Wednesday, June 13, 2018

MAMLAKA YA HALI YA HEWA SIERRA LEONE YAFANYA ZIARA YA MAFUNZO KATIKA OFISI ZA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA

Ujumbe kutoka Sierra Leone katika ukumbi wa mkutano wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano walipokutana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Uchuuzi)  Dkt. Leonard Chamuriho, wajumbe hao waliambatana na wenyeji wao kutoka TMA wakati wa  ziara yao ya mafunzo


Kaimu Mkurugenzi Mkuu-TMA, Dkt. Pascal Waniha akifafanua jambo kwa ujumbe kutoka Sierra Leone, Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Bw. Usman Banya (Tai ya Bluu), Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Sierra Leone Bw. Ibrahim S. Kamara na Bw. Moses Baiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Sierra Leone wakati walipokutana na menejiment ya TMA katika ziara yao ya mafunzo.
 
Ujumbe kutoka Sierra Leone katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) Bw. Hamza Johari walipomtembelea katika ofisi yake wajumbe hao waliambatana na wenyeji wao kutoka TMA wakati wa  ziara yao ya mafunzo
 
Ujumbe kutoka Sierra Leone  wakipata maelezo ya uandaaji wa utabiri kutoka kwa Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri, Dkt. Hamza Kabelwa wakati wa  ziara yao ya mafunzo
Ujumbe kutoka Sierra Leone wakipata maelezo ya uandaaji wa taarifa za hali ya hewa hatarishi (severe weather) kutoka kwa mtaalam wa hali ya hewa Bw. Abuubakari wakati wa  ziara yao ya mafunzo
 
 
 
Ujumbe kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Sierra Leone umefanya ziara katika ofisi za TMA, lengo likiwa ni kujifunza namna bora ya utoaji huduma za hali ya hewa kwa jamii ili kuboresha huduma zao. Ujumbe huo uliambatana na  Katibu Mkuu wa Wizara ya uchukuzi anayesimamia huduma za hali  ya hewa nchini Sierra Leone, Mkurugenzi Mkuu kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Sierra Leone na wajumbe wengine wa nne kutoka Mamlaka ya Usafiri wa Anga, kitengo cha Maafa na kitengo cha huduma za maji. Wajumbe walipata fursa ya kuonana na Katibu Mkuu wa Uchukuzi na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania.
 

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...