Tuesday, January 28, 2020

TMA YAISHUKURU TAASISI YA EUMETSAT KWA USHIRIKIANO WA KUWAKUTANISHA WATAALAMU KUTOKA SEKTA MBALIMBALI PAMOJA NA WIZARA KUPITIA MKUTANO WA WADAU WA MAANDALIZI KUELEKEA MKUTANO MKUBWA WA KUMI NA NNE (14) WA WADAU WA HUDUMA ZA SETILAITI BARANI AFRIKA, “14th EUMETSAT User Forum in Africa”

Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania(TMA), Dkt. Hamza Kabelwa akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi katika ufunguzi wa mkutano wa wadau wa kitaifa wa maandalizi ya mkutano mkubwa wa wadau wa huduma za setilaiti barani Afrika (14th Eumetsat User Forum in Africa) unaotarajiwa kufanyika Jijini Dar es salaam mwezi Septemba 2020. 






Wadau kutoka sekta mbalimbali wakichangia mada katika mkutano wa wadau wa kitaifa wa maandalizi ya mkutano mkubwa wa wadau wa huduma za setilaiti barani Afrika (14th Eumetsat User Forum in Africa) unaotarajiwa kufanyika Jijini Dar es salaam mwezi Septemba 2020.





Washiriki wakifuatilia kwa umakini mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa  katika mkutano wa wadau wa kitaifa wa maandalizi ya mkutano mkubwa wa wadau wa huduma za setilaiti barani Afrika (14th Eumetsat User Forum in Africa) unaotarajiwa kufanyika Jijini Dar es salaam mwezi Septemba 2020.
Washiriki wa mkutano katika picha ya pamoja na mgeni rasmi Dkt. Hamza Kabelwa ambaye pia ni Mkurugenzi wa huduma za Utabiri wa TMA aliyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi katika mkutano wa wadau wa kitaifa wa maandalizi ya mkutano mkubwa wa wadau wa huduma za setilaiti barani Afrika (14th Eumetsat User Forum in Africa) unaotarajiwa kufanyika Jijini Dar es salaam mwezi Septemba 2020.



Dar es salaam, 24 Januari 2020.

Dr. Hamza Kabelwa ambaye ni Mkurugenzi wa huduma za utabiri wa hali ya hewa wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TMA ambaye pia ni Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), Dkt. Agnes Kijazi amefungua mkutano wa wadau wa kitaifa wa maandalizi ya mkutano mkubwa wa wadau wa huduma za setilaiti barani Afrika unaotarajiwa kufanyika Jijini Dar es Salaam mwezi Septemba 2020 (14th EUMETSAT User Forum in Africa).

Katika hotuba ya ufunguzi aliyoiwasilisha kwa niaba ya Dkt. Kijazi aliwashukuru waandaaji wa mkutano huo ambao ni taasisi ya utafiti ya Ulaya (European Organization for the Exploration of Meteorological Satellite- EUMETSAT) kwa kuwezesha mkutano huo wa wadau wa maandalizi na juhudi wanazofanya katika kujenga daraja kati ya watoa huduma (EUMETSAT na TMA) pamoja na watumiaji wa huduma za Setilaiti zinazohusiana na hali ya hewa kwa nchi wanachama wa Shirika la Hali ya Hewa Barani Afrika.

“Napenda kuishukuru taasisi ya EUMETSAT ilivyoshirikiana na TMA, kuwakutanisha wataalamu kutoka sekta mbalimbali pamoja na Wizara kuja kwenye mkutano huu wa wadau wa maandalizi ya mkutano wa 14 wa EUMETSAT kwa wadau wa Bara la Afrika “(National Preparatory Workshop for the 14th EUMETSAT User Forum in Africa)”, pia nawashukuru EUMETSAT kwa mchango wenu mkubwa katika kutoa huduma za uangazi ambazo zinatumika katika utabiri wa hali ya hewa wa kila siku na ufuatiliaji wa hali ya mazingira; ikizingatiwa pia kuwa mimi ni Mwenyekiti wa Kamati ya WMO ya kuongeza uwezo wa Nchi Wanachama wa WMO katika kuboresha huduma za hali ya hewa “Capacity building”, alisema Dkt. Kabelwa kwa niaba ya Dkt. Kijazi.

Dkt. Kabelwa aliwakumbusha wadau kuwa Bara la Afrika linakabiliana na changamoto za kutokuwa na taarifa za kutosha za uangazi wa hali ya hewa na mazingira ambazo ni muhimu sana katika kufanya maamuzi, hivyo akawahimiza wadau wa mkutano kushiriki kwa wingi katika mkutano wa wadau wa Septemba 2020 ikiwa ni pamoja na kuwa mstari wa mbele katika maandalizi yake ili ufanyike kwa ufanisi na kwa heshima ya Tanzania. 

Aidha, wadau wa mkutano huu wa maandalizi waliwasilisha mada zilizoonesha uzoefu wao katika matumizi ya huduma zitolewazo na EUMETSAT hususan namna wanavyoshiriki katika miradi ya kikanda ya ufuatiliaji wa hali ya hewa na mazingira ambayo inalenga kuboresha huduma za hali ya hewa na mazingira katika nyanja kuu nne (4) ambazo ni ufuatiliaji wa matukio ya ukame, matukio ya mafuriko, matukio ya moto na kilimo. Taarifa hizi ni za muhimu sana katika maendeleo ya kijamii na uchumi wa nchi yetu.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...