Saturday, October 25, 2025

MWENENDO WA KIMBUNGA “CHENGE” KATIKA ENEO LA KUSINI MAGHARIBI MWA BAHARI YA HINDI

 


Dar es Salaam, 25 Oktoba, 2025 Mchana:

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoataarifa ya mwenendo wa Kimbunga “CHENGE katika Bahari ya Hindi, Kaskazini mwa Kisiwa cha Madagascar

 

Kimbunga “CHENGE” kimeendelea kusalia baharini nakusogea kuelekea magharibihuku kikipungua nguvu yake. Hadi asubuhi ya leo kilikuwa katika eneo la Bahari umbali watakribani kilometa 1,280 Mashariki mwa pwani ya kisiwa cha Mafia.

 

Uchambuzi wa mifumo ya hali ya hewa unaonesha kuwaKimbunga hicho kinatarajiwa kuendelea kusogea kuelekeaMagharibi zaidi mwa Bahari ya Hindi ulipo ukanda wa pwaniwa nchi yetu huku kikiendelea kupungua nguvu yake kadrikinavyosogeaHali hiyo inatarajiwa kusababisha uwezekanomdogo wa ongezeko kidogo la kasi ya upepo na mawimbimakubwa ya Bahari kati ya tarehe 26 hadi 28 ya Mwezi Oktoba, 2025 kwa maeneo ya ukanda wa pwani ya nchi yetuVilevileupo uwezekano mdogo wa vipindi vichache vya mvua kubwa kujitokeza hususani katika maeneo ya visiwa vyaUnguja na Pemba pamoja na mikoa ya Morogoro, Pwani, Dar es salaam na Tanga na maeneo jirani katika kipindi hicho cha tarehe 26 na 28 ya Mwezi Oktoba 2025.

 

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendeleakufuatilia mwenendo wa kimbunga CHENGE na athari zakekwa mifumo ya hali ya hewa hapa nchini na itaendelea kutoataarifa kila inapobidi.

 

USHAURI: Watumiaji wa Bahari na wananchi kwa ujumlawanashauriwa kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania pamoja na kupata ushauri na miongozo ya wataalam wakisekta.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...