Monday, March 28, 2022

MWENENDO WA MVUA NCHINI.

 


Dar es Salaam, 28 Machi, 2022:

Mvua za Masika, 2022 katika maeneo yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka (Ukanda wa Ziwa Victoria, nyanda za juu kaskazini na pwani ya kaskazini) zilianza kunyesha wiki ya tatu(3) na ya nne(4)ya mwezi Februari 2022 katika maeneo mengikama zilivyotarajiwa. Hata hivyo, vimejitokeza vipindi virefu vya ukavu kati ya wiki ya kwanza na ya tatu yamwezi Machi, 2022 hususan kwa baadhi ya maeneo ya nyanda za juu kaskazini mashariki na ukanda wa pwani ya kaskazini.Vipindi hivyo virefu vya ukavu vimesababishwa na matukio ya vimbunga hususan kimbunga Gombe kilichodumu kwa muda mrefu katika Bahari ya Hindi eneo laRasi ya Msumbiji pamoja na kujitokeza kwa joto la bahari la chini ya wastani katika eneo la pwani ya Afrika Mashariki.Hali hiyo imechangia pia Ukandamvua (ITCZ) kuendelea kusalia katika maeneo ya kusini mwa nchi ambapo kwa kawaida katika kipindi cha mwanzoni mwa mwezi Machi huanza kuelekea maeneo ya kaskazini mwa nchi.

Hata hivyo, unyeshajiwamvua unatarajiwa kuimarikakatikabaadhi ya maeneomwishoni mwa mwezi Machi, 2022na mwanzoni mwa mwezi Aprili,2022 na kufuatiwa na upungufu kati ya wiki ya kwanza na ya pili ya mwezi Aprili, 2022hususani kwa maeneo ya nyanda za juu kaskazini mashariki na pwani ya kaskazini.

Kwa upande mwingine, kusalia kwa Ukandamvua katika maeneo ya kusini kumesababishamvua za Msimu kuendelea kunyesha kwa kiwango cha kuridhisha katika baadhi ya maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua kwa mwaka (magharibi mwa nchi, kanda ya kati, nyanda za juu kusini magharibi, Ruvuma pamoja na maeneo ya kusini mwa mkoa wa Morogoro).

Wananchi wanashauriwa kuendelea kuzingatia taarifa na tahadhari za hali ya hewa zilizotolewa na zitakazotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania sambamba na kutafuta, kupata na kufuata ushauri wa wataalam katika sekta husika ili kupunguza athari zinazotokana na hali mbaya ya hewa.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...