wa WMO (WMO Community Platform). Aidha, maboresho hayo yanatoa fursa kwa viongozi na wataalamu katika kandakujielekeza zaidi katika kujadili na kutoa mapendekezo stahiki ya kutatua changamoto za Nchi Wanachama katika kanda husika. Maboresho hayo pia yataweka mfumo bora wa kuratibu utekelezaji wa maamuzi ya WMO, kwa kuweka utaratibu wa kupima utendaji kazi na utekelezaji wa maamuzi hayo.

Faida zingine ni kuimarika zaidi  kwa ushirikiano baina ya Taasisi za Hali ya Hewa, taasisi za maji, sekta binafsi,  taasisi za elimu ya juu na mashirika ya Umoja wa Mataifa; Kuimarika na kuongezeka kwa fursa za mashirikiano baina ya Nchi au maeneo yanayohusiana katika kanda; na uboreshwaji wa vituo vya huduma za hali ya hewa vya kikanda (Regional Specialized Meteorological Centres-RSMC) katika kuzijengea uwezo zaidi Nchi Wanachama katika Kanda. 

Faida hizo alizoeleza ni sehemu ya mapendekezo ya jopo analoliongoza yatakayowasilishwa na kutolewa maamuzi katika Mkutano Mkuu wa WMO “Extra-Ordinary Meteorological Congress (2021)”unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu. Mapendekezo hayo yanajumuisha pia majukumu ya Nchi Wanachama katika kanda husika, pamoja na majukumu ya viongozi waandamizi katika kanda. Maboresho hayo ya muundo na majukumu ya kanda za WMO ni mwendelezo wa mabadiliko ya kimfumo yanayotekelezwa na WMO ili kuboresha zaidi huduma za hali ya hewa kwa Nchi Wanachama.

Sambamba na faida zilizoainishwa, mkutano huo pia ulijadili mada mbalimbali, ikiwa ni pamoja na masuala ya uboreshaji wa miundombinu ya hali ya hewa, utafiti na huduma za hali ya hewa barani Afrika. Katika eneo la miundombinu, Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri wa TMA, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya WMO inayoshughulikia uchakataji wa data na utabiri wa hali ya hewa “Standing Committee on Data Processing for Applied Earth System Modeling and Prediction (SC-ESMP)”,Dkt. Hamza Kabelwa aliwasilisha mada kuhusu mwongozo wa WMO wa uchakataji wa data na utabiri “Manual on the Global Data Processing and Forecasting System (GDPFS)”. Aidha,Mkurugenzi wa Miundombinu na Huduma za Ufundi wa TMA, Dkt. Pascal Waniha alichangia katika mkutabno huo na kushauri Nchi za kanda ya Afrika kuuhuisha mpango wa kuwa na satelaiti ya hali ya hewa ya Afrika itakayosaidia kuboresha upatikanaji wa data za hali ya hewa na hatimaye kuboresha zaidi huduma za hali ya hewa barani Afrika.

 

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...