Wednesday, April 17, 2019

TMA YAPATA MAFUNZO YA KUTUMIA MFUMO WA SERIKALI WA KIELEKRONIKI KATIKA UKUSANYAJI WA MAPATO YA SERIKALI (GePG)).


Washiriki wa mafunzo ya kutumia mfumo wa serikali wa kielektroniki katika ukusanyaji wa mapato katika picha ya pamoja na mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya hali ya hewa dkt. Agnes Kijazi (katika ya waliokaa)
Matukio mbalimbali katika picha wakati wafanyakazi wa TMA wakipata mafunzo ya kutumia mfumo wa serikali wa kielektroniki katika ukusanyaji wa mapato ya serikali (GePG).

12/04/2019; DAR ES SALAAM

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imepata mafunzo ya kutumia mfumo wa serikali wa kielektroniki katika ukusanyaji wa mapato ya serikali (GePG) ikiwa niutelezaji wa sheria ya fedha za umma, sura 348 iliyopitishwa na bunge kifungu cha 44 cha mwaka 2017.

Akizungumza wakati wa kuhitimisha mafunzo hayo, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dkt. Agnes Kijazi alieleza kuwa mafunzo hayo ni mwendelezo wa juhudi za Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) katika kutekeleza maelekezo yote yanayotolewa na Serikali inayoongozwa na mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa lengo la kuongeza tija na ufanisi katika utoaji huduma bora kwa umma. Alisisitiza kwamba mafunzo hayo yataiwezesha Mamlaka kuboresha njia za ukusanyaji wa mapato na hivyo kutoa huduma bora kwa wananchi.

Kwa upande wa washiriki wa mafunzo hayo, meneja wa fedha na uhasibu Bw. Michael Ntagazwa alieleza faida za mfumo huo kuwa ni kuboresha utendaji kazi ikiwa pamoja na urahisi katika kuandaa na kupata taarifa za mapato kwa vituo vyote na kwa wakati wowote.

Naye mtaalam kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Jane Kazoba alieleza kuwa mfumo huo umeunganishwa na ofisi mbalimbali zinazokusanya mapato ya serikali zikiwemo wizara na taasisi zake na taasis zinazotoa huduma za fedha nchini.

Imetolewa:
Ofisi ya Uhusiano
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...