Thursday, October 18, 2018

MVUA ZA MSIMU: TMA YATOA UTABIRI KWA MAENEO YANAYOPATA MSIMU MMOJA WA MVUA

Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania(TMA) dkt. Agnes Kijazi, mbele ya waandishi wa habari  akichambua  mwenendo wa mifumo ya hali ya hewa na mwelekeo wa mvua za Msimu kwa maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua
Wajumbe wa bodi ya ushauri wa Mamlaka (TMA) wakiongozwa na mwenyekiti wa bodi hiyo dkt. Buruhani Nyenzi wakifuatilia uchambuzi wa mwenendo wa mifumo ya hali ya hewa na mwelekeo wa mvua za Msimu kwa maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua.
Baadhi ya waandishi walioshiriki mkutano wa wanahabari wa kutoa mwelekeo wa mvua za Msimu kwa maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua


Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa rasmi utabiri wa msimu kuanzia mwezi Novemba, 2018 hadi Aprili, 2019 katika mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika katika Ofisi za TMA. Mkutano huo uliudhuriwa na wajumbe wa Bodi ya Ushauri wa TMA wakiongozwa na mwenyekiti wa Bodi hiyo Dkt. Buruhani Nyenzi
Taarifa hiyo inatoa uchambuzi wa mwenendo wa mifumo ya hali ya hewa na mwelekeo wa mvua za Msimu kwa maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua (kanda ya magharibi, kati, nyanda za juu kusini magharibi, kusini mwa nchi, ukanda wa pwani ya kusini pamoja na maeneo yaliyoko kusini mwa mkoa wa Morogoro) katika kipindi cha miezi ya Novemba, 2018 hadi Aprili, 2019. Aidha, taarifa imeendelea kwa kutoa mrejeo wa mvua za Vuli katika maeneo ya ukanda wa ziwa Victoria, pwani ya kaskazini na nyanda za juu kaskazini-mashariki.
Vile vile, ushauri na tahadhari umetolewa kwa wadau wa sekta mbali mbali wanaotumia taarifa za hali ya hewa katika utekelezaji wa majukumu yao kama vile kilimo na usalama wa chakula, mifugo na wanyamapori, maliasili na utalii, uchukuzi na mawasiliano, nishati na maji, mamlaka za miji, afya pamoja na menejimenti za maafa. Kusoma zaidi ingia humu http://www.meteo.go.tz/pages/climate-outlook-for-msimu-rains-nov-2018-apr-2019


No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...