Tuesday, December 16, 2025

MAFUNZO YA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO KWA MENEJIMENTI YA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA

 MAFUNZO YA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO KWA MENEJIMENTI YA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA 











Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya hewa Tanzania (TMA) na Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika Shirika la Hali ya Hewa Duniani(WMO), Dkt. Ladislaus Chang'a  alifungua  mafunzo ya usimamizi wa miradi ya  maendeleo kwa menejimenti ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) yanayoendeshwa na Chuo Cha Uhasibu Arusha (IAA),  ambapo mafunzo hayo yamejikita zaidi  katika usimamizi wa miradi ya uwekezaji wa miundombinu kama “Capital Expenditure (CapEx)”.


 Dkt. Chang'a katika ufunguzi alisema kuwa TMA ikiwa ni Taasisi ya Serikali  iliyopewa majukumu ya kutoa huduma za hali ya hewa, kuratibu na kudhibiti shughuli zote zinazohusiana na masuala ya hali ya hewa nchini. Mamlaka inashiriki pia kutekeleza miradi mbalimbali yenye malengo yanayochangia kufanikisha utekelezaji wa majukumu ya TMA ya kitaifa, kikanda na kimataifa.


Aidha, alieleza kuwa miongoni mwa miradi ambayo inatekelezwa na TMA ni ikiwemo miradi ya uwekezaji wa miundombinu mbalimbali “Capital Expenditure (CapEx)”, Ujenzi wa Kituo cha Ufuatiliaji wa matukio ya Tsunami (Tsunami Centre), TMA inapata ufadhili wa kujenga vituo vipya vitatu (3) vya kupima hali ya hewa katika anga za juu kupitia mradi wa (SOFF) na nyinginezo nyingi. 


Kwa upande wake Mtiva wa Kitivo cha Mafunzo ya Insia na Sayansi za Jamii, Dkt. Leticia Rwabishungi wa chuo Cha Uhasibu Arusha aliwashukuru sana  TMA kwa kufika  IAA kwa mafunzo  ya usimamizi wa miradi na kusema chuo kina kozi nyingi sio tu Uhasibu bali kozi mbalimbali na kwa ngazi zote hivyo aliwakaribisha kuendelea kupata mafunzo katika chuo cha IAA.


Mojawapo ya walioshiriki katika ufunguzi wa mafunzo hayo ni  Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, Mkurugenzi wa Huduma za Ushauri wa Chuo cha IAA,  Menejimenti ya Mamlaka ya Hali ya Hewa, Wakufunzi kutoka Chuo cha IAA, Wataalamu mbalimbali kutoka TMA, IAA na UNDP.


Mafunzo haya yameanza Disemba 15 mpka 19, mwaka 2025.

TMA YAPONGEZWA KWA KUIMARISHA IMANI YA WATANZANIA KUPITIA TAARIFA SAHIHI ZA HALI YA HEWA





Arusha 15 Disemba 2025,

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ilipata fursa adhimu ya kutembelewa na Naibu Waziri wa Uchukuzi, Mheshimiwa David Kihenzile(MB), katika Mkutano Mkuu wa 18 wa Tathmini ya Utendaji wa Sekta ya Uchukuzi. Mkutano huo ulifanyika katika Ukumbi wa AICC, Jijini Arusha.

Katika mkutano huo, Mheshimiwa Naibu Waziri aliipongeza Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania kwa mchango wake mkubwa katika utoaji wa taarifa sahihi na za kuaminika za hali ya hewa, ambazo zimeendelea kusaidia kuboresha usalama na ufanisi katika sekta ya uchukuzi na kuwa taasisi yenye kuaminiwa na Watanzania.

Mkutano huo unafanyika kwa muda wa siku tatu, kuanzia tarehe 15 - 17 Desemba 2025 na kuwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya uchukuzi.

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...