Saturday, August 9, 2025
TMA YANYAKUA KOMBE MAONESHO YA NANE NANE 2025.
Thursday, August 7, 2025
VIONGOZI WAKUMBUSHWA KUHAMASISHA WANANCHI KUTUMIA TAARIFA ZA TMA
Wednesday, August 6, 2025
ELIMU YA HUDUMA MAHUSUSI ZA HALI YA HEWA ZAWAVUTIA WENGI NANENANE MOROGORO
Monday, August 4, 2025
TMA YATUMIA FURSA YA MAONESHO YA NANENANE KUTOA ELIMU KWA JAMII
Dodoma, 03 Agosti 2025
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetumia fursa ya Maonesho NaneNane 2025 Kitaifa yanayofanyika katika Viwanja vya Nzuguni, Dodoma kutoa elimu kwa jamii kuhusu huduma zitolewazo pamoja na jukumu kubwa la TMA la kudhibiti shughuli za hali ya hewa nchini.
Kupitia maonesho haya, wananchi na wadau mbalimbali wakiwemo wakulima, wavuvi na wafugaji wamepata elimu ya moja kwa moja kutoka kwa wataalamu wa TMA wakiwemo viongozi.
TMA imeeleza namna taarifa za hali ya hewa zinavyokusanywa, kuchakatwa na kuchambuliwa kupitia mifumo ya kisasa, na jinsi huduma hizo zinavyoweza kusaidia jamii.Aidha, TMA imeeleza umuhimu wa kuendesha shughuli za hali ya hewa zenye kukidhi viwango vya kitaifa na kimataifa.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA ,Dkt.Ladislaus Chang'a na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC), akiwahudumia wateja kwenye Banda la Mamlaka aliwahimiza wadau wote kufuatilia utabiri wa kila siku, utabiri wa msimu pamoja na tahadhari za hali mbaya ya hewa, huku akisisitiza matumizi sahihi ya taarifa hizo katika shughuli zote za kiuchumi na kijamii.
Aidha, aliishukuru Serikali kwa kuendelea kuwekeza katika miundombinu ya hali ya hewa na rasilimali watu na hivyo kuleta maendeleo makubwa ya utendaji kazi wa Mamlaka.
Mamlaka ya Hali ya HewaTanzania inashiriki katika maonesho ya NaneNane Dodoma, Zanzibar, Mbeya na Morogoro.Kauli Mbiu ya mwaka huu ni “Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi 2025”.
Featured Post
DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.
Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...
-
DODOMA; Tarehe 19 Agosti, 2024; Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imekutana na wadau kutoka sekta mbalimbali nchini ili kujipanga na...
-
Dar es Salaam, 22 /0 8 /202 4 ; Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa utabiri wa msimu wa mvua za VULI 202 4 kwa maeneo yanayopat...
-
Dar es Salaam, Tarehe 30/01/2025 Katika kuboresha ufanisi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),Taasisi ya Uongozi imetoa mafunzo ya sik...