Thursday, September 1, 2022

DKT KIJAZI AWAHIMIZA WANAHABARI KUTOA UTABIRI ULIOSAHIHI KWA JAMII.

 

Mgeni rasmi na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) Dkt Agnes Kijazi, Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa wanahabari  wa Utabiri wa Mvua za Vuli 2022 katika Ukumbi wa TARI, Kibaha, Tarehe 31/08/2022.

Kaimu Mkurugenzi wa kituo kikuu cha utabiri cha TMA Dkt. Mafur Kantamla akiongea na wanahabari katika Mkutano wa wanahabari  wa Utabiri wa Mvua za Vuli 2022 katika Ukumbi wa TARI, Kibaha, Tarehe 31/08/2022

 

 Meneja Mitambo na miundombinu  wa TMA  Ndugu. Samwel Mbuya akiongea na wanahabari katika Mkutano wa wanahabari  wa Utabiri wa Mvua za Vuli 2022 katika Ukumbi wa TARI, Kibaha, Tarehe 31/08/2022.







Matukio katika picha wakati waandishi wakisikiliza mada mbalimbali zilizowasilishwa katika Mkutano wa wanahabari  wa Utabiri wa Mvua za Vuli 2022 katika Ukumbi wa TARI, Kibaha, Tarehe 31/08/2022. 

Waandishi kutoka vyombo mbalimbali katika picha ya pamoja na mgeni rasmi katika katika Mkutano wa wanahabari  wa Utabiri wa Mvua za Vuli 2022 katika Ukumbi wa TARI, Kibaha, Tarehe 31/08/2022. Utabiri huo unatarajiwa kutolewa rasmi Tarehe 02 Septemba,2022 katika ukumbi wa mikutano wa TMA, Ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza - Dar es Salaam, Tanzania.

 

Tarehe 31 Agosti, 2022; Kibaha

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) Dkt Agnes Kijazi, amewataka wanahabari kutoa taarifa za hali ya hewa kwa jamii zilizosahihi  haswa kwa maeneo ya ziada ya kisekta kutoka kwa wataalamu ili taarifa iweze kuifikia jamii kwa ukamilifu. Aliyasema hayo wakati akifungua rasmi Mkutano wa wanahabari  wa Utabiri wa Mvua za Vuli 2022 katika Ukumbi wa TARI, Kibaha, Tarehe 31/08/2022.

“Napenda kuwakumbusha kufikisha taarifa hizi kwa usahihi na kutafuta, kupata na kuwasilisha ufafanuzi na maeneo ya ziada ya kisekta kutoka kwa wataalamu ili taarifa iweze kuifikia jamii kwa ukamilifu”. Alisema Dkt. Kijazi

Dkt.Kijazi alisema kuwa taarifa  za hali ya hewa zilizo sahihi na za uhakika zitaisaidia jamii kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya hali ya hewa. Pia zitazisaidia Mamlaka zinazohusika kupanga mipango ya kukabiliana na majanga yatokanayo na hali mbaya ya hewa, upatikanaji wa chakula na lishe bora pamoja na afya kwa ustawi wa jamii na hivyo kuchangia katika maendeleo endelevu.

Aidha, wakati akiendelea kusema hayo, aliongezea kuwa kupatikana kwa utabiri wa msimu wa Vuli 2022 kwa usahihi na kwa wakati kutachangia katika jitihada za seriakali ya awamu ya sita katika kukuza uchumi wa mwananchi mmoja mmoja, nchi kwa ujumla pamoja na kuboresha miundombinu na huduma za kijamii hapa nchini.

Kwa upande wake David Gumbo, mwandishi kutoka EATV akizungumza kwa niaba ya waandishi aliipongeza Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania kwa kutoa ushirikiano mzuri kwa vyombo vya habari ambao umesaidia kutoa taarifa za hali ya hewa zilizo sahihi na kwa wakati kwa jamii.

Katika Mkutano huo, wahabari  walipata fursa ya kuona rasimu ya utabiri wa hali ya hewa katika kipindi cha mwezi Oktoba hadi Desemba 2022  na kujadili na kupata uelewa wa pamoja ili kurahisisha uwasilishwaji wa utabiri huu kwa jamii kwa ufanisi na katika lugha inayoeleweka kirahisi pindi utakapotolewa rasmi Tarehe 02 Septemba,2022.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...