Wednesday, April 24, 2019

KIMBUNGA KENNETH



23/04/2019

Taarifa hii inatoa mrejeo wa mwenendo wa mifumo ya hali ya hewa katika bahari ya Hindi na athari zake kwa maeoneo mbalimbali hapa nchini.

Mifumo ya hali ya hewa inaonesha kuendelea kuimarika kwa mgandamizo mdogo wa hewa uliopewa jina la “Kenneth” katika eneo la kaskazini magharibi mwa kisiwa cha Madagasca ambao unambatana na mvua kubwa na upepo mkali katika eneo hilo. Mgandamizo huo unaendelea kusababisha mawingu mazito na ongezeko la mvua katika maeneo mengi hapa nchini hususan katika maeneo ya kanda ya ziwa Victoria, nyanda za juu kaskazini mashariki na ukanda wa pwani. Aidha, vipindi vya upepo mkali unaofikia kasi ya kilometa 40 kwa saa vimeendelea kujitokeza katika ukanda wa pwani kama ilivyotabiriwa na vinatarajiwa kuendelea. Hata hivyo, pamoja na kuendelea kuimarika kwa mgandamizo huo bado haujafika kiwango cha kimbunga kamili na upo umbali wa takribani kilometa 1000 mashariki mwa Mtwara. Inatarajiwa kuwa Mgandamizo huo utaendelea kuimarika kwa kasi na kufikia kiwango cha kimbunga kamili “Kenneth” kati ya tarehe 25 na 26 April 2019 na kuendelea kutawala mwenendo wa Mifumo ya hali ya hewa hapa nchini.

Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania inaendelea kufuatilia mwenendo wa kujengeka kwa mfumo huo uliopo kusini magharibi bahari ya Hindi pamoja na mwenendo wa mifumo mingine ya hali ya hewa kwa ujumla na itatoa taarifa za mrejeo kila itakapobidi.

USHAURI: Wananchi wanashauriwa kuendelea kufuatilia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania na kuzingatia tahadhari zilizotolewa na mirejeo yake pamoja na kupata na kuzingatia ushauri na miongozo ya wataalam katika sekta husika ili kupunguza athari zinazoweza kujitokeza.

Imetolewa na:
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...