Thursday, January 28, 2021

WANANCHI WA BAGAMOYO NA TANGA WAFURAHISHWA NA JUHUDI ZA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA.






Bagamoyo - Tanga, Tarehe 19 Januari, 2021.

Mamlaka ya Hali ya hewa Tanzania imekutana na wadau kutoka sekta ya uvuvi pamoja na wananchi kwa ujumla ambapo lengo la kukutana na wadau hao ni kutoa uelewa wa taarifa za hali ya hewa pamoja na kuwapa njia mbalimbali ambazo wanaweza kutumia ili kupata kirahisi taarifa za hali ya hewa. Mkutano huo ulifanyika katika Bandari ya Bagamoyo, Bandari Tanga pamoja na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kuanzia tarehe 15 mpaka 19 Januari, 2021.

Warsha hiyo iliandaliwa na TMA na kufadhiliwa na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (World Meteorological Organization – WMO), chini ya mwamvuli wa Programu ya kidunia ya kuwaongezea ujuzi waandaaji na watumiaji wa taarifa za hali ya hewa barani Afrika (Weather and Climate Information Services for Africa - WISER).

 

Washiriki walikumbushwa kuwa Mamlaka ya Hali Ya Hewa inatoa huduma zake kwa ajili ya usalama wa watu na mali zao hivyo kila mmoja anawajibu wa kuhakikisha kua anafatilia taarifa hizo ili kuepukana na majanga yanayoweza kutokea.

Aidha, wakati wa mkutano huo, mambo mbali mbali yalijadiliwa ikiwa ni pamoja na uwelewa wa taarifa za hali ya hewa, uandaaji wa taarifa za hali ya hewa za muda mfupi, wa kati na mrefu, usambazaji wa taarifa za hali ya hewa, uandaaji wa taarifa za hali ya hewa kwenye maeneo madogo na mipaka ya matumizi ya taarifa husika pamoja na kupokea mirejesho ya wadau juu ya matumizi ya taarifa za hali ya hewa kwenye maeneo.

Kwa upande wa washiriki walishukuru na kufurahishwa sana na Mamlaka kwa juhudi walizozichukua katika kutoa tofauti, pamoja na kuongeza thamani kwa wadau kuweka ushauri na madhara yanayo tarajiwa kwenye taarifa za hali ya hewa zilizo boreshwa. Wakatoa mapendekezo yao kuwa kuwepo na mikutano ya namna iyo mara kwa mara ili wananchi wengi waweze kufikiwa kwa wakati na kuwafikishia taarifa za sahihi.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...